Diamond usiwapuuze wanaokuandama sasa, hao sio shilawadu au Konde Gang. Chukua hoja zao

Diamond usiwapuuze wanaokuandama sasa, hao sio shilawadu au Konde Gang. Chukua hoja zao

Hajasoma huyu alibahatisha kwenye mziki hivyo sio rahisi kusikiliza watu ngoja wamnyooshe kwanza atakuwa na Adabu siku nyingine.

Unajua ukizoea kubishana na kushindanishwa na watu wa local hapa nchini kama alivyozoea kushindanishwa na Alikiba huku akisaidiwa na TV yake na redio yake ya wasafi anashinda basi yeye anazani hivyo hivyo kwemye mitandao.
Diamond hajui Power of Society katika ulimwengu wa Music. Ninamuonea huruma maana ninajua dunia ilivyo hivyo anapoteza maana sana kwenye mtandao. Alafu Entertainment kubwa kama BET aisee wakikuweka Black list anayo kazi ya kurudi juu ulimwenguni.
Yani unamuinea huruma Mondi aliekuzidi kila kila kitu?

Kwa nini usiuonee huruma ukoo wako unaotafunwa na umasikini?
 
DIAMOND USIWAPUUZE KINA KIGOGO NA WANAMTANDAO, HAO SIO KINA KONDE NA SHILAWADU


Na, Robert Heriel


Diamond hapaswi kupuuza hii movement ya Wanaharakati wa kimtandao na wanasiasa, asije akafikiri kundi hili nila Wale Wasanii wenzake ambao hata shule hawajaenda.


Diamond anapaswa Ajue kuwa Wanaharakati wa mtandaoni ni wasomi tena sio wakubahatisha, wana-exposure ya hali ya juu kumshinda hata yeye mwenyewe,


Kama ningeambuwa nimshauri Diamond kuhusiana na kile kinachoendelea mtandaoni ningemwambia aombe radhi hata ya kinafiki kwani yote anayotuhumiwa ni kweli.

Diamond anapaswa Ajue kuwa kundi hili ndilo lile lile lililokuwa linamshambulia Mwendazake bila kukoma mpaka dakika ya mwisho kabisa bila kujali athari zozote. Ikiwa kundi hili lilimudu kumkabili Mkuu. WA nchi lazima Diamond afikiri mara mbili mbili asifikiri Kama mtoto mdogo.

Simtishi Ila namtahadharisha ili achukue hatua zinazostahili. Nafikiri Diamond Kama atazichukua hoja za hawa wanamtandao akazifanyia kazi atakuwa msanii Bora zaidi kuliko akizipuuza.

Ni kweli kabisa Diamond hakuweza kuzungumzia uonevu na ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanyika miaka ya 2016 - 2019 zaidi ya yote alitoa kibao kisemacho ACHA NIKAE KIMYA.


Diamond asije akadhani hawa wanamtandao ni Wale kina Konde na shilawadu


Diamond lazima aangalie hili kundi linaloongozwa na #Kigigo_kigogo, na wenzake halijawahi kushindwa katika movement wazifanyazo.


Hilo kundi asilipuuze na Kama atalipuuza basi Ajue anafanya makosa makubwa yatakayo mgharimu pakubwa mno.


Diamond asilione kundi hilo Kama watafuta Kick Kama yeye na wenzake kwani kundi hilo halitegemei kick.


Management ya Diamond na washabiki wake ambao kimsingi nafahamu wengi wao wanafikiri kuwa kila anayemkosoa Diamond ni haters wabadilishe huo mtazamo.


Hakuna anayemchukia Diamond labda Wasanii wenzake huko.


Diamond unachopaswa kufanyia KAZI ni madai ya hao Wanaharakati wa mitandaoni.


Wanamtandao hawakatai Diamond kuwa CCM hiyo ni Haki yake Kama apendavyo, lakini tatizo ni diamond kushindwa kutetea maslahi na haki ya jamii yake pale zinaposiginwa.


Diamond Kama anaakili aichukue hii Kama changamoto na ajifunze ili wakati mwingine aweze kutetea maslahi na haki za jamii yake wakiwemo Wasanii.


