Dewji: Biashara yangu ya kwanza nilikuwa nauza Mafuta ya Taa, Baba yetu alikufa masikini

Dewji: Biashara yangu ya kwanza nilikuwa nauza Mafuta ya Taa, Baba yetu alikufa masikini

Azim dewji ni ndugu yake Gulamabbas dewji. Huyo Gulamabbas ndio Baba yake Mo Dewji. Huyo Gulam ndio muanzilishi wa hiyo kampuni ya familia ya akina Mo. Hao ndio waanzilishi wenye mzigo wenyewe, huyo Mo kaikutia kampuni katikati. Wengine wanasema Mo ni msimamizi wa mali, wengine wanasema Mo ni muuza duka tu.
Ninavyojua Azim na Gulam ni mtu na mdogo wake toka nitoke. Na Mo anamuita Azim Baba mdogo kwa maana ni mdogo wa Gulam ambaye Baba yake Mo
 
Mwl Nyerere aliamua,watz asili ya Asia wawe matajiri kuliko wazawa!!

Dr.Reginald Mengi aliandika kwenye kitabu chake Cha I can,I must and I Will!

Ndio maana matajiri wanaoeleweka hapa tz no hao waaarabu na wahindi !sisi wamatumbi hata ufanyaje utaanguka tu!!

Vuta picha top five yote ni hao tu!

Nadhani
 
Mwl Nyerere aliamua,watz asili ya Asia wawe matajiri kuliko wazawa!!

Dr.Reginald Mengi aliandika kwenye kitabu chake Cha I can,I must and I Will!

Ndio maana matajiri wanaoeleweka hapa tz no hao waaarabu na wahindi !sisi wamatumbi hata ufanyaje utaanguka tu!!

Vuta picha top five yote ni hao tu!

Nadhani
Hiyo historia nishawahi kusikia. Wanasema nchi nyingi za kiafrika zilivurugika baada ya wamatumbi kuwa na hela na kuamua kufadhili waasi kivita au kupindua viongozi. Labda mwalimu aliogopa kupinduliwa
 
Gari yako ya kwanza ulienda Kukopa, ulikopa Wapi...!? Kwa dhamana gani....!?

Ulikopa Gari then ndo ukaanza biashara yako ya kwanza kuuza Mafuta ya Taa...!

Nyie hamkua Masikini, story za aina hii hazimsaidii ama kum motivate Masikini, ambaye hawezi hata kukopesheka kwa Pikipiki....!

Mimi nataka kusikia kama hivi....!

Nilichukua Gunia 3 za mahindi ambazo nilivuna baada ya kulima kwa mkono, Gunia 2 nikaenda kuuza, Gunia moja nikasaga Unga, nikanuua Mafuta, Dagaa, Panga, Shoka n.k.
Nikaenda msituni kukata miti na kuchoma mkaa, mkaa wangu wa kwanza kuchoma nikapata Gunia 15, nikauza nikapata laki 3, nikachoma tena mkaa nikapata laki 5...! Nikaenda wilayani kununua hiki na hiki, nikaenda kuuzachuku na huku n.k

Tunataka mifano halisi kama hii....!

Sio unatuambia tu Biashara ya kwanza ya Azam ilikua Bakery ya kutengeneza Mikate.....!

Alipata wapi pesa za kuanzisha kiwanda cha kutengeneza mikate hamsemi....!

Hatutaki hizo story.....! Tunataka mtiririko unaoeleweka tokea chini.
 
It's all about perception; As a Motivation to People well and good..., lakini kama msomaji kila ukiambiwa na mtu alichofanya usichukulie maneno anayokwambia kama ndio msaafu..... kuna Nuts and Bolts huwa hazisemwi....
Unawakumbuka wale wa vibubu?

Walivyokuja kuswendemwa maisha, ndo kila mtu alibakia ghaa!
 
Mfanyabiashara mkubwa nchini Azim Dewji, ameweka wazi kuwa biashara yake ya kwanza kuifanya ilikuwa ni kuuza mafuta ya Taa.

