Dini zingesambazwa kama ambavyo Atheism inasambaa sidhani kama zingekuwa na wafuasi wengi hivi

Dini zingesambazwa kama ambavyo Atheism inasambaa sidhani kama zingekuwa na wafuasi wengi hivi

Kwa hiyo kwa nini hamtumii vitabu vya sayansi kwenye mahubiri yenu?
Sayansi ni sayansi na dini ni dini, hata hivyo sayansi imesaidia kuelewa baadhi ya mambo kwa vizuri kutoka kwenye vitabu vya dini.
 
Inasmbazwa,ipo kwenye new world order pamoja na ushoga,inasmbazwa kupitia nadharia za kisayansi,ukishasimama kusema hakuna Mungu vitu vyote vimetokea kwa mlipuko tu,hapo unahubiri atheism hata Kama huna msikiti Wala kanisa

Mungu yuko wapi?hakuna mwenyejibu kamili ibaki kuwa nadharia tu ya waaminio,ili uamini lazima ujitoe akili,ukihoji wanasema unakufuru,
 
Dini kama zingetumia nguvu africa zingetoka kama mkoloni ...Dini zilikuja na nasaha ni mpango wa Mungu kusambaa ...Watu wameacha tamaduni zao miaka sembuse dini miaka kibao wangeachana nazo.

Sasa kaangalie dini ipi inakuwa zaidi? Yaani wanadai zimeanzia mashariki ya kati ila mpaka America zimefika....je Wazungu ni dhaifu mpaka kuingia kweny dini
 
Mkuu mwenyewe umeeleza hapo kuwa watu wanaingia atheism baada ya kukosa majibu kwenye dini zao, nachojua kuachana na dini hakukufanyi moja kwa moja kuwa atheist kuna mitazamo mingi kuna member juu huko amiesema yeye sio mkristo wala muislamu na pia hakubaliani na atheism. Sasa kuna hoja zipi za msingi kwenye atheism?

Yani nikiona sielewi elewi dini basi nikimbilie kuwa atheist? Ndio mnaita kufungua akili?
Basi sawa kila mtu aishi tu apendavyo sioni vibaya mtu akiamini Mungu yupo au asiamni .

Binafsi siamni Mungu yupo na sitakaa nishikwe kwenye huo mtego.
 
Sayansi ni sayansi na dini ni dini, hata hivyo sayansi imesaidia kuelewa baadhi ya mambo kwa vizuri kutoka kwenye vitabu vya dini.
Yoshua alisimamisha jua, ukoma ni laana kutoka kwa Mungu , sayansi imesaidia uelewe nini apo?
 
Msingeshindana kufungua nyuzi za kuponda wanaoamini katika Dini, Nyie mkipewa mamlaka ndo mtakuwa wa kwanza kuchoma nyumba zote za ibada
Kuna wayu wengi wenye iwezo mdogo kiakili na matapeli ndiyo wamekimbilia kwenye dini sababu kule ni swala la kuaminibtu bila ushahidi sababu imeandikwa. Huko wamejibebea wafuasi na umaarufu, wakati huohuo dunia inajikita kwenye kuhoji hao waliokimbilia kwenye dini hawana majibu zaidi ya kusema imeandikwa.
Lama ni kuandikwa vimeandikwa vingi sana.
Mfano Katiba ya Tanzania inaposema binaadam wote ni sawa, Je wewe unaamini katika hilo?
Imaposema hakuma aliye juu ya sheria, je umaamini?
Katiba inapinga ubaguzi, lakini kuna vyama vimekuja na ubaguzi usio na tija. Vina katiba iliyo kinyume na katiba ya nchi. inalekeza vyama vyao kwamba wateule katika nafasi za uwaziri ni lazima watokane na vyama vyao, hapo tayari vinalea ubaguzi sababu tu ya tofauti ya itikadi kisiasa badala ya kuziweka pamoja tofauti hizo za kiitikadi ili kutafuta suluhu za matatizo ya nchi.

