denooJ
JF-Expert Member
- Mar 31, 2020
- 18,509
- 68,228
Makamba mtoto wa mama arudi nyumbani, hakuna anapopaweza, kama mpaka mazingira yalimshinda anaweza wizara ya familia yake tu.Wizara ya Biashara angepewa January yule mama imemshinda kabisa!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Makamba mtoto wa mama arudi nyumbani, hakuna anapopaweza, kama mpaka mazingira yalimshinda anaweza wizara ya familia yake tu.Wizara ya Biashara angepewa January yule mama imemshinda kabisa!
Yaani huyu mbunge ni Bure kabisa50% ya wafanya biashara wa kariakoo wametoka makete amepima kwa tumbo sio?
Na posho juu anapata.ameamua kubadilisha maneno kutoka mgomo kuwa uhuru wa kufunga na kufungua maduka,
Yuko happy anagonga meza hana wasiwasi kiongozi shupavu aliyeaminiwa na Mh. Rais!
Uchawa + kujuanaDuu,watu kama hawa walipataje huo uwaziri?
Huyu jamaa anakuaga mbabe sana huyu.#HABARI Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla amewataka wafanyabishara wanaofanya biashara katika eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam, kuendelea na biashara hizo, baada ya wafanyabishara hao kugoma kufungua biashara hii leo...
Hoja ipi nzito hapo wewe PIMBI?Nchi ya ajabu sana hii hoja nzito inajibiwa na jibu la hovyo tena hovyo kabisa, stupid, pumbafu
Ulitaka hao wafanyabiashara wapigwe? Ni uhuru wao, wakitaka wafungue au wafunge ila sheria iko pale pale.Duu,watu kama hawa walipataje huo uwaziri?
Ni kweli kabisa wakinga ndio wanaokimbiza kariakooMbunge wa Makete mh Festo Sanga ameliambia bunge kwamba 50% ya Wafanyabiashara wa Kariakoo wanatoka kwenye Jimbo lake la Makete ( Wakinga)
Source TBC
Je, Sanga yuko sahihi au amelidanganya bunge?
Msamehe bure mkuu,50% ya wafanya biashara wa kariakoo wametoka makete amepima kwa tumbo sio?
Na wewe unakimbiza kipande ipi mwambaNi kweli kabisa wakinga ndio wanaokimbiza kariakoo
Kuna jipya gani?
😂😂😂Yote ya zamani, hakuna jipya
[emoji23][emoji23][emoji23]
Naona umeuliza kwa ID moja ukadhani unajijibu kwa ID nyingine Kumbe ileile
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la Bunge la 12 Mkutano wa 11, Kikao cha 25 leo Mei 15, 2023.
WAZIRI MASAUNI: SERIKALI HAIJAJIRIDHISHA URAIA PACHA NI MATAKWA YA WENGI
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni amesema “Bado Serikali haijajiridhisha kwamba uraia pacha ni takwa la Wananchi wengi, ndio maana hata katika mchakato wa katiba uliokwama hakukuwa na pendekezo, Serikali ipo katika hatua za mwisho kuanzisha utaratibu wa Hadhi Maalum kwa Watanzania waliochukua uraia wa Nchi nyingine.”
Awali, Mbunge Agnesta Lambert Kaiza alihoji kama Serikali haioni haja ya kuwasilisha Muswada wa marekebisho wa uraia Pacha akieleza kuwa kuwakana Watanzania wanaochukua uraia wa Nchi nyingine ni sehemu ya ubaguzi.
MWONGOZO KUHUSU MGOMO SOKO KUU LA KARIAKOO
Mbunge wa Makete Festo Sanga ameomba mwongozo wa Spika kuhusu mgomo unaoendelea kwenye soko la kariakoo ukihusishwa na kamata kamata pamoja na changamoto zingine za ukusanyaji wa mapato.
View attachment 2622501Sanga amesema kuendelea kwa mgomo huu kunakosesha taifa mapato, pia mikoa inatikisika kwa kuwa wafanyabiashara wengi nchini huchukua biadhaa hapo.
Festo Sanga, Mbunge wa Makete
Akitolea maelezo ya kinachoendelea kariakoo muda huu, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu Kijaji amesema "Kumekuwa na majadiliano ambayo yanaendelea kati ya Serikali na wafanyabiashara wetu ambao wapo kariakoo, kuhusu hoja zao mbalimbali ambazo wanatamani Serikali izifanyie kazi na mpaka sasa hivi tunapoongea Mhe. Spika, Mhe. Mkuu wa Mkoa pamoja na wataalamu wetu kutoka wizara ya fedha, wizara ya viwanda na biashara wapo kwenye kikao na uongozi wa wafanyabiashara wa kariakoo"
View attachment 2622490
Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Ashatu KijajiAmeongeza, "Na yapo baadhi ya maeneno ndani ya Kariakoo ambayo shughuli zinaendelea na wengine kama ilivyo uhuru wa kila mtu kufanya kile anachokiona, anatakiwa kukifanya, wengine wamefunga maduka yao wengine maduka yanafanya kazi"
Kwa mujibu wa Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson, Bunge halitajadili hoja hii kwa sasa hadi pale atakapojiridhisha kuwa madai ya Mbunge Festo Sanga yana ukweli, pia kwa kuwa jambo hilo linafanyiwa kazi na Mkuu wa Mkoa.
Katika Mwendelezo wa Sakata hili, Mbunge Hawa Mwaifunga amesimama kuomba pia mwongozo ambapo amesema Wafanyabiashara wamegoma kufungua maduka yao hadi siku ya Alhamisi watakapopatiwa majibu ya malalamiko yao.
View attachment 2622494
Hawa Mwaifunga, Mbunge wa viti maalumuAmedai pia kauli ya Waziri wa Viwanda kuwa baadhi ya maduka yamefunguliwa sio ya kweli kwa kuwa hakuna duka lolote lililofunguliwa, na kuna onyo kwa wafanyabiashara yeyote atakayefungua biashara ni halali ya wengine.
Waziri Dkt. Ashatu Kijaji amesisitiza kuwa "Wapo wafanyabiashara waliotumia uhuru wao kufungua maduka na wapo waliotumia uhuru wao kufunga maduka, ni demokrasia, hakuna mtu anayelazimishwa kufanya jambo"
Amesema kwa sasa Serikali bado ipo kwenye mazungumzo na wafanyabiashara na ikitokea kuna maelezo mengine atayatoa.
SPIKA ASITISHA BUNGE BAADA YA HITILAFU YA UMEME
Shughuli za Bunge Jijini Dodoma zimesitishwa kwa muda hadi saa kumi jioni kutokana na hitililafu ya umeme ndani ya Bunge
Spika Dkt. Tulia Ackson amelazimika kusikitisha shughuli hizo saa nne asubuhi ya leo Jumatatu Mei 15, 2023
Nyakati zile tusingekuwa naye huyu na hawa ndio wanamfanya maza aonekane hajui kulea watoto kuliko baba.Mbunge wa Makete Mhe. Sanga ameomba Bunge lijadili kwa dharura mgomo wa Kariakoo.
Spika amemuuliza Waziri wa Biashara ambaye amejibu hakuna mgomo ila Wafanyabiashara wametumia uhuru wao wa kufunga au kufungua.
Festo Sanga amesema anazo taarifa kamili kwa sababu 50% ya Wafanyabiashara wa Kariakoo wanatoka Makete.