Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

Alichosema pro safari ktk hoja yake ni kuwa,baadhi ya wanajamii wanakichukulia cdm kuwa ni chama cha udini(ukristo) na ukabila(chaga).yeye kasema anataka kiti hicho ili aieleze jamii kuwa chadema haikiko hivyo jinsi baadhi ya watu ktk jamii na hasa ccm kuwa chadema ni chama cha kitafa.sema tu waanzlishi wake wengi walikuwa ni kutika kilimanjaro.Ikumbukwe pia,dhana ya udina na ukabila zilipandikizwa na ccm ili kufifisha nguvu ya upinzani ambay n hatari kwa ustawi wa ccm.ikumbuwe pia cuf walipandikizwa dhana ya udini mwanzono mwa 2000.Tuwe tunasikilizwa hoja ya mtu anayoitoa na kuielewa vizuri na si kukurupuka mitaandaoni na kupost upumbavu.
 
Ndugu,
Hawa vijana wa BAVICHA kila siku ninawaambia kuwa, kazi waliyopewa ya kukitetea chama iko juu ya uwezo wao.

Kila wanalolisema ukiliangalia kwenye hoja fikirishi linaleta maswali mengi.

Inawezekana huyu kijana hafahamu kuwa anachokisema kinajenga hoja inayodhihirisha kuwa Prof. Safari ndiyo chaguo hasa anaposema sitafanikiwa kwa Prof. Safari kutochaguliwa.
Uchaguzi wamesha panga washindi hadi kule kanda ya ziwa! Chadema wana weweseka! Sijui kwanini wanaitisha uchaguzi?
Hata yule Mpemba wamempa ushindi kwa hofu!
 
Yani Prof Safari kwa kinywa chake anasema yeye ndio atakuwa tiba ya ugonjwa unao sumbua ndani ya chadema!
Ni wazi wamepanga kumpa kiti na hakukuwa na sababu ya kuitisha uchaguzi!
 
Umeanza vema, kwamba Safari ameanza safari na kachagua aina ya vipaumbele vyake ambavyo umenukuu. Mlolongo wote wa maelezo mengine ni mawazo yako binafsi. Ungekuwau umemtendea haki Safari kama ungemdodosa undani wa vipaumbele vyake badala ya kusema "ukiangalia kwa mapana. ........." unamsemea yasiyo yake
Ndugu,
Mimi sikutaka kudodosa vipaumbele vya kitaifa kwa sababu kila Mtanzania mwenye akili timamu anavifahamu.

Nilipenda kufahamu kilichoko ndani ya CHADEMA kutokana na mantiki ya hoja zake nikiwa kama mmoja wa wanaoiangalia CHADEMA wakiwa nje.
 
Ndugu Ritz,
Kwa hiyo una maanisha CHADEMA wanachofanya ni sawa na kupaka rangi ya nyumba kwa nje inayovutia wapita njia lakini kwa ndani kuna uchafu mwingi!
Ndugu yangu, wanachofanya Chadema ni sawa na kuziba shimo la panya kwa mkate wa nyama.
 
Licha ya kwamba Profesa Safari ametaja sababu za kugombea Umakamu Mwenyekiti, nadhani huyu msomi hakutafakari kwa umakini na kwa kina, eti anataka kukomesha Ukanda, Udini, Ubaguzi wa rangi au Ukabila na Kijinsia, Umaskini na Ujinga pamoja na Ubadhirifu.

Kwanza kuhusu Ukanda, CHADEMA kilianzishwa na Mtei wa Kanda ya Kaskazini, lakini kwa juhudi kubwa za huyu Muasisi, akisaidiwa na waliomrithi na wanachama wengine, kimeenea nchi nzima: Kigoma, Kagera, Mwanza, Mara, Mbeya, Iringa, Ruvuma, Mtwara, Lindi na mikoa yote ya Pwani, Kati na Kaskazini kwao Mtei.

Kuhusu Udini, yeye mwenyewe Muislamu, na mgombea uenyekiti taifa ni Mkristo. Anataka nini cha zaidi ya
kushirikisha dini zote? Labda CHADEMA washirikishe wasio na dini (atheists) zaidi?

Ukabila na Rangi haviko Chadema. Hata sijui kabila la Prof. Safari, na nikiwa mpiga kura katika jimbo lake, namhakikishia kura yangu. Ubaguzi wa kijinsia hauko kabisa CHADEMA. Uliza wakina mama wa Chama.

Umaskini, Ujinga na Maradhi vinatushinda sisibsote, kutokana na ufinyu wa fedha na zana za kukabiliana navyo. Hilo ni tatizo la kitaifa kwa chama chochote cha siasa, hata CCM chama tawala, licha ya kwamba Ubadhirifu na Rushwa vikitokomezwa tutamudu zaidi majukumu hayo.

