Dereva wa Daladala aliyemuua mkewe Dar kisha kukimbia, akamatiwa Lindi

Dereva wa Daladala aliyemuua mkewe Dar kisha kukimbia, akamatiwa Lindi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemkamata Maarifa Hadith Matala (45), Dereva wa daladala, mkazi wa Kimara Suka Golani Wilaya ya Ubungo kwa tuhuma za mauaji ya mpenzi wake, Sharifa Twaha Nyamaishwa (31), Kondakta wa Daladala aliyekuwa mkazi wa Kimara Suka Golani Wilaya ya Ubungo.

Inadaiwa Maarifa alimshambulia sehemu mbalimbali za mwili mpenzi wake huyo na kusababisha kifo chake, tukio hilo limetokea tarehe 16 Agosti 2022 huko maeneo ya Kimara Suka, na mara baada ya tukio hilo mtuhumiwa alitoweka.

Jeshi la Polisi baada ya kupata taarifa hiyo lilianza upelelezi na ufuatiliaji wa haraka na kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa Mkoani Lindi alipokuwa amejificha.

Uchunguzi wa awali umebaini kuwa wapenzi hao walikuwa na migogoro inayosababishwa na wivu wa kimapenzi na kupelekea kugombana mara kwa mara, na mwili wa marehemu ulikutwa na majeraha.

Uchunguzi wa shauri hili unakamilishwa na mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo baada ya tuhuma hizo za kikatili uliovuka kiwango.
 
Yaan Aliya Jana akakimbilia Lind haraf leo kakamatwa ?? Sasa alijifichaje yaan unakamatwa mapema hivi?

Mapenz haya yatatumaliza tuspokuwa makini, hasa hasa cm znachangia Sana kugombanisha na kusababisha migogoro na vifo kwa wanandoa!!

Zaman sm hazkuwepo na ndoa zlikuwa na aman, kwa hyo wanandoa tuwen Makin na cm zetu
 
Yaan Aliya Jana akakimbilia Lind haraf leo kakamatwa ?? Sasa alijifichaje yaan unakamatwa mapema hivi?? Mapenz haya yatatumaliza tuspokuwa makini, hasa hasa cm znachangia Sana kugombanisha na kusababisha migogoro na vifo kwa wanandoa!! Zaman sm hazkuwepo na ndoa zlikuwa na aman, kwa hyo wanandoa tuwen Makin na cm zetu
Umezungumza pointi.
 
Yaan Aliya Jana akakimbilia Lind haraf leo kakamatwa ?? Sasa alijifichaje yaan unakamatwa mapema hivi?? Mapenz haya yatatumaliza tuspokuwa makini...
Mkuu simu mnazisingizia tu. Watu wangekuwa waaminifu wala kusingekuwa na shida. Sema simu zinasababisha watu kushikwa (Kwa sababu ya kupekuliana simu). Unadhani zamani watu walikuwa hawapigani miti nje ya ndoa?

Ilikuwa sana tu ila ilikuwa hawashikwi vile hamna viushahidi. Wanakutana njiani wanenda fanya yao kisha wanapanga tukutane jumatano ijayo saa tisa na robo hapa hapa, fullstop!

Sasa siku hizi jitu linakula mke wa mtu na kila saa linamtumia msg umekula, umevaaje leo? Nakumiss baridi hii!
 
Back
Top Bottom