Uchaguzi 2020 Dkt. Magufuli akiwa Misungwi; Nimebaki mimi tu kwa sababu hamnipendi, hamjanipitisha bila kupingwa

Huyu Baba la Baba kachanganyikiwa.
Juzi jumapili kawafokea watu kwamba wakichagua upinzani watakoma. Hadi kabadilisha lugha ili wamuelewe.
Leo ana sema tusibaguane. Huyu mzee ana ndimi ngapi? Ni mtu wa kumuogopa sana
Laana ya Uonevu inamtafuna, na tutasikia mengi sana yasiyoeleweka kutoka kinywa chake
 
Dr wake afanye consultation haraka sana kwa Neurologist
 
inategemea wewe unamuonaje,pengine wewe ndo hauko sawa.
So, hata kwenye hilo la kuropoka maneno yanayopishana bado nyinyi mashabiki wake mnaona yuko sahihi ? sio kwamba mnamsaidia kwa kumsifia hata anapoyakoroga bali mnamharibu, Nchi yetu imejengeka kwa kuwa na viongozi wenye staha katika kusema, sio huyo wa sasa
 
mweye staha ni nani Lisu au mtei?
 
Nimebaki mimi tu kwa sababu hamnipendi, hamjanipitisha bila kupingwa, wangapi mtanipitisha bila Kupingwa? [emoji848][emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
Mzee choka mbaya....Ubishi tu,vinginevyo angeachia ngazi
 
Nimebaki mimi tu kwa sababu hamnipendi, hamjanipitisha bila kupingwa, wangapi mtanipitisha bila Kupingwa? [emoji848][emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
Mzee amepanic huyu,, hakika 28th October tunamwelekeza Kibra asubuhi na mapema!
 
Tunataka mgombea urais anaehubiri amani Kama Dr John Pombe Magufuli hawa wengine wanaohubiri fujo na chuki hakika kura zetu hawatapata tutawaelekeza watoto wetu mama zetu na baba zetu hakuna kuchagua hao wahuni
Anayelazimisha wananchi wasitumie demokrasia yao kuchagua viongozi wawapendao ni nani?
2.Anaeweka hadharani vitisho kwa wananchi kama watachagua viongozi wa upande wa 2 ni nani?
3.Wakati huohuo anayeendelea kuuutumia ujinga wa kutokuwa na uelewa wa wananchi kwa kusema 'Maendeleo hayana vyama ni nani?' Natamani sn hofu ya Mungu ingewatawala wanaotuomba kura kwa mustakabali wa jamani ya nchi yetu.
Eti mkuuu umejifanya kauzu huelewi, muheshimu aliekuweka hai.
 
Mzee wa utopolo katika viwango vyake.
 
Nimebaki mimi tu kwa sababu hamnipendi, hamjanipitisha bila kupingwa, wangapi mtanipitisha bila Kupingwa? [emoji848][emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
Maneno ya mlevi na kichaa
 
Replica, Magufuli anajua pa kuanzia kampeni zake mfano katika miradi mikubwa aliyotekeleza na maendeleo kwa ujumla Sasa sijui wenzetu huwa wanaanzia wapi manake hawana reference.

Kwa heshima na taadhima tunakuomba urudi shule ukasome somo la uraia mpaka utakapotoa ujinga katika ubongo wako, serikali yako imejenga shule za kata usisite kurudi ukasome.

Wapinzani wawe na reference kwani wao ndio walikuwa wameshika nchi? Ni wao ndio walikuwa na serikali? Ni wao ndio walikuwa wanakusanya kodi? Mpaka lini tuwaeleweshe vitu vidogo vidogo kama hivi nyie wanyonge?
 
Nina uhakika usiku wa kuamkia leo, huko Mwanza walifanya kikao cha faragha cha kumkanya aache kauli zake za "sagala sagala"

Hakuna kikao cha ndani kinaweza kukaa kumuonya huyu mtu, amini nakwambia. Kinachomfanya leo ameact kama mtu ni umati wa watu waliokuwa kirumba, majuzi alikuwa amepanikishwa na watu waliokuwa kwa TL kwa ukanda wote ule wa ziwa. Hakuamini na hakujua kama viongozi wa CCM wangeweza kumkusanyia na yeye umati wa kutambia, ni kweli viongozi wamehenyaka kumkusanyia watu ikiwemo wanafunzi wa shule. Kukusanyika kwa watu kirumba kumemfanya ashushe pressure na kupunguza kufokea wananchi na kuwatisha. Magu anapanikishwa na vitu vidogo sana na anakuwa impressed na vitu vidogo vilevile kama kumsifia. Sijui ni lini waTZ wataelewa exactly tabia za huyu mtu, ni wa hovyo sana.

Kuwa na Rais anayepanikishwa na vitu vidogo kama “umati wa watu” ni jambo la hatari sana.
 
Kuna vitu sivielewi.

Tupendane... tusibaguane kwa misingi ya vyama, kabila, dini.

Maendeleo hayana vyama.

Msiponichagulia watu wa chama changu siwapi maendeleo.

Siwezi kuwaacha watoto wangu na njaa nikawapa chakula watoto wa jirani!
 

Wewe unaona mashabiki zake wako sawa? Hao ni wale wale hawana usawa wowote. Juzi nilisema humu anayemshabikia magufuli ana tabia kama zake.

Kwa kuongozwa na sheria za asili, binadamu ni kawaida yetu kushabikia vitu vizuri na kushabikia mtu mwenye tabia nzuri, hii ya kushabikia mtu Muongo, katili, mwenye jazba, asiyependa kupingwa, mropokaji, mdhalilishaji wa wanawake, fisadi, mbaguzi, mkurupukaji, mpenda kusifiwa hata kama sifa za uongo, mnafiki. Lazima tujiulize mara mbili mbili juu ya hawa wanaomshabikia huyu mtu mwenye mambo ya hovyo namna hii.
 
Hakuna Mtanzania mwenye Akili timamu atawapigia kura CCM
Kwa hiyo tuipigie kura Chadema ambayo imeshindwa hata kujenga ofisi ya makao makuu ya chama licha ya kupata ruzuku ya zaidi ya bilioni tatu kila mwaka? wewe ndiyo akili yako haiko timamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…