Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli achukua fomu ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania Ofisi za NEC

Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli achukua fomu ya kuwania nafasi ya Urais wa Tanzania Ofisi za NEC

"Tumechoka Taifa hili unalima pamba unaisafirisha kama malighafi, halafu wakishatengeneza nguo wanazivaa wanakuletea mitumba wakati pamba ni yako. Sisi tunataka tukilima pamba tunaichakata hapa zile nguo tunawapelekea ikiwezekana tunazivaa kwanza." -Rais
@MagufuliJP
Hahah 2015 alisema hivyo hivyo tena,sijui amesahau?
 
"Tumechoka Taifa hili unalima pamba unaisafirisha kama malighafi, halafu wakishatengeneza nguo wanazivaa wanakuletea mitumba wakati pamba ni yako. Sisi tunataka tukilima pamba tunaichakata hapa zile nguo tunawapelekea ikiwezekana tunazivaa kwanza." -Rais
@MagufuliJP
Hii kauli kaiongea tangia mwaka 2016!
 
Hiko kitabu kimejaa miradi bila shaka. Hivyo basi watumishi ambao muliambiwa musubiri miradi ikamilike ndipo mkumbukwe inakwenda kula kwenu.

Vijana mnaosubiri ajira, mjipange na vibarua vya muda mfupi vya kwenye miradi mikubwa ya kimaendeleo.

Ajira rasmi na za kudumu mtazisikia redioni tu.
 
Miaka 5 hii ameshindwa kutengeneza hizo ajira,kutoa ajira zilizo rasmi haijawahi kua kipaumbele chake na wala haitakua na kwny awamu yake vibarua/saidia fundi imekua ndio ajira rasmi sasa kwa maono yake yeye.

Mwambie wanyonge wanamshukuru sana.
Ajira ni janga la dunia kichwa umefugia nywele tu
 
Hana mda na vijembe, vijembe tunamuachia Lisu maana kila akilala na kuamka anamuona magufuli sasa anabaki kuweweseka.
Hawezi taja sentesi bila maguguri, na bado ataiimba saana.

Kama ulivyo wewe kwa Lisu , au wewe ni mdogo wake Musiba ?
 
Kumekucha salama,



Leo tarehe 06.08.2020 mgombea nafasi ya kazi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Kwa Chama cha Mapinduzi, atachukua fomu kwenye ofisi ya NEC makao makuu ya Dodoma.

Baada ya kuchukua fomu ataongea na wananchi pia wanachama wa CCM kwenye ukumbi wa white house jijini Dodoma.

Watanzania wanatakiwa wanaombwa kumsikiliza.

UPDATES:

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Mh. Jaji Rufaa (Mst), Semistocles Kaijage akikabidhi fomu za kugombea kiti cha Rais Kwa Mgombea wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Dkt. John Pombe Magufuli (kushoto)katika Ofisi za Tume, Njedengwa Jijini Dodoma leo Agosti 6,2020. Kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera Charles na Wa pili kulia ni Makamu Mwenyekiti wa NEC, Jaji Rufaa (Mst) Mbarouk Salim Mbarouk.

View attachment 1528677
Mgombea wa Urais, Dkt. Magufuli akiwa na Mgombea Mwenza Mama Samia Suluhu Hassan wakionesha begi lenye fomu ya Urais

Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM:
Ushindi wa mwaka huu ni wa kishindo kikubwa. Tutashinda nafasi za kutosha. Tutashinda nafasi za kutosha za udiwani. Tutaongoza halmashauri zote nchi nzima. Tutakuwa na wingi wa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano.


Rais Magufuli:

Napenda nikiri. Sikutegemea ningekuta watu wengi hivi hapa, kwasababu mimi nikawaida yangu kuheshimu sharia.

Kitabu cha mwaka huu cha ilani ni kikubwa kuliko miaka iliyopita, kina mambo mengi sana. Siwezi nikayasema hapa yote. Tutayasema siku ya uzinduzi wa kampeni.

Na ninawaomba viongozi viongozi wenzangu, kuzindua kampeni hizi ikiwezekana kuzianzia hapa Dodoma, kwakuwa Dodoma ni Makao Makuu ya Nchi.

Nilipomaliza kuchukuwa fomu pale kwenye jengo la NEC pamoja na Mama Samia, Mama mchapa kazi, jabali la kwelikweli, nilipokuwa nateremka kwenye gari nikiwa pale juu nikakiangalia Chuo Kikuu cha Dodoma, nikaangalia chini nyumba na maghorofa yalivyojengwa katika eneo hili la Dodoma, nikajaribu kutupa macho yangu mpaka Chuo cha Mipango kule. Nikaangalia kila mahali. Hujagusa Chuo Kikuu cha St. John, unaenda pale CBE na maeneo mengine. Hombolo sijakisahau jirani yetu kule.

Lakini nilivyoiona Dodoma ilivyo, nilijiuliza nikiwa njiani nikasema: “Dodoma kweli imekuwa hivi? Mbona sikuikuta hivi nilivyoteuliwa kuwa Rais” Nikafurahi kuwa ndoto za Baba wa Taifa zimekamilika kwamba Dodoma ni Makao Makuu ya nchi yetu.

Tulipochaguliwa kuongoza taifa hili kupeperusha bendera ya CCM, tumefanya mengi…kila mahali katika nchi hii, pamefanyika kitu.

Kwa kumbukumbu zangu tu, shule zaidi ya 908 za msingi zimejengwa katika nchi hii. Hizo ni za msingi. Za sekondari ni 228, vituo vya afya karibu 500. Mambo mengi.
Viwanda hajasema ni vingapi vimejengwa? Atasema siku ya uzinduzi wa kampeni.
 
Uzuri ni kwamba Mataga wengi hawana ajira na maisha yao magumu tu. Msione wanasifiasifia tu na wao kibano wanakipata.
 
Sidhani kama anaweza kuwa na guts za kuongea hivyo kama mwenyekiti wake hajazungumz naye, maana watu wanaongea kile kinachomfurahisha mwenyekiti
Ni kweli, ni moja ya njia ya kuondoa hofu na kuvuna kura kutoka kwa wapiga kura (wale wasio wanachama wa vyama vya siasa) na ambao hawataki kuwa na Rais wa maisha.
 
'Nilipomaliza kuchukuwa fomu pale kwenye jengo la NEC pamoja na Mama Samia, Mama mchapa kazi, jabali la kwelikweli, nilipokuwa nateremka kwenye gari nikiwa pale juu nikakiangalia Chuo Kikuu cha Dodoma, nikaangalia chini nyumba na maghorofa yalivyojengwa katika eneo hili la Dodoma, nikajaribu kutupa macho yangu mpaka Chuo cha Mipango kule. Nikaangalia kila mahali. Hujagusa Chuo Kikuu cha St. John, unaenda pale CBE na maeneo mengine. Hombolo sijakisahau jirani yetu kule.'

'Kwa kumbukumbu zangu tu, shule zaidi ya 908 za msingi zimejengwa katika nchi hii. Hizo ni za msingi. Za sekondari ni 228, vituo vya afya karibu 500. Mambo mengi.'

Angalia hapo juu mkuu,Masaa yeye 24 hua anawaza ujenzi tu mambo mengine hua anaona hayamhusu kabisaa.

Kazi ipo.
Ulitaka aseme nimewagawia kila shilingi laki mbili mbili?
 
Speech imepoa kama mate ya mgonjwa, nimejaribu kumsikiliza kiukweli anatia huruma, kwanza hana hata nyomi la kumsindikiza kufata fomu.

Lissu atawaua watu mwaka huu
 
Back
Top Bottom