Dini ni kwa ajili ya "Low minded people", Genius can't be trapped!

Dini ni kwa ajili ya "Low minded people", Genius can't be trapped!

Umeandika kwamba mambo yakienda mrama watu watatafuta muujiza.

Kutafuta muujiza hakuna maana kuwa muujiza upo.

Kama vile wewe kutafuta dollar bilioni moja nyumbani kwako, kama haipo, hakuifanyi iwepo.

Umeelewa?
Anzia mwanzo usibadili ujumbe wa msingi, vipi mbona kama unasoma huku unasinzia wewe?
 
Uchawi ni uchawi = tautology. Logical fallacy.

Unapotoa definition ya neno uchawi, hutakiwi kulitumia tena hilo neno uchawi.

Huelewi kanuni za msingi kabisa za definition. Ndiyo maana ninapata matatizo sana kujibizana nawe.

Kwa sababu hilo neno uchawi ndilo unaloli define na hivyo ukilitumia katika ku define uchawi unatuingiza katika loop isiyo na mwisho.

Bado huja define uchawi ni nini.

Unalazimisha tu "uchawi ni uchawi"
Hahaaa😅😅😅 kwani nimeanzia hapo brother, mbona nimeelezea sana nilipokuwa najibu hoja zako katika post za awali. Tatizo lako unakimbia hoja ya msingi na kuangalia wapi utajitetea
 
Anzia mwanzo usibadili ujumbe wa msingi, vipi mbona kama unasoma huku unasinzia wewe?
Umekubali kwamba watu kutafuta au kutotafuta muujiza ni moot and irrelevant point kwa sababu kama muujiza haupo, hata watu wakiutafuta, huko kuutafuta kwao hakufanyi muujiza uwepo?
 
Hahaaa😅😅😅 kwani nimeanzia hapo brother, mbona nimeelezea sana nilipokuwa najibu hoja zako katika post za awali. Tatizo lako unakimbia hoja ya msingi na kuangalia wapi utajitetea
Mpaka sasa bado huja define uchawi ni nini.

Nimekuuliza uchawi ni nini?

Umenijibu uchawi ni uchawi.

Inaonekana wewe mwenyewe hujui uchawi ni nini.
 
Mpaka sasa bado huja define uchawi ni nini.

Nimekuuliza uchawi ni nini?

Umenijibu uchawi ni uchawi.

Inaonekana hujui uchawi ni nini.
Screenshot_20231109-231004.jpg
 
Nimekuuliza, tukio ambalo hatulielewi leo na halina majibu ya kisayansi, ukasema ni uchawi.

Kesho tukalielewa na tukapata majibu ya kisayansi ambayo hayahitaji dhana ya uchawi kulielezea hilo tukio, bado utaliita uchawi?

Ukiliita uchawi, huoni kwamba hapo utakuwa umevuruga definition yako ya uchawi?

Ukisema hili si uchawi, kwa maana tumepata maelezo ya kisayansi ya kulielezea vizuri, bila kuhitaji dhana ya uchawi, huoni kwamba hapo unaweza kuita mambo mengi uchawi leo kwa sababu hatujayajua kisayansi, wakati kiukweli mambo hayo si uchawi, hatujayajua vizuri kisayansi tu, na tukiweza kuyajua tutaona si uchawi?

Nimetoa mifano ya mababu zetu walivyoona mambo mengi ya wazungu uchawi, redio, magari, bunduki, kutabiri kupatwa kwa jua etc.

Lakini leo tumeyajua haya mambo kisayansi, tumejua si uchawi.

Huoni kwamba hiyo definition yako ya uchawi inakuweka katika position waliyokuwapo hao mababu zetu walioamini teknolojia ya wazungu ni uchawi, kwa sababu hawakuielewa tu?

Huoni kwamba na wewe umejipa tabia ya kuvipa vitu usivyovielewa jibu la rahisi la uchawi, wakati kuna uwezekano mkubwa si uchawi, ni mambo ambayo hujayaelewa vizuri tu?
 
Endeleeni... Kwa kigezo hakuna Mungu, watu wapumbavu huwaza kuwa hakuna Mungu(biblia )huu upuuzi wako biblia ilishauandika tiyari
Walioleta mambo ya kufirw ndio hao walioitengeneza biblia na huyo mungu wenu, saivi ndio hao wanaotetea haki za mashoga, kwa maana wanatumia hiyohiyo biblia kwamba, mpende jirani,usimbague binadamu, so kama jiran yako ni shoga inabidi umpende kwa maana ni amri,
 
Dini na sayansi kwnye uislam uko wazi kabisa watafute wataalam akiwemo sheikh mmoja huwa hampendi mwamposa[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] huwa namfitilia san mafundisho yake
 

Astronomers​

Physiologists​

Chemists and alchemists​

Economists and social scientists​

Geographers and earth scientists​

Mathematicians​

Philosophers​

Physicists and engineers​

Nimesema mkubwa, hao uliowataja hamna hata mmoja nnaemjua.
 
