Diamond Platnumz akiri kuwa anapenda sana nyoka

Diamond Platnumz akiri kuwa anapenda sana nyoka

Nyoka ni mdudu na


Bosi wa WCB Naseeb Abdul Juma almaarufu Diamond Platnumz amejipatia mnyama aina ya nyoka wa kuweka nyumbani.
Katika tangazo lake kwenye Instagram, mwanamuziki huyo alibainisha kuwa siku zote kumiliki nyoka kipenzi imekuwa ndoto yake.
Staa huyo wa Bongo mwenye umri wa miaka 32 alimtambulisha nyoka huyo wake kama rafiki yake mpya.

"Siku zote nimekuwa na shauku ya kuwa na nyoka wangu kama kipenzi ❤️🐍.. jameni tukutaneni na rafiki yangu mpya," alitangaza siku ya Ijumaa.

Aliambatanisha ujumbe huo na video yake akicheza na mnyama huyo anayeteleza huku kundi kubwa la watu wakiwa wamemzunguka.
Katika video hiyo, Diamond alisikika akikiri upendo wake mkubwa kwa nyoka na kueleza furaha yake kwa kumpata wa kufuga nyumbani

"Huyu mimi namfuga mnyama huyu nyumbani. Mimi napenda nyoka sana," alisika akisema.
Umati ulitazama kwa udadisi alipokuwa akichezea na nyoka huyo kwa usaidizi wa mwanamke aliyekuwa akimuonyesha jinsi ya kumshika. Hakuonesha uoga wowote na badala yake alionekana kufurahi sana kumshika.

Mwimbaji huyo anayetambuliwa kote duniani alifichua kwamba nyoka huyo wake atatambuliwa kwa jina Chichi.
Katika hali ya kawaida nyoka sio wanyama wa kupendwa miongoni mwa watu wengi. Wengi wa wanyama hao wana sumu ambayo inaweza kusababisha kifo au ugonjwa mbaya mara tu wanapomng'ata mtu.

Baadhi ya jamii za Kiafrika huhusisha mnyama huyo na uchawi na hivyo kamwe hawawataki karibu nao. Wale wanaofuga wanyama hao mara nyingi huchukuliwa kuwa wanashiriki katika uchawi.
Siyo mnyama
 
Sio kweli,kuna watu wanapenda nyoka kama ilivyo kwa watu kupenda mbwa paka nk.
Nina bro wangu tangu tupo shule ya msingi alikuwa akiona nyoka anamvizia anamkamata kwa mikono karibu na kichwa anamng'oa meno anamuweka mfukoni(wa kaptura) anakuja kututishia nyumbani na shuleni,baadae anamuachia

Kwakua maranyingi tulikuwa nae akifanya hivyo nikajikuta namimi woga ukatoka nikaanza kukamata, japo Mimi nilikuwa siweki mfukoni wala kumtoa meno,namkaba karibu na kichwa nikishamchezea namrusha mbali

Yeye hata vinyonga alikuwa anakamata anamuweka begani anaingia nae darasani wanafunzi wenzake wanatoka mbio.

Kuna wale buibui wakubwa sana wanakuwa na tumbo kubwa,wanatembea taratibu, anachumkua anamnatisha mgongoni kwenye shati halafu anajifanya kamsahau anakuja nae nyumbani au anaenda nae shuleni.

Kwahio naamini wapo wanaopenda nyoka.
Watu wa hivyo wapo. Ni one in a million.
Kaka yako ana hii tabia kitaalam inaitwa Ophidiophilia - tabia ya kupenda na kutoogopa nyoka. Alifaa sana asome awe research scientist wa viumbe hai. Wenzetu wanawaendeleza watu wa namna hii kusaidia kazi za utafiti.
Ni mnoma!
 
Sio kweli,kuna watu wanapenda nyoka kama ilivyo kwa watu kupenda mbwa paka nk.
Nina bro wangu tangu tupo shule ya msingi alikuwa akiona nyoka anamvizia anamkamata kwa mikono karibu na kichwa anamng'oa meno anamuweka mfukoni(wa kaptura) anakuja kututishia nyumbani na shuleni,baadae anamuachia

Kwakua maranyingi tulikuwa nae akifanya hivyo nikajikuta namimi woga ukatoka nikaanza kukamata, japo Mimi nilikuwa siweki mfukoni wala kumtoa meno,namkaba karibu na kichwa nikishamchezea namrusha mbali

Yeye hata vinyonga alikuwa anakamata anamuweka begani anaingia nae darasani wanafunzi wenzake wanatoka mbio.

Kuna wale buibui wakubwa sana wanakuwa na tumbo kubwa,wanatembea taratibu, anachumkua anamnatisha mgongoni kwenye shati halafu anajifanya kamsahau anakuja nae nyumbani au anaenda nae shuleni.

Kwahio naamini wapo wanaopenda nyoka.
Macho ya miilini ni tofauti na macho ya rohoni, si kila Mtu ni Binadamu na si kila Binadamu ni Mtu, nadhani umenielewa.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Watu wa hivyo wapo. Ni one in a million.
Kaka yako ana hii tabia kitaalam inaitwa Ophidiophilia - tabia ya kupenda na kutoogopa nyoka. Alifaa sana asome awe research scientist wa viumbe hai. Wenzetu wanawaendeleza watu wa namna hii kusaidia kazi za utafiti.
Ni mnoma!
Ni kweli,Baadae yeye alipenda kusomea mambo ya utalii(tour guide) so ni kama alienda kulekule maana aliwajua wanyama in and out,akiona hata mjusi atakwambi anaitwa hivi na hivi anakula nini,scientific name nk.
 
Nyoka ni mdudu na

Siyo mnyama
Wadudu na nyoka hawa wote ni wanyama wadudu ni moja ya kundi katika wanyama, wadudu ni kama nyuki na panzi na nyoka yupo kundi la reptilia pamoja na mamba, kinyonga, kobe n.k
Kuna kundi linaitwa mamalia ambalo linajumuisha binadamu, ng'ombe, simba, kondoo, mbuzi n.k ambapo watu wengi wanajua hao ndio wanyama pekee.
 
Nyoka ni viumbe wasio zuru mtu bila sababu...ndio maana anweza kukaa kwako akiwa mdogo hadi akawa lijoka kabisa na asikudhuru. Ila mwanada akimuona yeye atataka amuue huyo nyoka! Tu waajabu ndio maana kwenye Ecosystem tunatajwa kwamba tu viumbe namba mona waharibifu wa mazingira na Ecosystem....Btw watu watamwambia ni mshirikina.
Mungu alituamuru tumponde kichwa na atuume kisigino,sinaga urafiki na nyoka
 
Kweli ukipata hela bana unaweza kujua hata una mapenzi na wanyama.

Hivi mwaka 2006 huyu dogo ungemwambia habari za nyoka angekuelewa kweli?
2006 mbali sana mkuu mrudishe hadi 2000 tu hapo panatosha, 23 yrs ago angeulizwa unapenda kulala kitandan kimoja na brother🐍 angejibu?
 
Kha anaiga sana huyu jomba kamuona tu dimpoz kamshika nyoka kwa woga basi naye akajifanya anajua kila kitu
 
Back
Top Bottom