Diaspora tukutane hapa: Tupeane ushauri wa kuanza maisha mapya Tanzania

Diaspora tukutane hapa: Tupeane ushauri wa kuanza maisha mapya Tanzania

ndugu wana diaspora'inakuwa ngumu sana sisi tulioshi nje ya Tanzania kwa miaka mingi kurudi na kuanza new life'mnafanyaje mbona wengine tumeshindwa? Nina rafiki zangu watatu walirudi kwa wakati tofauti wamekufa baada ya kuishi Tanzania kwa muda mfupi'tupeane mbinu how to start'kwa mtazamo wangu naona kitu kinaitwa mid setup'ya kwamba ukiondoka Tanzania na kuishi nchi nyingine miaka mingi ile mind setup inabadilika na ukirudi inabidi ubadilishe tena mind setup iwe kama ya watanzania'
hatari ni pale unarudi older than 40 years unaeza kufa on the process'tupeane ushauri tafadhali
Tatizo hamuwekezi kwenu.
Mnakosa hata kibanda cha kufikia.
Njooni niwajengee nyumba za kufikia mkirudi
 
Labda picha zitasaidia. Chumba cha darasa la pili kina muonekano huu:

e56935ed5cf258fa8afab6ca6e78cea2.jpg


9d94c4ab1d97ecb600a4124cc46aef34.jpg
 
Na asikuongopee mtu teknoloji inafanya watoto wa wenzetu kuwa na akili. Yaani mtoto wa kimarekani wa miaka kumi haya makitu ya computer sijui kudownload app, kuskan, kunetwok na wenzie kwenye vitablet na gemu atakutoa ushamba wewe babake.
Utakuta mtoto wa miaka kumi anajua kununua tiketi za treni za kwenye mashine. Anaweza kusoma njia na ratiba za matreni.
Halafu TV. Huu ni ushauri kwa wabongo. Waacheni watoto waangalie vipindi vya televisheni za watoto vya kingereza hasa channel za kimarekani. Yaani mtoto anasoma email na text zako kabla wewe mzazi hujajua kama anajua kusoma.

Teknoloji zimefanya mpaka walimu wao wa shule wanasema watoto wa siku hizi ni balaa.
Na mambo mabaya wanayaiga.Maadili potofu.udhibiti yafaa uwepo
 
Na mambo mabaya wanayaiga.Maadili potofu.udhibiti yafaa uwepo

Maadili mabaya Tanzania hakuna? Malezi ndio yanayompa mtoto maadili. Uzuri wa watoto wanasikiliza sana wazazi. Yaani kupotea kwa mtoto asilimia 100 ni kosa la mzazi au kukosa walezi wazuri.
 
Tatizo lipo hapa..
Bado ni kijana mdogo thana yaani ndo nipo kwenye 0 zero hustling, sijui naanza vp kabisa
Mkuu ingia Google andika how to apply America business visas. Au how to apply Europe tourist visas. Hapo utapata maelezo kibao tu.
 
labda zamani,siku hizi ukiwa na biashara unataka kuinvest unatakiwa uwe na kiasi kikubwa tu kabla ya kufanya biashara yenyewe,
Ya hio kweli lakini kuna njia za kufanya account fake(njia za kienyeji) nyingi tu. Sema ni kubahatisha tu kuna jamaa ana hela(tajiri) lakini kishaomba visas ya USA mara 3 zote kakataliwa na mtu maarufu sana. Sitaki kumtaja jina lake hapa
 
Kama huko ni kuzuri msirudi huku chukueni na ndugu zenu wote
Na kama unaona kila anaerudi anakufa ,hatuna cha kukujibu!
 
Kwanza ikumbukwe tofauti na ubaharia kuhamia nje balozi zinabana sana kwenye viza. Zinajitahidi kuchukua wasomi na watu wenye rekodi nzuri.
Hivyo wengi wa diaspora wana elimu au wanajua umuhimu wa elimu.

Kuna aliyesema wanabaguliwa kimaendeleo kwa sababu ya rangi huo ni uongo. Utabaguliwa kwa umasikini wako. Kuna maeneo au kazi hutazipata kwa umasikini wako na kwa elimu yako.

Ukifika nje usitegemee degree yako ya UDSM itakupa umeneja. Tafuta taaluma ya nje. Hata kama ni ufundi wa umeme. Jamaa wanaangalia zaidi ujuzi kuliko elimu. Hata biashara zipo usipokuwa muoga unatoka na hutabaguliwa kwa sababub una ngozi nyeusi.

Cha muhimu ubadilike sio uko nje unataka uishi kama uko Bongo. Stori nyingi kijiweni kila wikiendi sherehe na vijishughuli na umbea. Hawa wa hivi mwisho wa siku wanakuwa nyumbani hawana kitu na nje hawana kitu.

Nje kujituma ikibidi kuongeza elimu ongeza elimu. Ikibidi kazi mbili fanya kazi mbili. Ikibidi uwe na mke mnasaidiana maisha oa. Na si lazima mke afanye kazi anaweza kulea watoto ukaokoa magarama ya mabebi sita. Kuna familia ziko hivyo. Ila na huyo mwanamke anayekaa ndani awe na plan B ikitokea mumewe haingizi tena kipato au akifariki. Hapo ndio watu wanakuwa na bima za maisha.
Asilimia 90 ya waafrika walioko Ulaya ukiwaambia wanunue bima ya maisha watagoma kwa sababu za kijinga. Wakati bima hizo zinatajirisha sana wazungu.
 
Tatizo wanalokosea ni ku loos touch na tz mm binafsi nimeishi mbele miaka ya kutosha ila nina mpango 2020 nirudi hme nilichofanya nimenunua mashamba
mifugo pia nimeanzisha kilimo nataka pia nifungue shebeen/bar/hotel moja ya wastan very classic nadhani nitakuwa vema kimtindo siwezi kufia nchi za wazungu hilo nimekataa nimeisha tengeneza connection ya kuuza nyama SA na Congo kuna uhitaji mkubwa wa nyama ya ng'ombe
 
.........All I can say maisha ni popote.

Rudini bongo kama mmeshafanya savings za "kueleweka na mmejipanga" vizuri (relative term so to speak).

Maisha popote au warudi bongo?

Excuse me Sir, but you are contradicting yourself. Kama maisha popote usiwaambie warudi Bongo!

Msemo maarufu sana wa diaspora huo, "maisha popote," msemo wa kukata tamaa na wa uongo, masikini ya Mungu.

Sasa kama huyu Copenhagen yuko humu bila aibu anasema anaishi kwa kulipiwa renti na kanisa! Nani Tanzania analipiwa renti na kanisa zaidi ya Mzee wa Upako na Mama Rwakatare?

Namfahamu ni mchangiaji maarufu kwenye thread za immigration, anasema yuko Scandinavian countries lakini siku moja alianzisha mada hapa tukakuta hajui kuandika maneno Denmark wala Finland, yani yuko Scandinavia na darasa la saba la Afrika, he is definatelly gonna be shut out of even touching the bottom rung of the economic ladder. Mtu kama huyo atakueleza nini kuhusu maisha ya Ulaya zaidi ya kukushauri ukawe omba-omba wa makanisani?

Halafu anakuja mtu hapa anasema diaspora wakirudi wanataka kuishi standard za juu, nimemuuliza standard gani hizo ambazo walizoea Ulaya, kunywa Heineken? Kakimbia.

mengi uko sahihi. kama huna shughuli ya kufanya ughaibuni.

of course I am right, I know what I am talking about. Si wapo humu, kama naongopa watasema.

Na hilo la "kama huna shughuli ya kufanya ughaibuni..." hapo pia unawapotosha.

Sio shughuli mradi shughuli. A more helpful question is "Ulaya unafanya shughuli gani?" Kama ni odd job, "kazi za ajabu ajabu," mustakabali na hiyo kazi ni nini, utalea wazee mpaka lini, uta stock Wallmart aisles mpaka lini, utakaa kwenye kibanda cha security nje kwenye sub zero degrees mpaka lini? Au kama hujioni ukitoka humo, okay, unapata nini out of it, umefanya miaka 5, 10, do you have anything to show for it? Au unapokea tu subsistence paycheck, umelala umeamka, maisha popote!

Vast majority of the diaspora exist on subsistence compensation, mdomo uende kinywani. Na si wao tu, nanukuu, "...approximately 62% of Americans have less than $1,000 in their savings accounts and 21% don't even have a savings account..." Nenda google andika "USA Savings..."

Hawa ndugu zetu msiwadanganye eti wakija bongo tatizo wanapenda kuishi standard za juu, standard za juu zipi?
 
Nitatoa mchango wangu kutokana na experience ya kuishi kama diaspora na kuishi nyumbani pia.

1. Ukiondoa upweke na kupoteza connection za nyumbani maisha nje ni marahisi zaidi kiuchumi. Kwa kazi zinazofanana basi mtu aliye nje ataishi vizuri zaidi. Wengi tu akosea kufananisha cashiers wa ulaya na meneja wa benki wa Tanzania. Tufananishe vitu vinavyofanana. Maisha ya watu wanaofanya kazi zinazofanana nje na tanzania ya nje yana afadhali sana.

2. Kwa wanaofanya manual labour ulaya wana nafasi zaidi za kukuza kipato upesi kwa muda mfupi kuliko wanaofanya manual labour Tanzania.

3. Kwa wasiopenda shortcut nje ni rahisi zaidi. Ni hivi karibuni tu tanzania tumeanza kuishi kwa kipato chetu. Kabla ya hapo maisha hayakuwa na uhalisia. Kula senti unayoipata ughaibuni serikali inaijua. Kuudanganya mfumo ni kazi ngumu sana.

4. Acces to basic human needs kama usafiri,hospitali,dawa,malazi, elimu n.k kwa kiwango cha juu ni rahisi kupata ukiwa ulaya kuliko tanzania. Kwa Tanzania ukiumwa magonjwa makubwa Tanzania ni changamoto. Ukiwa na mjamzito ni changamoto, ukiwa na mtoto msogo ni changamoto. Huduma za afadhali kidogo zipo kwa upper middle class tu. Hospitali kama Agakhan kwa ulaya bado sana. Ila huku kwetu ndio best of the best.

5. Ukiwa na watoto ulaya wanauhakika wa kusoma shule hadi vyuo vikuu bora zaidi duniani kwa gharama ndogo sana. Elimu kama hiyo mtu wa kipto cha chini tanzania kuipata ni nadra hadi kwa scholarship. Na wale wenye vipato vya juu sana inawabidi walipe pesa nyingi sana kusomesha watoto wao kwenye vyuo vya nje.

Kujumuisha. Diaspora ni sehemu nzuri kama umeamua ku-sacrifice maisha yako kwa watoto wako(second generation immigrants). Tanzania kunafaa kama unataka wewe ndio ufurahie maisha zaidi bila kujali sana future ya watoto hasa kama huna pesa nyingi.

Hakuna haha ya kugombana sote sisi ni ndugu, ni vema tukapendana. Leo waweza kuwa diaspora kesho ukawa tanzania na kinyume chake.
 
Maisha popote au warudi bongo?

Excuse me Sir, but you are contradicting yourself. Kama maisha popote usiwaambie warudi Bongo!

Msemo maarufu sana wa diaspora huo, "maisha popote," msemo wa kukata tamaa na wa uongo, masikini ya Mungu.

Sasa kama huyu Copenhagen yuko humu bila aibu anasema anaishi kwa kulipiwa renti na kanisa! Nani Tanzania analipiwa renti na kanisa zaidi ya Mzee wa Upako na Mama Rwakatare?

Namfahamu ni mchangiaji maarufu kwenye thread za immigration, anasema yuko Scandinavian countries lakini siku moja alianzisha mada hapa tukakuta hajui kuandika maneno Denmark wala Finland, yani yuko Scandinavia na darasa la saba la Afrika, he is definatelly gonna be shut out of even touching the bottom rung of the economic ladder. Mtu kama huyo atakueleza nini kuhusu maisha ya Ulaya zaidi ya kukushauri ukawe omba-omba wa makanisani?

Halafu anakuja mtu hapa anasema diaspora wakirudi wanataka kuishi standard za juu, nimemuuliza standard gani hizo ambazo walizoea Ulaya, kunywa Heineken? Kakimbia.



off course I am right, I know what I am talking about. Si wapo humu, kama naongopa watasema.

Na hilo la "kama huna shughuli ya kufanya ughaibuni..." hapo pia unawapotosha.

A more helpful question is "Ulaya na Marekani unafanya shughuli gani?" Sio shughuli mradi shughuli. Na kama ni odd job, "kazi za ajabu ajabu," mustakabali wako na hiyo kazi ni nini, utalea wazee mpaka lini, uta stock Wallmart aisles mpaka lini, utakaa kwenye kibanda cha security nje kwenye sub zero degrees mpaka lini? Au kama hujioni ukitoka humo, okay, unapata nini out of that job, umefanya miaka 5, 10, do you have anything to show for it? Au unapokea tu subsistence paycheck, umelala umeamka, maisha popote!

Vast majority of the diaspora wana exist on subsistence compensation, mdomo uende kinywani. Na hii sio wao tu "...approximately 62% of Americans have less than $1,000 in their savings accounts and 21% don't even have a savings account..." Nenda google andika "USA Savings..."

Hawa ndugu zetu msiwadanganye eti wakija bongo tatizo wanapenda kuishi standard za juu, standard za juu zipi?

Fikiria mtanzania ambae katoka Tanzania akiwa maskini. Ana paspoti ya Marekani popote atakapo duniani anaenda. Hasumbuliwi visa labda za Iraq na North Korea. Ni uamuzi tu kwenda Jamaica au Hawaii kwa wikiendi. Au aungane na marafiki wachukue livu ndani ya boti kubwa (cruise) wazurure visiwa vyote vya Caribbean wiki nzima au wiki mbili. Ni kula, kunywa, muziki, wanawake na kulala.

Mtanzania huyo ana miliki mjengo wa gorofa tatu. Anachagua alale chumba kipi. Hata kama ana mkopo wa nyumba lakini nyumba ina jina lake. Na ikipanda bei anaweza kuuza na kuchukua cha juu.

Mtanzania huyu ashindwe mwenyewe akitaka kusoma atasoma mpaka Phd kumi kwa mkopo wa serikali.

Familia yake ina uhakika wa kwenda shule, huduma za matibabu. Kula sio ishu. Mataifa yaliyoendelea hayajui bei za sembe na sukari kwa sababu vyakula ni vyingi na vya aina nyingi.

Umezungumzia savings. Wengi hawana savings kwa sababu hawana nidhamu ya kusevu. Wana ma credit card mpaka ya laki. Wengi wakiwa na shida ya pesa hawafikiri kumtapeli mtu wanachaji credit card.

Hizo kazi hovyo ulizozitaja ni za kuanzia kwa wanafunzi na ni kazi za pili za kuongeza kipato.

Sasa basi katika huu mjengo wa gorofa tatu. Mtanzania kaweka viflat screen mpaka jikoni. Akipika kaugali anamcheki mzee Majuto na Senga kwenye Youtube. Na anatumia internet ambayo haina cha bando la kuchacha. Ni high speed ya ukweli haina chenga wala nini.

Wakiitwa wenye magari huyu jamaa anakwenda na ushangingi mrefu kushinda Prado. What the hell? Kwanza hakuna Prado. Ni mwendo wa ma escalade, tahoe, yukon denali, lexus, benz, infinity, bmw nk. Ni magari yaliyojaa ma gps na bluetooth. Unaliambia gari piga cd, piga mwimbo wa tatu. piga youtube, piga simu mpigie nanihii. Wabunge wa Tanzania wanayo hiyo? Hata kina Manji hoi hapo. Wana viyoyozi tu.

Barabara ndio usiseme mpaka mlangoni. Unaweza kukaa mwaka hujaona mchanga. Ni lami, pavement, bustani na majani. Sio Bongo hata nyumbani kwa waziri nje kuna makorongo na mazalia ya mbu na vyura.

