Diversity Visa 2020 Green Card Lottery Starts Today!

Diversity Visa 2020 Green Card Lottery Starts Today!

Nenda mlimani city au mayfair ukiwaambia passport za green card(wanaita hivyo) watakupatia, nenda na flash yako kabisa.
Piga passport kwa kutumia simu kisha nenda Play store download US visa passport utaiedit. Simple tu, sasa upeleke familia nzima studio kwaajili ya bahati nasibu
 
Majibu ya nyodo na kejeli pasipo na hoja ndani yake ni 'uxhoga', unapozungumza na mwanajukwa mwenzako si vyema kujibu kwa kuzodoa bila hoja ndani yake. Lengo ni kuangalia generally na kwa ujumla wake kama kuna tija ya wasomi tuliosomesha kwa gharama kubwa kwenda kutumikia nchi za wenzetu na kuacha fursa mbalimbali za kulikwamua taifa hapa lilipo, sio tukiona meli inazama tunaanza kuruka na kuikimbia, lazima tuangalia namna ya kuiokoa, hilo ndio la msingi hapa. Nimekupa hoja ya extreme racial bias na profiling huko USA hasa hasa katika utawala huu wa Trump, wewe unajibu eti bora tukatumikishwe na kubaguliwa na wazungu kuliko kubaguliwa kisiasa / na wahindi; sasa kweli hii ni sababu ya kuikimbia Tanzania? Kule Marekani uliza kama kuna watz hata 10 wanaomiliki nyumba kule, na uliza hao watz walipoondoka waliacha nyumba ngapi huku, it doesn't make sense? Utakesha kulipa bills za maji, umeme, rent/mortgage maisha yako yote, bafo upambane na mibaguzi ya rangi, its bullshit, tusiingizane cha kike!
Unapayuka maneno kibaao wakati hakuna ata point 1 kama hawamiliki majumba lakini hao hao ndio wanaitwa wafalme kwenye jamii wanakotoka mm nina mtoto wa shngaz alienda huko anakaa kwenye apartment Kentucky lakn anasomesha watoto wa dada zake tena wawil wanasom Feza mmoja now anamalizia IFM kwa pesa ya mpangaji USA na hakuwa na elimu ya kueleweka just a certificate ila ndio alipata zali la mentali but now anamalizia masters na kazi anafanya. Sijui kama angebak TZ angekuwa wap, kama unaona kupanga ULAYA ni mbaya sasa mbona TZ watu wanaishi kwenye nyumba za kupanga mpaka wanatoka mvi tena chumba na sebule tu.
Wewe baki ujalazimishwa kwenda ila ukumbuke kuwa USA itabaki USA tu ata mchina , mwingereza nao wanatamani kwenda USA utakuwa wewe.
Mtoto wa Fernandes anawadanganya et mzalendo kaacha kazi ya mamilioni kuja nyumbani lakin unashndwa kutambua kuwa yule ni kama MO tu coz utajiri alionayo baba yake ni haki yake arud nyumbani ili apewe nafasi ya kurithi makampuni ya baba yake maana ata MO alipotoka Duniani alikuja tu kuchukua nafasi.
TANZANIA hii hii tunabaguana kwa ukanda, ukabila japo tunajaribu kuiwekea mwavuli lakin kama umejiajiri na unazungukaga kutafuta tender huku na huku ndio utajua ni bora ubaguliwe na mzungu kuliko mwafrica mwenzangu tena wa nchi mmoja......
NB: MTU AKIFA ULAYA ANASAFIRISHWA KUJA KUZIKWA AFRICA ILA MZUNGU AKIFA KWETU ANAZIKWA HUKUHUKU uhue kuwa kwetu ina hadhi ya kama Makaburi hivi..
 
