Dkt. Abbas na Msigwa lazima mazingira yenu ya kazi yawe magumu kufanya kazi na Nape Nnauye

Dkt. Abbas na Msigwa lazima mazingira yenu ya kazi yawe magumu kufanya kazi na Nape Nnauye

Unachotakiwa kujua mleta mada, hawa wateule wayasemayo siyo hiari yao, kama haujagundua hilo basi wewe ni mtoto, mara ya mwisho kusikia mteule au mtumishi ameacha kazi kwa sababu ya kutofautiana na boss wake au mamlaka ilikuwa lini??? Hao walikuwa kama vipaza sauti.
 
Nape mwenyewe hajawahi kuwa muumini wa uhuru wa kujieleza wala kuamini uhuru wa habari,
Hajawahi na hatawahi kwa mfumo huu huu wa CCM.
Na wala hajawahi kujiuzulu eti kwa kushindwa kuendana na utawala wa Magu tuache unafiki.
Kilichopo hapa ni kuwa Nape anataka kuonyesha tu ubaya wa mwendazake kwa vile tu hakuwa miongoni mwa wapendwa kwenye awamu ya Magu lakini sio kwa kuwa anapenda uhuru wa habari.
 
Back
Top Bottom