Lakini Kama atashupaza shingo yake Nina uhakika Diamond huu unaweza kuwa mwanzo wa mwisho wake.


Diamond akileta mawazo ya mwendazake akidhani kila anayemshauri na kumkosoa ni hater basi anguko lake halipo mbali.


Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Hawa wanaharakati unaowaita ni wasomi na wana exposure ya hali ya juu sana wananifikirisha sana.Exposure yao na usomi wao unawafanya wanashindwa kutambua sio kila mtu lazima awe mwanaharakati kama wao,watu wengine wameamua kuwa wafanyabiashara na mfanyabiashara yeyote anaside na upande utakaomletea faida hyo ndo principle dunia nzima.Hata hao wazungu mnaowaona ni watu wanaosimamia haki pale linapokuja swala la biashara watasimama na ilipo faida.Ndo maana mpaka leo wanaendelea kuinvest Uganda na Rwanda.Diamond ni mwanamziki na mfanyabiashara cku Chadema wakiwa madarakani ataside nao na ccm ikirudi tena atakuwa nao vilevile.Na labda wanashindwa kuelewa au wanajitoa ufaham serikali zetu za Africa ni ngum sana kukuacha ukaishi kwa amani ukianza kuwakosoa refer akina Lissu,Mbowe,Sugu na wengine ndo maana hao akina Kigogo wamejificha kuhofia usalama wao ila wanataka wenzao waende front wakale shaba,au wamesahau kilichomkuta Marehem Remmy Ongala na wimbo wake wa Mrema?
 
Kijana hana washauri wazuri !! mambo ya Usanii na Siasa ni kuwa makini nayo saana, watanzania wanamuhukumu kupitia mitandao.

Ningekuwa mimi, nabadilisha benchi lote la ufundi, naomba radhi naanza ukurasa mpya !!
Ila Roma ndio ana washauri wazuri? Sugu je?

Pr. J?
 
Ila Roma ndio ana washauri wazuri? Sugu je?

Pr. J?
Kuna tofauti kubwa kati na Msanii mpigania HAKI za binadamu na Msanii anayesifu dhuruma na uovu wa watawala!! nafikiri hapo ndipo mnapompoteza Nasibu. Sasa kwa sababu nyie ni wabishi haya mwambieni aendelee then atauona mwisho wake.

Mitandao ya kijamii ndiyo silaha tosha iliyobakia ya watanzania.

1623053505806.png
 
Kuna tofauti kubwa kati na Msanii mpigania HAKI za binadamu na Msanii anayesifu dhuruma na uovu wa watawala!! nafikiri hapo ndipo mnapompoteza Nasibu. Sasa kwa sababu nyie ni wabishi haya mwambieni aendelee then atauona mwisho wake.

Mitandao ya kijamii ndiyo silaha tosha iliyobakia ya watanzania.

View attachment 1811098
Endeleeni kujidanganya ahahahhahah
 
Ule wimbo wa Diamond "acha nikae kimya" nadhani watu wengi hawakuuelewa au waliuelewa lakini wameamua kujifanya hawakuelewa. Acha nikae kimya ilikuwa ni mamna ya kuwasilisha hisia zake kuwa hata yeye hafurahishi na baadhi mambo mabaya yanayotendwa na watu wake wa karibu. Sioni kama ni sawa kusema eti alikuwa anafurahia au anawatetea waliomteka roma na kuufungia wimbo wa ney wa mitego
 
Yaani aombe radhi kisa hakuisapoti chadema ila aliisapoti sisiemu, upuuzi kabisa! Ungewashquri hao unaowaita wasomi wanaharakati wa-mind their own eff business...
kua mtulivu, soma kwa makini. hawamshutumu kwa kufanya kampeni ccm, analalamikiwa kwa KUKAA KIMYA pindi uonevu uliposhamiri katika jamii, mfano baada ya kutekwa ROMA yeye akatoa nyimbo inaitwa ACHA NIKAE KIMYA leo yamemkuta hahahahahaha
 
