Dkt. BITEKO na EWURA, Zuio la kuwauzia mafuta wateja wenye dumu (gallon) linaleta maafa vijijini kwa wakulima wanaotumia mashine za diesel na petrol

Imenilazimu kununua mafuta ya uchochoroni kimagendo ambayo ni hatari. Pia yanaweza kuwa machafu yakaharibu mitambo. Mafuta haya huchangia wizi wa mafuta na serikali inakosa kodi.
 
Badala ya kudhani wamepata suluhu kumbe wameongeza tatizo
 
Badala ya kudhani wamepata suluhu kumbe wameongeza tatizo
Huku mitaani kuna mapipa au madumu madogo ya bati (siyo Jerry cane) ndiyo wanaruhusu kununulia mafuta kwa sasa.
Haya mapipa hayajazuia biashara ya mafuta ya videbe. Yale ya kuweka kwenye chupa za maji za lita1 au nusu lita. Wanatunza majumbani ovyo kama kawaida.
Kwahivyo lengo la kuzuia hatari itokanayo na uuzaji mafuta holela halijatimia.
Limetimia lengo la waliotajwa kufanya biashara yao ya madumu/mapipa ya bati/chuma.
Hii nchi sijui itajiondoa lini kwenye utumwa wa mafisadi waliovaa koti la wanasiasa. Vijijini kote wanasema hiyo biashara ya watu siyo kuhusu usalama wa raia.
 
Naomba kusaidiwa taarifa - kwa hapa Dar wapi hizo Jerry can za chuma zinauzwa?
Nenda kaulizie maduka ya mashine na vipuri vya mashine mbalimbali kule Ilala CBD Posta, Morogoro road.
Barabara ya BRT (mwendokasi).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…