Inaposema kufanya kazi ni haki ya kila mmoja, yaani haki inatolewa na Katiba lakini serikali haihangaiki kutengeneza mazingira ya ajira mpya kulingana na mahitaji.
Watu wameona Katiba inawapumbaza, inadanganya kutoa haki wakati hakuna misingi ya kuwajibishana.

Wameamua kuipuuza na kuendelea na maisha yao. Sasa kwanini maandiko nayo yasipuuzwe pale yanapoonekana kutojibu maswali na shida za watu? Watu wanajikuta wanakusanywa na kuishi kwa ajili ya dini, badala ya dini kuwepo kwa ajili yao. Wamegoma mafundisho ya kuwapumbaza na kuwajengea hofu, na ahadi za Kikamali, yaani maisha mazuri baada ya kifo.
 
Dini ni ya watu wasiojitambua , wanaojitambua hawahitaji vitisho na ahadi za kidini kufanya mambo mema( utu).

Ukiona mtu anafanya mambo mema kisa ahadi za Peponi na vitisho vya jehanam jua huyo hajitambui.

Ukitoa tu hivyo vitisho na ahadi huyo mtu atakua zaidi ya mnyama .

Atheists ni watu wanaojitambua kiakili na kiutu , Atheists ndio asili ya kila binadamu .
Maneno ya mtu wenu akimtamka Yesu
Screenshot_20240130_161825_com.android.chrome.jpg
 
Basi sawa kila mtu aishi tu apendavyo sioni vibaya mtu akiamini Mungu yupo au asiamni .

Binafsi siamni Mungu yupo na sitakaa nishikwe kwenye huo mtego.
Kweli kila mtu aishi apendavyo mwenye kuona kuamini Mungu yupo kuna mashiko basi aamini na mwenye kuona kudai hakuna Mungu kuna mashiko basi asimamie huo msimamo na mwenye kuona hakuna njia ya kujua uhakika wa kuwepo au kutokuwepo Mungu nao pia washikile huo msimamo, tatizo hapa ni mmoja kujiona et kwamba ana akili sana kwa kushikilia huo msimamo aliyonao.

Ila binafsi ni bora agnostic kuliko atheist.
 
Kweli kila mtu aishi apendavyo mwenye kuona kuamini Mungu yupo kuna mashiko basi aamini na mwenye kuona kudai hakuna Mungu kuna mashiko basi asimamie huo msimamo na mwenye kuona hakuna njia ya kujua uhakika wa kuwepo au kutokuwepo Mungu nao pia washikile huo msimamo, tatizo hapa ni mmoja kujiona et kwamba ana akili sana kwa kushikilia huo msimamo aliyonao.

Ila binafsi ni bora agnostic kuliko atheist.
Ni mtazamo wako tu , kwa sababu hata hao wanao amini Mungu kila mmoja anaamni Mungu wenye sifa na tabia tofauti na mwenzake na kila mmoja anaona mwingne kapotoka .
 
Msingeshindana kufungua nyuzi za kuponda wanaoamini katika Dini, Nyie mkipewa mamlaka ndo mtakuwa wa kwanza kuchoma nyumba zote za ibada
Binafsi nimekuwa mtetezi wa uhuru wa kuamini na kuabudu, pamoja na wa kutoanini na kutoabudu, kwa watu wote.

Mara nyingi tu, nilisema hii ni haki ya kikatiba, ni haki ya kiutu, imewekwa kwenye mikataba ya kimataifa, mpaka kwenye Universal Declaration of Human Rights.

Nilitoa mfano wa kupinga msimamo wa rais Kagame aliposema kuwa wachungaji wa makanisa wawekewe sharti la kuwa na degree ya chuo kikuu, nikisema sharti hilo linaingilia uhuru wa kuabudu.

Nilienda mbali kabisa na kusema kuwa, kimsingi, uhuru wa kuabudu ni upande mmoja wa shilingi ile ile ambayo upande wake wa pili ni uhuru wa kutoabudu., hivyo, kumvunjia mtu uhuru wake wa kuabudu, kutapelekea mmomonyoko wa uhuru wangu wa kutoabudu.