Nafikikiri hujaelewa kilichoandikwa,hakuna aliyesema kisa hakuisapoti chadema, hapa kinazungumzwa kipindi watu mbalimbali wanapata matatizo kama kutekwa kwa Roma, Nay, kufungiwa kwa wasanii kww kuonewa yeye kama msanii mkubwa alifanya jitihadw gani?
Kwani kutekwa kwa Roma si wasanii haohao waliandamana wakiwemo WCB mpaka kwa Mkuu wa mkoa na akaahidi atapatikana na akapatikana. Mbona hili halisemwi tena nakumbuka Babu tale ndio alikua mstari wa mbele kwelikweli toka utawala wa Nyerere mpaka Jpm watu wametekwa na wameuwawa kwanini iwe kwa hawamu ya tano tu na kwa diamond pekee?
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Kigogo aliwahi kufanikisha kitu gani tangu aanze harakati zake ili tumuone kweli ni akili kubwa?

Nyingi tu na wewe unazijua au kama umesahau muulize Kenge Lugola.
 
DIAMOND USIWAPUUZE KINA KIGOGO NA WANAMTANDAO, HAO SIO KINA KONDE NA SHILAWADU


Na, Robert Heriel


Diamond hapaswi kupuuza hii movement ya Wanaharakati wa kimtandao na wanasiasa, asije akafikiri kundi hili nila Wale Wasanii wenzake ambao hata shule hawajaenda.


Diamond anapaswa Ajue kuwa Wanaharakati wa mtandaoni ni wasomi tena sio wakubahatisha, wana-exposure ya hali ya juu kumshinda hata yeye mwenyewe,


Kama ningeambuwa nimshauri Diamond kuhusiana na kile kinachoendelea mtandaoni ningemwambia aombe radhi hata ya kinafiki kwani yote anayotuhumiwa ni kweli.

Diamond anapaswa Ajue kuwa kundi hili ndilo lile lile lililokuwa linamshambulia Mwendazake bila kukoma mpaka dakika ya mwisho kabisa bila kujali athari zozote. Ikiwa kundi hili lilimudu kumkabili Mkuu. WA nchi lazima Diamond afikiri mara mbili mbili asifikiri Kama mtoto mdogo.

Simtishi Ila namtahadharisha ili achukue hatua zinazostahili. Nafikiri Diamond Kama atazichukua hoja za hawa wanamtandao akazifanyia kazi atakuwa msanii Bora zaidi kuliko akizipuuza.

Ni kweli kabisa Diamond hakuweza kuzungumzia uonevu na ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanyika miaka ya 2016 - 2019 zaidi ya yote alitoa kibao kisemacho ACHA NIKAE KIMYA.


Diamond asije akadhani hawa wanamtandao ni Wale kina Konde na shilawadu


Diamond lazima aangalie hili kundi linaloongozwa na #Kigigo_kigogo, na wenzake halijawahi kushindwa katika movement wazifanyazo.


Hilo kundi asilipuuze na Kama atalipuuza basi Ajue anafanya makosa makubwa yatakayo mgharimu pakubwa mno.


Diamond asilione kundi hilo Kama watafuta Kick Kama yeye na wenzake kwani kundi hilo halitegemei kick.


Management ya Diamond na washabiki wake ambao kimsingi nafahamu wengi wao wanafikiri kuwa kila anayemkosoa Diamond ni haters wabadilishe huo mtazamo.


Hakuna anayemchukia Diamond labda Wasanii wenzake huko.


Diamond unachopaswa kufanyia KAZI ni madai ya hao Wanaharakati wa mitandaoni.


Wanamtandao hawakatai Diamond kuwa CCM hiyo ni Haki yake Kama apendavyo, lakini tatizo ni diamond kushindwa kutetea maslahi na haki ya jamii yake pale zinaposiginwa.


Diamond Kama anaakili aichukue hii Kama changamoto na ajifunze ili wakati mwingine aweze kutetea maslahi na haki za jamii yake wakiwemo Wasanii.


Lakini Kama atashupaza shingo yake Nina uhakika Diamond huu unaweza kuwa mwanzo wa mwisho wake.


Diamond akileta mawazo ya mwendazake akidhani kila anayemshauri na kumkosoa ni hater basi anguko lake halipo mbali.


Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Ni kweli tupu
 
Back
Top Bottom