Diamond awatukana vijana wa Tanzania; 'wana njaa'!

Diamond awatukana vijana wa Tanzania; 'wana njaa'!

Kweli njaa inakutesa mpaka unaona kama unatukanwa.
Unakoelekea wewe hata ukiona mende wawili wamesimama utahisi wanakusema.
Wewe unaona sawa tu kutukanwa matusi ya rejareja kisa njaa? Njaa kali imekufanya ushindwe kugundua matusi unayotukanwa na watu qenye pesa. Unakuwa kama chawa kwa kuwa chawa hata atukanajwe yeye haoni soni wala soo.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, msanii wa muziki na mmiliki wa biashara, ikiwemo WASAFIBET, ameamua kuwatukana vijana wa kitanzania kwa makusudi kwa kuchapisha tangazo lenye nia ovu ya kudhalilisha, kutweza na kubagaza utu wa vijana wa Tanzania. Ni dhahiri shahiri kuwa amewalenga vijana kwa kuwa wengi wao hawana ajira, hivyo wanategemea kubet ili wapate fedha za kujikimu.
View attachment 3206254
MAONI YANGU
Diamond amefanya kitendo kinachopaswa kulaaniwa na kila mtanzania mwenye utu, mpenda amani na anayezingatia na kujali maisha ya wengine, bila kujali hali zao za kiuchumi. Haikuwa na haja kuchapisha tangazo hili la kidhalilishaji, kibaguzi, kichochezi na kibagazaji. Kuna namna nyingi za kutangaza lakini sio kwa udhalilishaji wa kiasi hiki. Naomba serikali iingilie kati kwa kumuonya huyu kijana aache dharau kwa vijana wenzake na pia aondoe hilo tangazo, kuwaomba radhi vijana wenzake na kuapa kutorudia kosa kama hili wakati mwingine.

Nawasilisha.
You only see what your eyes want to see
 
Wewe unaona sawa tu kutukanwa matusi ya rejareja kisa njaa? Njaa kali imekufanya ushindwe kugundua matusi unayotukanwa na watu qenye pesa. Unakuwa kama chawa kwa kuwa chawa hata atukanajwe yeye haoni soni wala soo.
sijaona neno kwamba vijana wa kitanzania mna njaa sana ila nimeona neno njaanuary neno ambalo hutumika kila siku kuonesha ugumu wa january. Hapo matusi yanatoka wapi.
 
sijaona neno kwamba vijana wa kitanzania mna njaa sana ila nimeona neno njaanuary neno ambalo hutumika kila siku kuonesha ugumu wa january. Hapo matusi yanatoka wapi.
Kwa kuwa una njaa hayo matusi huwezi kuyaona. Subiri ushibe kwanza mkuu.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, msanii wa muziki na mmiliki wa biashara, ikiwemo WASAFIBET, ameamua kuwatukana vijana wa kitanzania kwa makusudi kwa kuchapisha tangazo lenye nia ovu ya kudhalilisha, kutweza na kubagaza utu wa vijana wa Tanzania. Ni dhahiri shahiri kuwa amewalenga vijana kwa kuwa wengi wao hawana ajira, hivyo wanategemea kubet ili wapate fedha za kujikimu.
View attachment 3206254
MAONI YANGU
Diamond amefanya kitendo kinachopaswa kulaaniwa na kila mtanzania mwenye utu, mpenda amani na anayezingatia na kujali maisha ya wengine, bila kujali hali zao za kiuchumi. Haikuwa na haja kuchapisha tangazo hili la kidhalilishaji, kibaguzi, kichochezi na kibagazaji. Kuna namna nyingi za kutangaza lakini sio kwa udhalilishaji wa kiasi hiki. Naomba serikali iingilie kati kwa kumuonya huyu kijana aache dharau kwa vijana wenzake na pia aondoe hilo tangazo, kuwaomba radhi vijana wenzake na kuapa kutorudia kosa kama hili wakati mwingine.

Nawasilisha.
Ni either tafuta ajira au tafuta hela kaka
 
sawa mkuundugu yangu ila jitahidi sana uwe unahuzuria hospital maana unakoelekea sio
Kwa haya maandishi, tayari nimegundua nabishana na mtu anayeongeleshwa. Natwanga maji kwenye kinu.
 
Back
Top Bottom