Dini zingesambazwa kama ambavyo Atheism inasambaa sidhani kama zingekuwa na wafuasi wengi hivi

Dini zingesambazwa kama ambavyo Atheism inasambaa sidhani kama zingekuwa na wafuasi wengi hivi

Namna ambavyo Atheism inasambaa ulimwenguni kwa sasa kadiri miaka inavyo songa katika njia ya amani inanipa faraja na kusema hii ndio njia ambayo dini ilipaswa kuitumia.

Huwezi kuta Atheists wanatumia nguvu kubwa kama vita, kuchinja watu, kulipua watu ili wasiamini kuwa kuna Mungu lakini haya matendo yasiyo ya kistaarabu yamefanywa sana na dini mbalimbali ili Mungu wao na mafundisho yao yaaaminiwe na kukubalika vizazi na vizazi.

Mafundisho ya vitisho vingi wamejaa katika usambazaji wa dini tofauti na njia ya amani haya matendo huwezi kuta Atheists wanafanya kulazimishwa watu .

Kuwa atheist imekuwa njia rahisi sana na inayo kubalika na kukua kwa kasi katika maeneo mbalimbali kwa sababu kinacho hitaji ni kuwa huru kufungua uwezo wako wa kiakili, elimu na kuwa huru kuhoji basi ni rahisi kuwa atheist hii ni tofauti na dini.

Dini zingetumia njia ya amani sidhani kama ingekuwa rahisi wao kujipatia wafuasi hawa wengi walio nao
Ingekuwa specific dini inayolazimisha maana sio zote 😅
 
Dini ni ya watu wasiojitambua , wanaojitambua hawahitaji vitisho na ahadi za kidini kufanya mambo mema( utu).

Ukiona mtu anafanya mambo mema kisa ahadi za Peponi na vitisho vya jehanam jua huyo hajitambui.

Ukitoa tu hivyo vitisho na ahadi huyo mtu atakua zaidi ya mnyama .

Atheists ni watu wanaojitambua kiakili na kiutu , Atheists ndio asili ya kila binadamu .
 
Dini kama zingetumia nguvu africa zingetoka kama mkoloni ...Dini zilikuja na nasaha ni mpango wa Mungu kusambaa ...Watu wameacha tamaduni zao miaka sembuse dini miaka kibao wangeachana nazo.

Sasa kaangalie dini ipi inakuwa zaidi? Yaani wanadai zimeanzia mashariki ya kati ila mpaka America zimefika....je Wazungu ni dhaifu mpaka kuingia kweny dini😅😅
Mbona wameshindwa kutoboa Asia hasa India na Uchina? Kwani wazungu wewe unawachukuliaje? Wazungu nao wanatawalika vizuri tu. By the way Mimi naona utamaduni ambao ni strong na haitawaliki kirahisi ni wahindi na dini yao. Jamaa wametoboa kwenye biashara Dunia nzima. Kwenye siasa ndio usiseme, wanaongoza nchi zote kubwa duniani USA, uingereza etc
 
Wewe leta hiyo historia ya watu kulazimishwa kuwa Atheists Urusi na China au unachanganya utekelezaji wa ukomunisti kisiasa
Stalin serikali yake ni Atheist government na watu waliuliwa sababu ya dini zao na kuwa forced Atheist, Fascism na Communism zote ni Atheist ideology ama hufahamu? Ukipenda boga penda na ua lake.

Soma hapo inaelezea vizuri kabisa

 
Mbona wameshindwa kutoboa Asia hasa India na Uchina? Kwani wazungu wewe unawachukuliaje? Wazungu nao wanatawalika vizuri tu. By the way Mimi naona utamaduni ambao ni strong na haitawaliki kirahisi ni wahindi na dini yao. Jamaa wametoboa kwenye biashara Dunia nzima. Kwenye siasa ndio usiseme, wanaongoza nchi zote kubwa duniani USA, uingereza etc
Majority ya hao wahindi unaowasifia sio wahindu ni waisilamu ama Atheist. Wafanyabiashara na Viongozi wengi toka India ambao wamefanya vizuri nje ya India ni Ismailia, Mabohora, ahmadiya etc nenda mjini utawaona, ndo hao hao wapo Canada, UK etc.
 
