Diamond platinumz atupiwa jini, lampata mama'ke!

Diamond platinumz atupiwa jini, lampata mama'ke!

Kuweni makini mnapojadili MAJINI maana kuna dini zingine wana ubia nayo, mpaka yana Surah maalum kwenye vitabu vyao
 
Nadhani kosa kubwa sana la Diamond ni kushine, hapa sizungumzii mambo ya majini au uchawi, nazungumzia ni jinsi gani huyu bwana mdogo anavyoshambuliwa na kukatishwa tamaa kwenye jitihada zake za kimuziki. Kitu nilichogundua ni kwamba watu wanachuki binafsi sana na huyu dogo na kuendelea kumsema vibaya.

Kuna siku moja nilikuwa nasikiliza Kiss FM ya Mwanza kulikuwa na watangazaji watatu mmoja binti na wengine wawili wanaume sasa the way walivyokuwa wanamsema huyu dogo kwa kejeli mpaka ilinifanya nipatwe na wasiwasi juu ya professional zao za utangazaji, mala Oooh Diamond hajui kiingereza, mara Oooh Diamond anajifanya anakataa kufanya kazi na msanii mmoja toka Kenya wa nyimbo za Injili kisingizio dini wakati kuna machafu kibao Diamond anayafanya ukianzia mavazi hadi anachoimba, sawa sikatai, lakini tuelewe Diamond ni binadamu na ana uwezo wa kufanya kile ambacho anaona ni sahihi kwake, sio lazima afanye kile ambacho wanakitaka watu wengine wakati yeye Diamond hayuko tayari.

Juzi kati pia nilisikia Clouds FM wakimsema vibaya huyu dogo kwa sababu tu ya kutokwenda kwenye msiba wa baba yake Dully. Jamani hivi tunashindwa kujua kwamba huyu Diamond na yeye pia anaweza kuwa na matatizo yake kama hayo ya kuuguliwa na mzazi wake, na vile vile nilimsikia mwenyewe Diamond akisema alishampa rafiki yake Dully pole mapema tu na kumueleza situation ya yeye kutoweza kwenda kwenye mazishi. Kitu ambacho mimi nakiona ni hawa watangazaji njaa wa hizi redio za kibongo kutaka kusafiria nyota ya huyu dogo, huyu Diamond yuko matawi sana kwa Africa hapa sizungumzii Tanzania au Kenya, nazungumzia Africa, kisha huyu Dogo amekuwa stable na makini sana kwa kazi zake na ndio maana amebaki kwenye game kwa muda mrefu.

Watangazaji njaa muwe mnachagua maneno ya kuzungumza kwenye hivyo viredio vyenu, manake hata kama Diamond akidrop kama mnavyotaka nyinyi sijui hata mtanufaika na nini. Keep up Diamond, keep up wasanii wote wa Bongo endeleeni kufanya kazi kwa nguvu ili muitangaze nchi ipasavyo. Tupo pamoja sana wadau wa muziki wa bongo na sanaa kwa ujumla. Wale wenye roho mbaya na nia chafu kwenu wasanii wala wasiwavunje nguvu nyinyi endeleeni tu kupambana.
 
waswahili bana tuna matatizo, eti jini!
haya mambo yaliwahi kunikuta, mke wangu alisafiri aliporudi akakaa wiki moja kisha akaumwa sana, sanaaa, mpaka akawa kama anaugua kichaa, akiwekewa dripu anachomoa, akikaa analia anaongea maneno ya ajabu na kujikuna kichwani. alikaa hospital karibia wiki mbili akawa kama amepona kabsaa, akarudi nyumbani akaniomba akapumzike kwao, kufika kwao tu kesho yake akaamka kichwa kinamuuma vibaya mno, mama yake akawa amepungukiwa imani akamchukua alfajiri wakaenda kwa "mtaalam", kule manyanga yakaonesha amerushiwa jini, tena hilo jini liloinilenga mimi likanikosa likaingia kwake!!!

Wakapewa mitishamba na kurudi nyumbani, alipofika nyumbani akachukua msaki akaenda nje akachuchumaa anapiga mswaki, mara hapohapo akaanguka chini, nikapigiwa simu nikamkuta yuko vibaya sana, nikambeba moja kwa moja mpaka hospital, akalazwa tena, wiki nzima haongei, ndugu na majirani wakienda kumtazama kila mmoja anarudi na maneno yake mtaani. akalamba dripu za kutosha, jamaa yangu mmoja ni doctor pale akamsimamia kwa ukaribu sana, baada ya wiki moja mtu akapona, mpaka leo hii yuko vizuri hakuna cha jini wala shetani!
 
Msongo tu wa mawazo,mama Diamond,nenda kawaone madaktari and you will be fine....
 
...alipenda limpate mamake?...GPL at their best....

Mkuu Tyta kwa shida hii tuliyonayo tutawamaliza maalbino wote..! Watanzania tunarudishwa nyuma na imani za kishirikina tulizonazo..
Mbaya zaidi hata wale ambao tunawaamini wamesoma na kufikia kwenye viwango vya kuitwa wasomi waliobobea nao wanakuwa na imani hizi za ushirikina.. Hawa ndo wanaodanganywa walete viungo vya albino ili wafanikiwe kwa kile kilichowapeleka kwa waganga..

Wakoloni walipitisha sheria ya uchawi sio kwa sababu waliamini kwamba upo.. Bali waligundua mipango yao mingi ilikuwa inakwamishwa pale kunapokuwa na tuhuma za uchawi.. Mtanzania wa sasa mtishie bunduki atakupeleka police.. Mtishie kumloga atakuogopa kama ukoma.. Na anaweza hata kuhama hapo mtaani..

Tumekuwa taifa la ulozi.. Very very sad..
 
Last edited by a moderator:
Kuweni makini mnapojadili MAJINI maana kuna dini zingine wana ubia nayo, mpaka yana Surah maalum kwenye vitabu vyao

hahahahaa watakuja sasa hivi, wakina jini maimuna na fatuma
 
Akili ndogo inapoongoza akili kubwa matokeo yake ndio hayo ya kuwaza ushirikina tu
 
Back
Top Bottom