Dkt. BITEKO na EWURA, Zuio la kuwauzia mafuta wateja wenye dumu (gallon) linaleta maafa vijijini kwa wakulima wanaotumia mashine za diesel na petrol

Unaweza kuwa una hoja lakini siyo mahala pake.
Ingependeza ungeshauri nini kifanyike kuondoa tatizo nililoleta hapa.
Mimi ni mkazi wa Dar lakini natafuta mkate shambani vijijini.
 
Kuna sheria mpya inaruhusu mwenye mtaji mdogo sana kufungua fuel station vijijini, hakuna tena ule utaratibu wa umbali mkubwa kati ya kituo kimoja hadi kingine.
Pia hakuna kile kigezo cha mtaji mkubwa.
Tatizo linakuja hata kama kila Kijiji au kitongoji kuna fuel station bado mwenye mashine hawezi kuibeba kwenda kujazia mafuta fuel station.

Ningeshauri waagize kila mtaa au Kijiji viongozi wasimamie watu wasiuze mafuta ya kwenye madumu na chupa za maji maarufu kama mafuta ya videbe.
Waruhusiwe kununua kwenye madumu au/na Jerry cane kwa matumizi binafsi.
 
Hii sheria au amri haikuzingatia maisha halisi ya nchi masikini kama Tanzania.
Mkuu hizi sheria ni wao wameamua tu lakini duniani kuna utaratibu hata kama ni nchi za magharibi wana utaratibu wa kununua mafuta ila kama wanataka wafanye kama huku nje
Kuna madumu ambayo bila hayo huwezi kuwekea mafuta
Dumu la kijani dogo kwa ajili ya Petrol na kubwa jekundu kwa ajili ya Diesel
Mbona miaka ya nyuma yalikuwepo na kukikuwa hakuna tatizo
Hatuwezi kuwa na sheria na zikawa rafiki why?
Kila kitu Kama tumeiga kwa mzungu kwa nia nzuri basi ziendelee hivyo hivyo

Wanipe tenda niyajaze huko
 
REA walione hili, haiwezekani hadi leo watu wanatumia mashinanza maafuta kisaga na kukoboa, ilihali umeme tunaao wa kutosha
 
REA walione hili, haiwezekani hadi leo watu wanatumia mashinanza maafuta kisaga na kukoboa, ilihali umeme tunaao wa kutosha
Mkuu kuna dharula barabarani, majenereta, n.k.
Kuna shughuli za kilimo au migodi midogo nje ya makazi ya watu maporini huko ambako REA hawawezi kupeleka umeme kwa watu wachache sana au mmoja.
Mimi nipo nje ya Kijiji mbali nimejitenga niweze kufuga na nguruwe bila kero kwa watu.
 
Naiona nyororo Ile ya zamani ikirejea...ilipelekea chopa ya jeshi kutua pale

Wamiliki wamalori,tujiandae kiakili malori kuanza kundondoka hovyo maeneo yasipotakiwa kundondoka
 
REA walione hili, haiwezekani hadi leo watu wanatumia mashinanza maafuta kisaga na kukoboa, ilihali umeme tunaao wa kutosha
REA kuhangaika na mafuta ni Sasa na Daktari kumuuzia mgonjwa dawa,wakati Kuna Pharmasia.

REA wamesambaza umeme na kuweka transformers ndogo, matumizi ni makubwa,tumeishia kwenye low voltage.

Nguzo wameweka za miti ,mchwa wameamza kuzila badala ya kuweka nguzo za zenge.

Sasa wataanza Tena kuondia nguzo za miti kuweka za zenge ni mradi na Kodi zetu.

Sasa waanze Tena kuuza mafuta???
 
Wasambaze.
Sasa hayapatikani kirahisi kama zamani.
Waruhusu madumu kwa muda ila iwe kwa muda maalumu wakati wanasambaza hayo maalum.
Mbona iliwezekana kwenye mifuko ya plastic na pombe za viroba.
Hukatazwi kununua mafuta kwenye kidumu bali kuna kidumu maalum kwa ajili ya petrol na diesel. Hili sio jipya. Huwezi kwenda kununua mafuta na dumu la maji ya uhai.
 
 
Ni sawa kwa upande wa dharura ,ila kilimo na migodini REA ipeleke umeme, hadi wewe mfuga nguruwe huko porini, unatakiwa ufikiwe na umeme, umeme tunao mwingi hadi tunafungulia mabwawa..
 
Ni sawa kwa upande wa dharura ,ila kilimo na migodini REA ipeleke umeme, hadi wewe mfuga nguruwe huko porini, unatakiwa ufikiwe na umeme, umeme tunao mwingi hadi tunafungulia mabwawa..
Mindset ya haya mashirika bado ipo nyuma karine nzima.
Wanataka faida badala ya huduma.
Hawawezi kuniletea umeme mtu mmoja 6KM kutoka kijijni, ukizingatia mimi mwekezaji mdogo ni start-up.
Sijaanza kufanya return yoyote ya investment.
 
Wasambaze.
Sasa hayapatikani kirahisi kama zamani.
Waruhusu madumu kwa muda ila iwe kwa muda maalumu wakati wanasambaza hayo maalum.
Mbona iliwezekana kwenye mifuko ya plastic na pombe za viroba.
Ni kweli hayo madumu hayapatikani kirahisi.
 
Kuna vidumu maalumu vya petrol waruhusu hivyo, kwa mfano hapo wizarani kwake akitaka mafuta ya Generator anapataje ? wasitufanye watanzania mbumbumbu..

View attachment 3110781
Usikute kuna mtu anataka kuleta biashara ya kuuza hivi vidumu. Kuna sehemu mtu yeyote anayenunua mafuta mkononi anatakiwa awe na dumu hili. Sehemu yoyote ya ujenzi inayotumia mafuta inatakiwa kuwa na dumu hili. Kuna mtu kaona fursa.
 
Kaka mimi mwaka huu huu wakati mafuta yamekuwa adimu nmeishiwa mafuta kwenye generator nikatuma boda sheli wakamkatalia wanasema aje na chombo husika ikabidi aje afunge generator aende nalo ndo wakamuuzia
Haya mambo ya ajabu kabisa.
Generators kubwa kabisa zile zinafungwa na mounting bolts au studs utafungua nati kisha utafunga kwenye boda au kwenye gari kisha ukafunge tena ukitoka sheli?
Mashine yangu ya maji ni kubwa kama power tiller za kulimia au mashine za kusaga, inabebwa na watu wanne au zaidi nifungue na kufunga tena?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…