Diamond Platnumz akiri kuwa anapenda sana nyoka

Diamond Platnumz akiri kuwa anapenda sana nyoka

Hujakutana na koboko bro ,
Ww ulishakutana nae au unaongea tu. Mimi nimeandika kutokana na nimeshayaona hayo sisemi stori tu na japo wametolewa sumu ila badi wanakua na tabia za kugonga ukimshika hana meno ila atafanya kama vile anakuuma wewe umejazwa stori za mitaani mara anaota nywele kama kiduku mara anakimbia akiwa kasimama hizo ni stori zawatu ila uhalisia bado koboko sio nyoka hatari zaidi japo anasumu kali sana
 


Bosi wa WCB Naseeb Abdul Juma almaarufu Diamond Platnumz amejipatia mnyama aina ya nyoka wa kuweka nyumbani.
Katika tangazo lake kwenye Instagram, mwanamuziki huyo alibainisha kuwa siku zote kumiliki nyoka kipenzi imekuwa ndoto yake.
Staa huyo wa Bongo mwenye umri wa miaka 32 alimtambulisha nyoka huyo wake kama rafiki yake mpya.

"Siku zote nimekuwa na shauku ya kuwa na nyoka wangu kama kipenzi ❤️🐍.. jameni tukutaneni na rafiki yangu mpya," alitangaza siku ya Ijumaa.

Aliambatanisha ujumbe huo na video yake akicheza na mnyama huyo anayeteleza huku kundi kubwa la watu wakiwa wamemzunguka.
Katika video hiyo, Diamond alisikika akikiri upendo wake mkubwa kwa nyoka na kueleza furaha yake kwa kumpata wa kufuga nyumbani

"Huyu mimi namfuga mnyama huyu nyumbani. Mimi napenda nyoka sana," alisika akisema.
Umati ulitazama kwa udadisi alipokuwa akichezea na nyoka huyo kwa usaidizi wa mwanamke aliyekuwa akimuonyesha jinsi ya kumshika. Hakuonesha uoga wowote na badala yake alionekana kufurahi sana kumshika.

Mwimbaji huyo anayetambuliwa kote duniani alifichua kwamba nyoka huyo wake atatambuliwa kwa jina Chichi.
Katika hali ya kawaida nyoka sio wanyama wa kupendwa miongoni mwa watu wengi. Wengi wa wanyama hao wana sumu ambayo inaweza kusababisha kifo au ugonjwa mbaya mara tu wanapomng'ata mtu.

Baadhi ya jamii za Kiafrika huhusisha mnyama huyo na uchawi na hivyo kamwe hawawataki karibu nao. Wale wanaofuga wanyama hao mara nyingi huchukuliwa kuwa wanashiriki katika uchawi.
Nyoka jau sana aise
 
Juzi almanusura tugongwe na black mamba[emoji3064][emoji3064]maskini sasa hivi chakorii angekuwa marehemu🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹🥹

Mungu yupo jamani
Ohoo pole Sana sister. Alikuwa nyoka gani?
 
Ww ulishakutana nae au unaongea tu. Mimi nimeandika kutokana na nimeshayaona hayo sisemi stori tu na japo wametolewa sumu ila badi wanakua na tabia za kugonga ukimshika hana meno ila atafanya kama vile anakuuma wewe umejazwa stori za mitaani mara anaota nywele kama kiduku mara anakimbia akiwa kasimama hizo ni stori zawatu ila uhalisia bado koboko sio nyoka hatari zaidi japo anasumu kali sana
Koboko nimekutana naye mara mbili katika mihangaiko yangu, ni near death experience na wala sitaki kukutana nazo tena

Mara ya kwanza ilikuwa ni serenje Zambia , nime drive usiku kucha ilipofika alfajiri nikatafuta parking rest bay nikalala sasa gari ni canter kwa hiyo kulala kwangu nimeweka miguu upande wa kushoto kichwa kipo kulia dirishani, nilikuja kushtushwa na mlio wa meno yake kwenye kioo kama nisingefunga kioo alikuwa ananiua, ,
Mara ya pili nimekutana naye hapo Tura njia kuelekea Tabora
 
Back
Top Bottom