Akifanya mahojiano na CloudsTv Dewji amesema,

"Biashara yangu ya kwanza nilinunua gari kwa mkopo, nikawa na gari lakini tulikuwa tunanunua mafuta ya taa kwenye madebe tunapeleka vijijini kwenda kuuza, wale wanapata huduma sisi tunapata kipato, ndio biashara ya kwanza kufanya."-Azim Dewji

Kwa upande mwengine Dewji ameelezea maisha ya dhiki waliyokuwa wanaishi,

"Maisha yetu hayakuwa mazuri sana, baba alikuwa sio tajiri. Alikuwa mtu wa kipato cha kati lakini alifariki akiwa maskini kwa sababu alikuwa hapendi kukaa na mali. Alipokuwa anakuja mtu mwenye shida basi yeye alikuwa anampatia"-Azim Dewji

Written by Mjanja M1 [emoji3578]
Kitu cha kujifunza hapo huwezi kuwa tajiri kwa kupenda kusaidia kila mtu

Sent from my SM-A137F using JamiiForums mobile app
 
Familia nyingi za kiarabu walitajirika zamani tokana na uwindaji haramu/ujangili kipindi waTanganyika bado wamelala.

Uzuri wao wanajua kutunza mali na kurithishana kizazi hadi kizazi na mtindo wao wa kimaisha kuoana karibu karibu mali inakuwa haitoki nje.
 
Mfanyabiashara mkubwa nchini Azim Dewji, ameweka wazi kuwa biashara yake ya kwanza kuifanya ilikuwa ni kuuza mafuta ya Taa.

Akifanya mahojiano na CloudsTv Dewji amesema,

"Biashara yangu ya kwanza nilinunua gari kwa mkopo, nikawa na gari lakini tulikuwa tunanunua mafuta ya taa kwenye madebe tunapeleka vijijini kwenda kuuza, wale wanapata huduma sisi tunapata kipato, ndio biashara ya kwanza kufanya."-Azim Dewji

Kwa upande mwengine Dewji ameelezea maisha ya dhiki waliyokuwa wanaishi,

"Maisha yetu hayakuwa mazuri sana, baba alikuwa sio tajiri. Alikuwa mtu wa kipato cha kati lakini alifariki akiwa maskini kwa sababu alikuwa hapendi kukaa na mali. Alipokuwa anakuja mtu mwenye shida basi yeye alikuwa anampatia"-Azim Dewji

Written by Mjanja M1 ✍️
Mafuta ya taa yana rangi nyeupe?
 
Ninavyojua Azim na Gulam ni mtu na mdogo wake toka nitoke. Na Mo anamuita Azim Baba mdogo kwa maana ni mdogo wa Gulam ambaye Baba yake Mo

Sio kweli

Babu yake na Mo dewji na babu yake Azim dewji ndio walizaliwa tumbo moja.

Undugu wao wameupatia kwa babu zao. Na wala sio kwa baba zao
 
Mwl Nyerere aliamua,watz asili ya Asia wawe matajiri kuliko wazawa!!

Dr.Reginald Mengi aliandika kwenye kitabu chake Cha I can,I must and I Will!

Ndio maana matajiri wanaoeleweka hapa tz no hao waaarabu na wahindi !sisi wamatumbi hata ufanyaje utaanguka tu!!

Vuta picha top five yote ni hao tu!

Nadhani
Mbona Manjagata anadai yupo top 5?
 
Mfanyabiashara mkubwa nchini Azim Dewji, ameweka wazi kuwa biashara yake ya kwanza kuifanya ilikuwa ni kuuza mafuta ya Taa.

Akifanya mahojiano na CloudsTv Dewji amesema,

"Biashara yangu ya kwanza nilinunua gari kwa mkopo, nikawa na gari lakini tulikuwa tunanunua mafuta ya taa kwenye madebe tunapeleka vijijini kwenda kuuza, wale wanapata huduma sisi tunapata kipato, ndio biashara ya kwanza kufanya."-Azim Dewji

Kwa upande mwengine Dewji ameelezea maisha ya dhiki waliyokuwa wanaishi,

"Maisha yetu hayakuwa mazuri sana, baba alikuwa sio tajiri. Alikuwa mtu wa kipato cha kati lakini alifariki akiwa maskini kwa sababu alikuwa hapendi kukaa na mali. Alipokuwa anakuja mtu mwenye shida basi yeye alikuwa anampatia"-Azim Dewji

Written by Mjanja M1 [emoji3578]
Mtu anayetoa msaada kwa kila anayemjia sio masikini!

Sent from my moto g 5G (2022) using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom