Diaspora tukutane hapa: Tupeane ushauri wa kuanza maisha mapya Tanzania

Mbona wenzenu wanasema Tz ni kuzuri Ulaya/US/Japan waTz wanateseka!

Tanzania kuzuri wewe!

Tanzania watu hawaishi kwenye vi apartments!

Tanzania watu hawaishi paycheck to paycheck!

Tanzania watu wana disposable income ya kumwaga.

Tanzania watu hawana mortgage za miaka 30. Wanamilikia ‘majumba’ yao free and clear!

Tanzania watu wanavaa luxury brands kila sehemu. Yaani hata ukienda pale Mwenge madukani unakuta Moschino, Gucci, Burberry, Fendi, Chanel, n.k. zinauzwa kwa bei rahisi sana ambazo Watanzania wengi wanazimudu. Ulaya na Marekani hizo kuxury brands ma diaspora wengi wa Kitanzania hawawezi kuzimudu gharama zake. Lakini hapa bongo unakuta zinauzwa nje tena zinaning’inizwa au zimetandazwa kwenye mkeka.

Tanzania watu hawaishi na roommates maana wana majumba mengi mengi tu na hivyo hawana sababu ya kubanana banana.

Maji hayakatiki Tanzania. Umeme haukatiki. Mabarabara ni mazuri.

Yaani kwa ujumla viwango vya maisha Tanzania viko juu sana kuliko Ulaya na Marekani.



Cheki Mwenge hapo...hapo huko luxury brand yoyote ile. You name it, they got it.

Kama mchuchu wako anapenda red bottoms we nenda Mwenge tu...utapata.

 
Good analysis
 
Watu wasio na vipaumbele sawa, historia sawa, nafasi sawa, akili sawa wala maumbile sawa hawawezi kuwa na mawazo sawa.

Ukweli kwamba wote tumetokea Tanzania hautufanyi tuwe sawa.

Na hilo ni hambo la kusheherekea. Tungekuwa sawa wote kungekuwa hakuna haja ya juwa na JF.

Tuwe na JF kubadilishana mawazo gani wakati wote tunawaza sawa?
 
Ufeki hauji kutokana na sehemu unayoishi. Unakuja kutokana na kuishi maisha ya uongo.

Twaib!

Kwa mfano, kuvaa fake luxury brands ndo ufeki wenyewe huo.

Mtu unaenda kununua eti gauni la Gucci pale Kariakoo halafu unapiga nalo picha unarusha Instagram [mtandao wa Kimarekani, btw] halafu unatamba eti ume ‘slay’. Unatamba kwamba wewe ni ‘slay queen’.

Yaani unatamba na fake designer brand.

Does it get any faker than that?
 
Na haya ndiyo maendeleo.
 
Wakati mimi nina access ya kununua hizo luxury brands zenyewe za kweli, lakini nina falsafa ya kukataa kununua nguo yoyote yenye maandishi makubwa inayonifanya nionekane kama tangazo la biashara linalotembea.

Na nikinunua nguo ni kwa sababu nimeipenda, si kwa sababu ya jina.

Halafu mtu atakwambia mimi feki kwa sababu naishi Marekani.
 

That’s right! Ukitaka kumnunulia Bi. Zuhra mkoba wa Hermès unaenda moja kwa moja kwenye duka la Hermès.

Ila baadhi ya hawa wenzetu vitu kama hivyo huwa wanavinunulia sehemu kama hizi!



 

Nasikitika kuwa wachangiaji tumetoka nje ya mada au nje ya lengo la mtoa mada.......

Mtoa anataka wale walioamua kurudi washauriane jinsi ya ku survive kwenye mazingira mapya.....
 
Umenielewa 300%....hamna kitu kizuri kama kuwa na experience ya pande zote.
 
Nasikitika kuwa wachangiaji tumetoka nje ya mada au nje ya lengo la mtoa mada.......

Mtoa anataka wale walioamua kurudi washauriane jinsi ya ku survive kwenye mazingira mapya.....
Ukifuatilia sana kuna wachangiaji wa mwanzo ambao ni wakazi wa Tz walivamia uzi na kuanza kuponda Diaspora. Hao ndio wamefanya huu uzi ubadili muelekeo.
Na si uzi huu tu ukija uzi wowote kuhusu Diaspora lazima waje wakazi wa Bongo na kuanza kuponda Diaspora.
 
Nasikitika kuwa wachangiaji tumetoka nje ya mada au nje ya lengo la mtoa mada.......

Mtoa anataka wale walioamua kurudi washauriane jinsi ya ku survive kwenye mazingira mapya.....

Well, too bad.....

Hapo ni kwenye outdoor diner moja hivi inaitwa kwa Mchambawima...

Hapo unapata kuku freshi, chipsi freshi na tamu, yaani kwa ujumla kila kitu freshi kwa ajili ya afya bora.

 

Hao ni miongoni mwa waTanzania walioachna na matumizi sahihi ya fahamu zao.....wanaongozwa na chuki na mihemko kuliko uhalisia

Wao wanaamini kuwa ukiwa ughaibuni tayari wewe ni bilionea na ukipanga kurudi maana yake umefirisika Na umeshindwa maisha huko ughaibuni....

Hawa ni wa kuwasamehe mpaka siku watakaporejewa na fahamu zao
 

Ni usongo wa maisha tu mkuu. [emoji23][emoji23][emoji23]

Tena hawa ndio wanaosababisha watu wengi wa diaspora washindwe maisha nje.

Ukiamua kuishi nje, jijenge usibabaishwe na wabongo. Wakikuambia huna hata choo Tanzania. Wajibu nakunya Marekani sihitaji choo cha Tanzania. Wakikuambia ukija utakunya wapi. Unawajibu hoteli. Choo chake kisafi kinakaribia na changu cha Marekani.

Bila ya hivyo watakupoteza muelekeo.
 
Nasikitika kuwa wachangiaji tumetoka nje ya mada au nje ya lengo la mtoa mada.......

Mtoa anataka wale walioamua kurudi washauriane jinsi ya ku survive kwenye mazingira mapya.....
Kutoka kwenye mada si kitu kizuri.

Lakini kujifunga katika mada wakati ambapo mada inaweza kuhitaji mawazo mapya ya kutoa changamoto nako si kitu kizuri.

Mtu anaweza kuanza mada kwa kutaka ushauri wa kurudi bongo, halafu mada ikapanuka na kujumuisha mazungumzo kama kurudi bongo ni suala zuri.

Ukienda kwa kufuata maagizo ya awali tu katika vita inayotaka mtu kuamua mambo upya na bila kuzingatia maagizo ya awali, unaweza kufa kwa sababu unafuata maagizo wakati ungeweza kujiepusha na kifo kwa kuangalia hali halisi ilivyo bila kuzingatia maagizo ya awali.

Ni muhimu kutokutoka nje ya mada bila sababu ya msingi.

Ni muhimu kupanua mada kwa sababu ya msingi.
 
Huu mtaro upo kwenye moja ya thoroughfares za jiji la Dar!




Mitaa ya matajiri hii....

 

Thumb up

Nimekuelewa......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…