Kwa hiyo kwa jumla, Profesa ni vema ujue matatizo na kiini chake. Nina hakika uongozi wa sasa wa CHADEMA utanufaika, endapo juhudi zako za kujiunga nao kama Makamu Mwenyekiti, zitafanikiwa. Kila la kheri.


Yani katika siku amabayo Prof Safari Kaimaliza chadema ni kwenye hiyo kauli na hapo kathibitisha kwa kinywa chake yale ambayo yamekuwa yakisemwa na wasio wana chadema!

Prof Safari ni mwana chadema kwa anajua vyema kinacho endelea ndani ya chadema na bila shaka hawezi kuropoka bila kufanya utafiti.
 
Uchuro huu kuitwa Ndugu na Intarahamwe
Ndugu,
Wewe niwa kupuuzwa tu kama ulivyo upuuzi wako.

Wewe unakuja kutoa michango yako kwa Interahamwe halafu unaanza kulalamika!. Huoni kuwa wewe ndiyo una matatizo kifikra.
 
Ndugu,
Wewe niwa kupuuzwa tu kama ulivyo upuuzi wako.

Wewe unakuja kutoa michango yako kwa Interahamwe halafu unaanza kulalamika!. Huoni kuwa wewe ndiyo una matatizo kifikra.

Narudia kukwambia.
Mimi sio ndugu yako,nduguzo ni Ubilisi wenzio.
Mia
 
Ndugu yangu, wanachofanya Chadema ni sawa na kuziba shimo la panya kwa mkate wa nyama.
Ndugu yangu.
Hoja yako ni fikirishi na inahitaji watu wenye fikra pana kuielewa vizuri.

Hoja yako ina maana kuwa, wanachofanya CHADEMA ni sawa na mtu anayekata majani ya mti akidhani hayatamea tena au anayekata majani ya mti akidhani mti utaanguka.

Swali la kujiiuza, kuna sialaha gani mpya itakayomfanya Prof. Safari kupambana na kushinda wakati akiwa Mjumbe wa Kamati Kuu hakuweza.
 
Kama unafahamu kuwa Prof. Safari anaenda kupambana na propaganda za CCM, ingekuwa vizuri pia ukatueleza nyenzo/silaha atakazotumia kupambana nazo.

Halafu wanatakiwa watwambie kuwa wanajuaje kama atashinda uchaguzi?
 
Alichosema pro safari ktk hoja yake ni kuwa,baadhi ya wanajamii wanakichukulia cdm kuwa ni chama cha udini(ukristo) na ukabila(chaga).yeye kasema anataka kiti hicho ili aieleze jamii kuwa chadema haikiko hivyo jinsi baadhi ya watu ktk jamii na hasa ccm kuwa chadema ni chama cha kitafa.sema tu waanzlishi wake wengi walikuwa ni kutika kilimanjaro.Ikumbukwe pia,dhana ya udina na ukabila zilipandikizwa na ccm ili kufifisha nguvu ya upinzani ambay n hatari kwa ustawi wa ccm.ikumbuwe pia cuf walipandikizwa dhana ya udini mwanzono mwa 2000.Tuwe tunasikilizwa hoja ya mtu anayoitoa na kuielewa vizuri na si kukurupuka mitaandaoni na kupost upumbavu.

Nenda usikilize hiyo video usimlishe maneno Prof!
 
Ukitaka kujua kama Chadema Waislam hawatakiwi muulize Said Arfi na Zitto Kabwe leo hii wapo wapi.
haa haa, je na yule mansur yusuphu himidi akiyetimuliwa ndani ya ccm ni mkristo? Acheni propaganda zenu!
 
Ndugu,
Mimi sikutaka kudodosa vipaumbele vya kitaifa kwa sababu kila Mtanzania mwenye akili timamu anavifahamu.

Nilipenda kufahamu kilichoko ndani ya CHADEMA kutokana na mantiki ya hoja zake nikiwa kama mmoja wa wanaoiangalia CHADEMA wakiwa nje.

Sawa boss, lakini hata yanayoendelea ndani ya Chadema kila Mtanzania makini anayajua, shida hapa umemsigle out mtu mmoja kuelezea aliyoyataja kama mtaji wake. Hata CCM wanatumia mikakati kama hiyo kushinda. Tuliambiwa maisha bora kwa kila mtanzania, kwani wakati huo watanzania wote walikuwa masikii? Na sasa je watanzania wote wana maisha bora leo? Wanasiasa wote wanatumia slogans.Ungemuuliza angekuambia yeye atafanikishaje, mambo hayo ni ya vyama vyote sio CDM tu hata wewe wajua
 
Back
Top Bottom