Nilisema pia, ingawa mimi si muumini wa dini yoyote na siamini hata katika uwepo wa Mungu, nitasimama na wanaoamini kat8ka kutetea uhuru wao wa kuabudi.

Kuna siku nilipata matatizo kutoka kwa jamaa mmoja atheist ambaye uelewa wake kwenye hiki suala ulikuwa finyu.

Rekodi za JF zipo, zitaonesha haya yote.

Naomba unitoe katika hilo kundi na uelewe kuwa dhana yabkwamba kila atheist anataka kuchoma na kufungia makanisa na misikiti ni dhana potofu.

Naweka mfano mmoja wa post hizi, huu ni wa August 2023.

Post in thread 'Rais Paul Kagame aahidi kuwasweka gerezani mahujaji wa Kikatoliki wanaotukuza ufukara' Rais Paul Kagame aahidi kuwasweka gerezani mahujaji wa Kikatoliki wanaotukuza ufukara
 
Ni mtazamo wako tu , kwa sababu hata hao wanao amini Mungu kila mmoja anaamni Mungu wenye sifa na tabia tofauti na mwenzake na kila mmoja anaona mwingne kapotoka .
Ndio ni mtazamo wangu kutokana na uelewa wangu na jinsi navyoona hoja za hao atheists ambazo kwa kiasi kikubwa zinaishia katika mitazamo ya kidini zaidi kuliko suala la kuwepo au kutokuwepo kwa Mungu na ndio maana wale wasio na dini ila wanaamini Mungu huwa hawana shida na hoja za atheists maana zinashambulia dini zaidi.
 
Dini ni ya watu wasiojitambua , wanaojitambua hawahitaji vitisho na ahadi za kidini kufanya mambo mema( utu).

Ukiona mtu anafanya mambo mema kisa ahadi za Peponi na vitisho vya jehanam jua huyo hajitambui.

Ukitoa tu hivyo vitisho na ahadi huyo mtu atakua zaidi ya mnyama .

Atheists ni watu wanaojitambua kiakili na kiutu , Atheists ndio asili ya kila binadamu .
Stephen hawking kabla hajafa alisema haamini kwenye Mungu ila alizikwa kikristo
 
Maneno ya mtu wenu akimtamka Yesu View attachment 2888868
Kwanza atheism si dini, hivyo haina mtume wala "mtu wetu".

Pili, hizo habari hazithibitishiki. Yani kuna nesi aliripotiwa kusema kuwa Voltaire alisema hivyo wakati anakufa. Nurse hana hata mtu wa pili kuwa shahidi wa ku corroborate story. Maana yake nesi anaweza kuwa muumini aliyetaka kupandikiza maneno kwa Voltaire tu.

Hearsay, baseless, unfounded, unverified, uncorroborated claim.

Lakini zaidi ya yote, hata kama Voltaire alisema hayo kweli, atheism haiendeshwi na maneno ya mtume mmoja, kila mtu ana akili zake na anapima mambo kimantiki mwenyewe. Na Voltaire kafa zamani sana wakati mambo mengi hayajagunduliwa, kwa nini tujali alichosema Voltaire?

Hizo tabia za kujali walichosema mitume wa zamani ni tabia za dini. Hizo ndizo tabia ambazo atheists wanazikataa katika dini.

Sasa kwa nini unataka kuturudisha katika dini kusujudia maneno aliyoyasema mtu aliyekufa mwaka 1778?

Kumalizia, moja ya vitu ninavyopenda katika atheism ni kukataa logical fallacy ya appeal to authority. Tunakataa authority ya Mungu, mitume, Voltaire. Tunakwenda na reason.

Sasa katika ulimwengu huo, hata ukimchafua Voltaire, hilo si muhimu kwetu, kwa sababu hatuendi kwa authority ya mtu, tunajua kufuata authority ni logical fallacy.

Tunakwenda kwa reason.
 
Back
Top Bottom