Mbona wameshindwa kutoboa Asia hasa India na Uchina? Kwani wazungu wewe unawachukuliaje? Wazungu nao wanatawalika vizuri tu. By the way Mimi naona utamaduni ambao ni strong na haitawaliki kirahisi ni wahindi na dini yao. Jamaa wametoboa kwenye biashara Dunia nzima. Kwenye siasa ndio usiseme, wanaongoza nchi zote kubwa duniani USA, uingereza etc
China na india nenda Kaangalie ? Wewe kijana unatokea wapi?😅😅😅China ina waislamu mil 23 mpaka sasa kutoka zero...Kaangalie dini zipo kila kona.
 
Watu wanajiuliza maswali walio aminishwa kwenye dini wanaona walipigwa mkuu.
Sasa atheism ndio kuna majibu? Ndio maana nasema atheists wengi ni watu waliyoshindwana na dini ndio wanarukia atheism ila hakuna cha kufungua akili wala nini. Hadi leo mimi sijawahi kuona hoja ya msingi kwenye atheism.
 
Sasa atheism ndio kuna majibu? Ndio maana nasema atheists wengi ni watu waliyoshindwana na dini ndio wanarukia atheism ila hakuna cha kufungua akili wala nini. Hadi leo mimi sijawahi kuona hoja ya msingi kwenye atheism.
Umeamua tu usione hoja kutoka na Ahadi za peponi ulizopewa kwenye dini .

Watu wengi wamefungwa na imani kwa sababu ya fear of unknown.
 
Theism inaboresha maelezo jinsi muda unavyoenda na sayansi na teknolojia zinavyobadilika. Kwa hiyo majibubyatapatikana leo au siku zijazo
Sayansi yanawahusu wote mwenye kuamini Mungu na asiyeamini Mungu, tunaweza kutofautiana baadhi ya mambo huko kwenye sayansi ila mwisho wa siku wote sayansi inatuhusu.
 
Sayansi yanawahusu wote mwenye kuamini Mungu na asiyeamini Mungu, tunaweza kutofautiana baadhi ya mambo huko kwenye sayansi ila mwisho wa siku wote sayansi inatuhusu.
Kwa hiyo kwa nini hamtumii vitabu vya sayansi kwenye mahubiri yenu?
 
Umeamua tu usione hoja kutoka na Ahadi za peponi ulizopewa kwenye dini .

Watu wengi wamefungwa na imani kwa sababu ya fear of unknown.
Mkuu mwenyewe umeeleza hapo kuwa watu wanaingia atheism baada ya kukosa majibu kwenye dini zao, nachojua kuachana na dini hakukufanyi moja kwa moja kuwa atheist kuna mitazamo mingi kuna member juu huko amiesema yeye sio mkristo wala muislamu na pia hakubaliani na atheism. Sasa kuna hoja zipi za msingi kwenye atheism?

Yani nikiona sielewi elewi dini basi nikimbilie kuwa atheist? Ndio mnaita kufungua akili?
 
Mkuu mwenyewe umeeleza hapo kuwa watu wanaingia atheism baada ya kukosa majibu kwenye dini zao, nachojua kuachana na dini hakukufanyi moja kwa moja kuwa atheist kuna mitazamo mingi kuna member juu huko amiesema yeye sio mkristo wala muislamu na pia hakubaliani na atheism. Sasa kuna hoja zipi za msingi kwenye atheism?

Yani nikiona sielewi elewi dini basi nikimbilie kuwa atheist? Ndio mnaita kufungua akili?
Yes, kujadili hoja iliyopo kwa kutumia sayansi iliyopo
 
Back
Top Bottom