Diaspora: Kumbe Freeman Mbowe kumsifia Rais Samia ni baada kufunguliwa Account zake za Fedha zilizokuwa zimefungwa

Kwani mwanzo mbowe alikuwa hajui kuwa HAKI NI GHARAMA?
Sasa kaamua kuunga JUHUDI?
aliyoyapigania mpaka mkaanza kumuita MWAMBA AMESHAYAPATA?
AU KABADILI GIA ANGANI
Yeye kaunga juhudi sawa,lianzishe wewe sasa mwenye misimamo thabiti.
 
Nchi itakua na maendeleo ya kweli vyama vya upinzani vikiwa si zaidi ya 3.
Vyama 20+ vya upinzani halafu mnategemea kushika dola ni ujuha.
Haya mkishinda bado kuibiwa ni rahisi sana.
 
Ungefungiwa wewe ungejisikiaje. Haki ya kufanya biashara na kumiliki akaunti je imezingatiwa? Unapeleka ujumbe gani kwa wawekezaji wa kimataifa kwamba mnapoka pesa zao na kufunga biashara mnavyotaka. Good governance ikoje hapo. Kaa kitako Bibie itafakari.
 
clip hii na ile jana nazipenda.
 
Hata kama ungekuwa wewe ungeachaje kumsifia Rais Samia?
Jaribu kuvaa viatu vya Mbowe uone mapito aliyopitia. Magufuli alimharibia biashara zote zinazompa kipato kuanzia Bilicanas hadi shamba la maua pale Machame. Kisha akakomba fedha kwenye akaunti zake zote.

Isitoshe alitaka kumuua ndipo TISS waliokuwa hawapendezwi na hila za Mwendazake wakamtonya akatorokea Dubai kupitia Kenya pale baada ya Uchaguzi Mkuu wa 2020.

Kwa mapenzi ya Mungu amekuja Rais Samia asiyependa dhulma amemrudishia fedha zake, JE MBOWE anaachaje kumsifia?

Kule Ukonga alikuwa peke yake na hakuna mwana CDM alikwenda kumsaidia kifungo. Muacheni apange maisha ya kizazi chake. Kama mnataka maadamano na mikutano anzisheni vyama vyenu. Mbona Msajili wa vyama yupo na ofisi iko wazi!!
 
Watu wanangalia mambo yao binafsi hakuna anayejali mwenzake.

Kwakua Sabaya alimdhibiti Mbowe pale hai.

Samia atakua anamshughulikia kwa ajili ya maombi ya Mbowe.
 
Sasa si pesa zake ama zenu. Humu kuna watu hata wajawahi kulala selo wanabwabwaja tu. Yule aliyelala CHATO hakuwa mtu yule. Unambomolea mtu nyumba yake bila sababu. Unataka kumfunga mtu bila sababu. Kisa tu ni mpinzania. Kuna watu hata kuzikwa ni natumizi mabaya ya ardhi walitakiwa watupwe kwenye bwawa lenye mamba.
 
Nchi hii imewahi pata viongozi Wazalendo wawili tu Mwalimu Nyerere na Hayati Dr JPM hawa wengine ni wachumia Tumbo ,hata tukiwapa Nchi watauza kila kitu .
kazikwe pembeni yake.
 
Kweli tupu umenena
 
Jiwe si alifunga zile ACC bila sababu,hata ungekuwa wewe ungeshukuru zinapofunguliwa
 
Jiwe si alifunga zile ACC bila sababu,hata ungekuwa wewe ungeshukuru zinapofunguliwa
Sasa account zimefunguliwa lakini tunahitaji demokrasia bado, hadi sasa Tz majukwa ya kisiasa yamefungwa, katiba mpya ndio imeekwa mfukoni, mbowe yuko bizz kurudisha Bilikanas
 
shida siyo hiyo ya kulipwa shida ni kwanini sasahivi amewageuka wanachadema wenziie mpaka kufikia kuwafokea wasifanye maandamano wasitukane viongozi na kuitambua rasmi serikali ya mama nakusema anaupiga mwingi wewe ni nani mpaka ubishe
 
Mtu mshamba anafunga account za watu. Kisa pesa zao tu.mama piga kazi kanyaga twende
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…