Bado naamini uchawi upo, Miujiza hipo na Mungu yupo bila ya shaka yeyote. Chukua muda wako nenda Kwa waganga, tembea vijijini huko utaona.

Shida watu wana-exagerate baadhi ya mambo mpaka wengine wanahisi kuwa hizi ni story za kutungwa but kabisa kabisa Kuna nguvu za Giza ambazo haziwezi kuelezewa kisayansi.

Ngoja tuangalie mifano hii ya kawaida ambayo huenda ikaonekana ya kipuuzi tu,

Wale watoto mashuleni wanaoanguka usidhani ni maigizo au matatizo ya kisaikolojia, ni nguvu za kichawi. Kwanini baadhi yao wawe na nguvu ya kuwashinda wanaume wengi? Kwanini hatujaona wale watoto wakitibiwa kisayansi? Yaani watoto wakianza kupandisha, suluhu huwa ni masheikh na mapadri. What is your comment on it?

Hivi ni kwanini baadhi ya maeneo huwa yanasifika sana Kwa uchawi, kwanini si maeneo mengine. Je ni 'tricks' tu wakazi wa maeneo hayo katika kuwazuru watu wengine? Jiulize tu kwanini cases za kujiua Kwa wahehe ni njingi? Unaweza ukasema ni genetic disposition, but je sayansi imeelezaje hutokeaji wa hiyo genetic disposition au ndio imeishia kusema tu ni 'genetic disposition'. Kwanini Salem, Massachusetts ni maarufu Kwa uchawi na si sehemu nyengine? Kwanini Misitu ya Romania inaogopwa sana Kwa matukio ya kichawi kuliko Misitu mingine? What makes this spatial variation?

Najaribu kufikiria baadhi ya mambo, nawaza ni coincidences au ni uchawi, miujiza au ni nguvu za giza. Wangapi huambiwa nitakuroga uwe chizi na hilo hutokea kweli?

Ngoja nikupe kisa hiki. Kuna kijana mmoja alisomasoma elimu ya uchawi wa kitabu (inahusishwa sana na masheikh). Basi huyu kijana akawa anatumia huu uchawi wake kuchukua wake za watu, na kuzini nao. Wengi walimuonya juu ya hilo ila kutokana na jeuri na kibri chake, huyu kijana hakuacha tabia hiyo. Baada ya muda huyu kijana alipatwa na uchizi then akafa.

Matukio kama haya ni mengi. Je uwingi wa matukio kama haya Huwa ni coincidences tu au Kuna kitu kingine.

Tunaishi katika Dunia ambayo inastaarabika, ni nadra sana kuona matukio ya uchawi hasa maeneo ya mjini kutokana na usasa. Lakini ukirudi vijijini Bado watu wanaishi Kwa kudumisha Mila zao na ni rahisi kuona miujiza. Sisi watu wa Quantum physics, sijui Geochemistry na fluid dynamics si rahisi kuexperience mambo hayo.

Wangapi ni madokta, maprofesa na wabobezi katika fani mbalimbali but still wanaamini katika hayo mambo ya miujiza na supernatural powers? Je, bado ni wajinga, elimu zao hazljawakomboa au ndio walisoma tu kujiingizia kipato?

Jamii Nyingi kote duniani kama Incas, Mayan, Aztecs, Mesopotamia, ancient Chinese, Nubian, Egyptians, Great Zimbabwe na nyengine nyingi zilikuwa Zina practice uchawi, je walikuwa wanawadangawa watu wao tu au uchawi ulikuwa una Practical uses.

Sheria za kupambana na uchawi ziliwekwa hasa nchi za Ulaya na bara la America na watu wengi waliuliwa baada ya kushukiwa kufanya uchawi, Historia inaeleza. Hivi jambo ambalo halina uhasilisia linaweza kusambaa kote duniani, tena likawa na athari zilezile?

Mkuu wewe binafsi(sio kuhadithiwa) umewahi kushuhudia muujiza wowote?
 
Mkuu wewe binafsi(sio kuhadithiwa) umewahi kushuhudia muujiza wowote?
Miujiza ipo,..na Mimi ni miongoni mwa watu waliowahi kushuhudia muujiza Kwa macho yangu mawili.

Au unataka useme kwamba miujiza ni story tu?,..

Kumbuka kwamba miujiza ni elimu ya sayansi ambayo hatuna elimu juu ya utendaji kazi wake bali huwa tunaona matokeo yake tu.,

Kwa mantiki hiyo kitu ambacho ni muujiza kwetu,..Kwa mjuzi/wajuzi wenye elimu juu ya jambo husika inakua sio muujiza bali ni elimu tu inatumika.
 
Back
Top Bottom