nielezee binadamu na viumbe vilitokanaje weka fact maana mm nmesoma hizo theory za evolution sijaonafact yoyote ambayo unaweza kuprove mindi u nmesoma hyo koz chuo kikuu nieleweshe hapo
Kiranga alitokana na nyani au cynobacteria?? ilikuwaje kuwaje
Kwenye sayansi kuna vitu vinavyojulikana na vitu visivyojulikana.
Sayansi ni mchakato endelevu, haujamalizika, hivyo, hauna majibu yote.
Wanasayansi wanajitahidi kupunguza visivyojulikana na kuongeza vinavyojulikana.
Kwa nadharia, experiemets, observation, peer review etc.
Na tunaweza kujua jibu fulani si sahihi, hata kabla hatujajua jibu sahihi ni lipi.
Yani ni hivi, tunaweza kujua square root ya 2 si 10, bila hata kujua square root ya 2 ni nini.
Tunaweza kujua kwamba mwanamme mwenye miaka 30 leo, ambaye hamjui mama yake mzazi, hawezi kuwa na mama mzazi mwenye umri wa miezi 6 leo. Hata kama hatumjui mama mzazi wa huyo mwanamme.
Tunaweza kujua kwamba Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote si chanzo cha ulimwengu huu, hata kama hatujui chanzo cha ulimwengu ni nini.
Mimi ninachosema ni kwamba, watu na viumbe wengine hawajatokana na kuumbwa na Mungu huyo. Naweza kusema hilo kwa uhakika, bila hata kujua wametokeaje.
Katika kutafuta jibu, tunaweza kutafuta jibu limelalia upande gani kwa kufanya "elimination method", kuindoa upande usio sahihi, na kujua kwamba, hata kama hatujajua jibu kamili ni lipi, tunaweza kujua kwamba jibu haliwezi kuwa upande fulani.
Ndivyo hivyo tunajua kwamba, square root ya 2 haiwezi kuwa kubwa kuliko 2, hivyo, mtu akituambia kuwa 10 ni square root ya 2, tutajua huo ni uongo. Bila hata ya kujua square root ya 2 ni ipi.
Mimi sijawahi kusema najua chanzo cha watu na viumbe ni nini, na wala sihitaji kujua chanzo ili kujua kwamba chanzo si Mungu.
Mimi ninasema kwamba chanzo cha watu, viymbe, ulimwengu, si Mungu huyo, kwa sababu tumeweza kuonesha kuwa Mungu huyo hayupo.
Hapa n8nekuja kusema kwamba, 10 haiwezi kuwa squarw root ya 2. Naweza kujua hilo bila hata ya kujua square root ya 2 ni ipi.
Wewe unaniukiza, square root ya 2 ni nini?
Mimi sijawahi kusema naijua square root ya 2 ni nini. Nimesema tu kwamba 10 haiwwzi kuwa squarw root ya 2, na naweza kujua hilo bila hata kujua square root ya 2 ni nini.