Kwani lilipoletwa hili tangazo la green card visa lottery humu jamvini lengo lilikuwa ni nini? Na kwakuwa tangazo limeletwa jamvini basi wanajamvi hatuwezi kuliacha tu hivi hivi, maana wapo watakaoshawishika, hivyo ni muhimu mjadala ufanyike ili wale watakaoshawishika hata kwenda kwa njia zingine (achilia mbali hiyo lottery) wajue wanaenda wapi. Suala la Tanzania kuwa na ubaguzi sawa na Marekani siwezi kubisha sana, ila sasa kwanini uende sehemu ambayo haina unafuu? Si ningetegemea ukimbie ubaguzi Tanzania ila uende sehemu isiyo na ubaguzi? Hilo suala la kutoweza kumiliki nyumba na ardhi USA na wewe ukaona ni bora kuliko sehemu ambayo unaweza ukamili nyumba na mashamba/ardhi ya kwako mwenyewe limenishtua. Yaani kuishi kama ndege/ ngedere kwenye vi-appartment kama vitundu vya ndege au ngedere mtini wewe unaona ni bora kuliko kumiliki nyumba na ardhi ya kwako, nina wasiwasi na afya yako ya akili.
Unakaa mkoa gani? inabidi unipe jibu maana swala la appartment ata dar es salaam watu wengi tu wanakaa na wanazeekea humo kuanzia Upanga, kariakoo, Ilala, Magomeni, Kawe, Masaki, Oysterbay, Mikocheni, nk sasa sijui appartment za huku na za kule zina utofauti gani au umezoea GIZA nini hahahhaha.......
Alafu Hapa duniani hakuna nchi iliyo perfect kwa kila kitu africa kwenyew tz tunajua wenyew, kenya ukabila, kwa madiba kule ni rangi, ukipanda juu kule nako ni shida, Waliozoea maisha ya ksng sng ya umbea umbea ndio wanapenda huku maana kule kila mtu ana time yake. Africa ni africa, Tanzania ni tanzania tu na USA itabki kuwa USA mwingereza na kutawala kote dunia nzima lakin lazima akanyage ardhi ya Manhattan NYC, Los Angeles, Las Vegas hatar sana wewe yaan kule ni sawa na Diamond tu usoni utasema namchukia ila Beat zake zikipigwa moyoni unacheza..
Bora ukabebe mabox USA wazazi waishi kama wazazi wa waziri kuliko uajiriwe TZ alaf uishi kwa stress kwanza huku KULOGANA kumezid mpaka mashambani shida, biashara ndio usiseme, ofisin shida kwenye tender balaa yaan.... All the time I say to live in TZ you must be Granted exceptional TALENT.
 
Kwani lilipoletwa hili tangazo la green card visa lottery humu jamvini lengo lilikuwa ni nini? Na kwakuwa tangazo limeletwa jamvini basi wanajamvi hatuwezi kuliacha tu hivi hivi, maana wapo watakaoshawishika, hivyo ni muhimu mjadala ufanyike ili wale watakaoshawishika hata kwenda kwa njia zingine (achilia mbali hiyo lottery) wajue wanaenda wapi. Suala la Tanzania kuwa na ubaguzi sawa na Marekani siwezi kubisha sana, ila sasa kwanini uende sehemu ambayo haina unafuu? Si ningetegemea ukimbie ubaguzi Tanzania ila uende sehemu isiyo na ubaguzi? Hilo suala la kutoweza kumiliki nyumba na ardhi USA na wewe ukaona ni bora kuliko sehemu ambayo unaweza ukamili nyumba na mashamba/ardhi ya kwako mwenyewe limenishtua. Yaani kuishi kama ndege/ ngedere kwenye vi-appartment kama vitundu vya ndege au ngedere mtini wewe unaona ni bora kuliko kumiliki nyumba na ardhi ya kwako, nina wasiwasi na afya yako ya akili.
Unakaa mkoa gani? inabidi unipe jibu maana swala la appartment ata dar es salaam watu wengi tu wanakaa na wanazeekea humo kuanzia Upanga, kariakoo, Ilala, Magomeni, Kawe, Masaki, Oysterbay, Mikocheni, nk sasa sijui appartment za huku na za kule zina utofauti gani au umezoea GIZA nini hahahhaha.......
Alafu Hapa duniani hakuna nchi iliyo perfect kwa kila kitu africa kwenyew tz tunajua wenyew, kenya ukabila, kwa madiba kule ni rangi, ukipanda juu kule nako ni shida, Waliozoea maisha ya ksng sng ya umbea umbea ndio wanapenda huku maana kule kila mtu ana time yake. Africa ni africa, Tanzania ni tanzania tu na USA itabki kuwa USA mwingereza na kutawala kote dunia nzima lakin lazima akanyage ardhi ya Manhattan NYC, Los Angeles, Las Vegas hatar sana wewe yaan kule ni sawa na Diamond tu usoni utasema namchukia ila Beat zake zikipigwa moyoni unacheza..
Bora ukabebe mabox USA wazazi waishi kama wazazi wa waziri kuliko uajiriwe TZ alaf uishi kwa stress kwanza huku KULOGANA kumezid mpaka mashambani shida, biashara ndio usiseme, ofisin shida kwenye tender balaa yaan.... All the time I say to live in TZ you must be Granted exceptional TALENT.
 
1.) Umeshindwa kuelewa nilichozungumza lakini umeweza kunijibu, very intresting.

2.) Sio kwamba nalazimisha, ndivyo ilivyo, nimeweka link ya 'advise show tv', ingia ili uone kama racism against black ni jambo ambalo nalazimisha au kweli lipo huko USA.

3.) Sijasema kila mTanzania anaweza kumiliki Ardhi kiholela, ninachosema ni kwamba, kama umeshindwa kumiliki nyumba/ardhi Tanzania, basi sahau kumiliki nyumba/ Ardhi marekani, na nikakupa mfano kwamba watz wanaomiliki nyumba USA sidhani kama hata 10 wanafika.
Sasa watanzania wangap wanabaguliwa humu humu au ujawahi kuingia mtaani bado unasoma? Kwenye ajira kwenyewe ubaguzi unazid wenye mioyo migumu ndio wanakomaa.
Alaf swala la kumiliki mali ni kitu differnt kabisa yaan unaweza ukakaa TZ ukashndwa ata kujenga chumba kimoja na ukazikwa ukiwa umepanga labda uwe unakaa kijijini na mtu mwingine akaenda let say Jo'burg na akawa na maisha mazur kweli kweli.
Wakat namaliza f4 my best friend hakufanya vizur kabisa so hakuweza kuendelea na masomo akaingia mtaani kama miaka miwl hvi coz kwao walikuwa wapo vizur kidogo kifedha aliniaga kuwa anasepa TZ akachukua kama 5M akaenda zake Jo'burg jamaa alikuja tmwaka jana daah yaan life aliyonayo nadhani ata mtu angelipwa 3M/ month bado anaweza tu akawa kora kwake, suala la nyumba sio shida tena ambayo mdao anazungumzia maana familia yake (wazazi) kawabadilish mpaka raha na nyumba kajenga MBEZI ya kimara ila sisi wazalendo tunaojifanya tumekunywa maji ya bendera bado hatuelew somo maana unaanzisha biashara lakin inamalizwa na mnyama anaitwa tra.
Example zipo nying na jamaa ambae nilikutana nae tu kwenye utafutaji kupitia kwa rafiki yangu alikuwa KORA tu ila sasa hivi ananunua Diamonds Shy bush na kupeleka SA coz yeye now anaish Pretoria.
Wewe ukiona TZ inakufaa kaa ujalazimishwa maana ata Human rights declaration imestate vizur tu kuhusu mahali pa kuish na ata MUNGU alipoumba dunia alimweka binadamu atawale dunia yote so mipaka tulijiwekea wenyew kwa utashi wetu.
NB: Sasa sio tunasepa alafu mnaanza kusema ooh msaidie nchi yenu kwenye diaspora
 
Achana nae huyo jamaa !! wapo watu wengi tu wanatafuta chance ya kwenda kwa Trump haya mambo ya Ubaguzi yapo kila mahali, Nenda India, china, sehemu nyingi Tu!! Sio binadamu wote wanaweza onesha ubaguzi..kuna wazungu sio wabaguzi kabisa na wanachukia ubaguzi na kuna wengine wabaguzi!! Tena sijui watanzania tuna shida gani mtu anapoleta opportunities tunaanza kuangalia dark side Nenda USA nenda UK the Nigerians wamejaa tele wanafanya life na wanasaidiana kutoboa.
Nigeria na china mpaka wamepigwa STOP yaan within a 5 years wamepeleka zaid ya watu 50,000. Angalia wakenya waliopo nje ya nchi wanavyosaidia ndugu zao yaan ata wa kwa MADIBA tu hapa yaan Nigerians, Kenyan, Ethiopian, pasipokusahau na somali hao jamaa wanasaidiana hatar yaan wakiona tu fursa wanaitana wote ndio maana ata Afrika kusini wamedominate sana. Lakini sisi ni majungu na roho ya korosho yaan mtu akipata chance hatak mwingine ajue kabisa angallia afrika kusini waTZ wanavyofanya vitu vya ajabu yaan ukijichanganya ata wewe Mtanzania mwenzake anakuingiza MJINI alaf anasepa..
Kwahyo ata hapa siwez kushangaa kauli tofaut maana KAMONGO mkubwa huw anawazaa Makamongo wadogo wadogo wengi
 
Sante sana kamanda.Je ni watanzania wangapi huwa wanajaribu na wangapi wanatoka kidedea kila mwaka kwa wastani?
Kujua idadi kamili ya watu wanaoomba huwa ni ngumu maana huwa wanatoa majina ya waliofanikiwa tu, mwaka wangu mimi tulipata watz 39 tu. Ila nchi nyingine kama Ghana, Ethiopia, kenya nk huwa wanachukuliwa wengi sana nazani wao watakuwa na muamko mkubwa wa kuomba hii kitu.
 
Kujua idadi kamili ya watu wanaoomba huwa ni ngumu maana huwa wanatoa majina ya waliofanikiwa tu, mwaka wangu mimi tulipata watz 39 tu. Ila nchi nyingine kama Ghana, Ethiopia, kenya nk huwa wanachukuliwa wengi sana nazani wao watakuwa na muamko mkubwa wa kuomba hii kitu.
Hongera sana kwa kupata tiketi ya ushindi
 
Assuming nimeshinda, watanipa pesa ya kuhamisha familia yangu kwenda huko? Na pia watanipa kazi ya kueleweka wao au mimi ndio nianze tena kusota kuanzisha biashara huko? Fafanua please.., na eleza kwanini niende kwenye nchi yenye high levels of Racial profiling kwa black people?
Kuaply sio lazima.. so kama unaona ni utumwa ni bora kuacha tu. Kiufupi hakuna unachopewa zaidi ya ww kujilipia kila kitu mpaka unaingia marekani.. na hata huko utajijua mwenyewe. Sisi tunaona kwenda marekani ni fursa tosha kwetu
 
Majibu yamekwishatoka, kwa wale mlioomba mwaka jana mnaweza kuangalia kama mmechaguliwa. Ikitokea hukuchaguliwa bado nafasi unayo unaweza kuomba tena mwezi October mwaka huu. Kila la kheri.
 
Majibu yamekwishatoka, kwa wale mlioomba mwaka jana mnaweza kuangalia kama mmechaguliwa. Ikitokea hukuchaguliwa bado nafasi unayo unaweza kuomba tena mwezi October mwaka huu. Kila la kheri.
Mkuu kwema? Nipo nahangaika kucheki tangu juzi ila naona mtandao upo busy sana ....
 
Back
Top Bottom