Dkt. Damas Ndumbaro: Wanaume tuliokuwa tunavizia Urais twende likizo, kazi anayoifanya Samia hakuna wanaume wanaoweza kuifanya

Dkt. Damas Ndumbaro: Wanaume tuliokuwa tunavizia Urais twende likizo, kazi anayoifanya Samia hakuna wanaume wanaoweza kuifanya

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Waziri wa Sheria, Damas Ndumbaro akiwa kwenye maadhimisho ya miaka 25 ya WILDAF yaliyohudhuriwa na Rais Samia amewataka wanaume wanaotaka kuwania Urais wakapumzike kwani aliyepo shughuli anaiweza barabara.

Ndumbaro ametaka wanawake waongoze nchi hata miaka 20 na kama wanaume wanataka kwenda kombe la dunia lazima Rais awe mwanamke kama wanawake walivyoweza kufika robo fainali.

=======

Damas Ndumbaro: Tumepata Rais wa kwanza mwanamke, sidhani kama kuna mafanikio makubwa kama hayo, rai yangu kwa nyinyi wanawake wapigania haki za wanawake, hapa tuliposhika tusiache.

Sisi kule Songea, wangoni tunaimba kwamba ninapotaka mimi ni hapa tu, sisi tunasema tunapotaka sisi ni hapo tu, tumefika.

Kwahiyo sisi wanaume ambao tulikuwa tunavizia vizia hii nafasi ya Urais hebu twende likizo kwanza. Hii shughuli sio yetu, siku hizi ina wenyewe hii, ndio ukweli na mbaya zaidi huyo mwanamke ambae ndio Rais kazi anayofanya hakuna wanaume ambao wanaweza kuifanya.

 
Ndumbaru ni jitu zima ovyo.

Ndumbaro.jpg
 
Hivi kwa nini Rais anakubali kudhalilishwa namna hii? Kila mtu anajua kwamba huyo Waziri hamaanishi anachosema kwa nini Rais anakubali kufanyiwa hivi?

Hata mtoto mdogo akisikia hayo maneno atacheka na kujua ni danganya toto, sasa kwa nini?
Too low!
 
Waziri wa Sheria, Damas Ndumbaru akiwa kwenye maadhimisho ya miaka 25 ya WILDAF yaliyohudhuriwa na Rais Samia amewataka wanaume wanaotaka kuwania Urais wakapumzike kwani aliyepo shughuli anaiweza barabara.

Ndumbaro ametaka wanawake waongoze nchi hata miaka 20 na kama wanaume wanataka kwenda kombe la dunia lazima Rais awe mwanamke kama wanawake walivyoweza kufika robo fainali.

=======

Damas Ndumbaru: Tumepata Rais wa kwanza mwanamke, sidhani kama kuna mafanikio makubwa kama hayo, rai yangu kwa nyinyi wanawake wapigania haki za wanawake, hapa tuliposhika tusiache.

Sisi kule Songea, wangoni tunaimba kwamba ninapotaka mimi ni hapa tu, sisi tunasema tunapotaka sisi ni hapo tu, tumefika.

Kwahiyo sisi wanaume ambao tulikuwa tunavizia vizia hii nafasi ya Urais hebu twende likizo kwanza. Hii shughuli sio yetu, siku hizi ina wenyewe hii, ndio ukweli na mbaya zaidi huyo mwanamke ambae ndio Rais kazi anayofanya hakuna wanaume ambao wanaweza kuifanya.

Nchi hii imelaaniwa kwa kujipendekeza. Mtu anavuruga kila siku lakini chawa hawathubutu kumkosoa zaidi ya sifa za kinafiki
 
Kwa Rais wangu mpendwa Samia timiza ahadi zako tuko pamoja.
636be486a7034f4c62b6d8f33e071314.jpg
 
Ebu Samia mtest huyu kama ni mkweli; mtumbue halafu baada ya miezi 6 usikie atakuwa anakusema nini!
 
Back
Top Bottom