Mtanzania ana pension atalipwa mpaka siku anaingia kaburini. Na atalipwa hata akiwa Tanzania. Kuna Mkenya karitaya kila January anaenda Kenya mpaka mwezi wa nne anarudi Marekani. Anakimbia baridi. Wenzetu Kenya wana uraia wa nchi mbili basi mambo ni mswano zaidi.

Na hayo yote unayapata kwa mshahara halali wa kawaida tu au kwa kuunga kazi mbili au kushirikiana na mkeo. Huhitaji kuwa mbunge, hakimu, daktari wala loya.

Kwa mwendo huo unarudi nyumbani Mungu akupe nini. Mbu wa maleria kali?

Ni hivi maisha ni kupanga. Mungu katupa akili tuzitumie. Kama umeenda nje na malengo yako ya elimu au pesa. Ukikamilisha rudi nyumbani. Ila kama umeenda nje kuishi. Jichanganye na mfumo wao wa maisha. Sio urudi nyumbani eti maisha magumu. Yakikushinda nje hasa Marekani na Tanzania yatakushinda. Wewe ni mshindwaji. Kama unakumbuka yalikushinda Tanzania kabla hujakimbilia nje.

Hao diaspora wanaoshindwa maisha hasa Marekani ni wale wasiojua wameenda kufanya nini. Mtu anakaa nyumba ya kupanga miaka 30. Akiulizwa niko kwa muda hapa. Lakini anazeekea nje. Hawajui kujiunga na mfumo wa Marekani.

BWEGE YOYOTE KUTOKA TANZANIA AKIINGIA MAREKANI ANAWEZA KUISHI HAYO MAISHA NILIYOYAELEZA HAPO NDANI YA MIAKA MITANO TU!
 
Tatizo kubwa linalokatisha tamaa kurudi Bongo ni institutionalised ‘petty’ corruption, na huduma mbovu za kijamii kama vile maji, umeme, afya, elimu, mfumo wa usafiri na usafirishaji.

Mpaka pale CCM itakapotoka madarakani, na kuingia watu wasio masalia ya CCM, ndipo Tanzania inaweza kutatua hizo changamoto.

Until then, kurudi ni vigumu
 
Tatizo kubwa linalokatisha tamaa kurudi Bongo ni institutionalised ‘petty’ corruption, na huduma mbovu za kijamii kama vile maji, umeme, afya, elimu, mfumo wa usafiri na usafirishaji.

Mpaka pale CCM itakapotoka madarakani, na kuingia watu wasio masalia ya CCM, ndipo Tanzania inaweza kutatua hizo changamoto.

Until then, kurudi ni vigumu

Kurudi na kuishi na Tanzania ni sawa kujihukumu kifo chako mwenyewe huku ukiwa selo ukingoja utekelezaji wa hukumu yako.....

Tanzania hakuna tumaini la maisha unless umetokea kwenye familia zilizo kwenye system other wise kila kitu kwako ni kamari


Ni kama msituni ambapo kila mnyama anaangalia namna yake ya ku survive.....

Nchi haipo organized kwenye mambo mengi sana ya msingi........

Kuishi Tanzania ni gharama kubwa ambapo hiyo inaweza kuku gharimu hata maisha yako.....


Just imagine

Unajibana bana unajenga nyumba nzuri ya kuishi ambapo unatakiwa utafute kampuni ya ulinzi kwa ajili ya usalama wako.....unatakiwa uwe na generator kwa ajili ya kujihakikishia upatikani wa nishati ya umeme au solar power.....unatakiwa uchimbe kisima kwa ajili kujihakikishia upatikanaji wa maji hapo kwako......bila ya kusahau unatakiwa uwe na usafiri kwa ajili kurahisisha mambo yako....vile vile unatakiwa uepukane na shughuli za usiku zisizo na ulazima kwa ajili ya usalama wako......ukitoa hela kwenye ATM machine unatakiwa ujifiche kwa usalama wako......

Kumbuka kuwa unayafanya yote huku ukiwa unalipa au kukatwa kodi katika huduma au bidhaa unayo nunua.........


Tanzania kubadilika ni mpaka lije gharika na kuangamiza uzao wote wa wanasiasa wa sasa....na kuanza upya.......
 
Back
Top Bottom