Dkt. Mpango ni kweli ulishiriki kumtuma Sabaya kufanya mambo machafu?

Dkt. Mpango ni kweli ulishiriki kumtuma Sabaya kufanya mambo machafu?

Afungwe kivipi wakati hakuna ushahidi wa kutosha kumfunga!? Labda Mpango aje Mahakamani aseme hawajawai kumtuma Sabaya kufanya kazi maalumu ya kuwasaka wahujumu Uchumi!!
Aliyemtuma ni JPM (mamlaka ya uteuzi), sio Mpango. Mpango alijua tu.

Swali kubwa: alitumwa kama undercover agent (mtu asiyejulikana) au kama DC? Mbona alikuwa akijinasibu sana kwenye misheni hizo? Hakuwa professional kabisa.

Ajiandae kurukwa na kuangushiwa jumba bovu na hao “wanaojua”. Aliyemtuma ndio hivyo tena. The dead tell no tales. Ni kawaida katika nchi zetu hizi wakubwa kutafuta watu wenye viherehere na kuwapa kazi chafu halafu kuwasakizia mbwa wasipohitajika tena ili wasije wakawa-contaminate. He is expendable.

Sabaya angekuwa smart angejua ile kufutiwa kesi ya kujifanya TISS na kupewa ukuu wa wilaya halafu kuanza kutumwatumwa ovyo tayari wajanja walishamfanya kifaa cha kufanyia kazi chafu. Angeenenda kwa tahadhari sana. Halafu anajua kazi yenyewe alirithishwa na nani. Mwenzake saa hizi anajifanya kama hakuwa yeye ingawa amechafuka kupita maelezo.
 
Watanzania wagumu kweli kuelewa. Kuna upotoshaji mkubwa sana unaendelea. Sabaya amesema alienda Arusha kwa maagizo ya mamlaka iliyomteua.

Prof. Lunga (Gavana) na Dr. Mpango (aliyekuwa Waziri wa fedha) wametajwa kama watu wanaojua moja ya kazi maalum aliyowahi kuifanya huko Dar es Salaam baada ya kukamata machine ya kutengezea fedha bandia.

Na amesema hivyo ili kuonesha kuwa kuna kazi nyingi tu aliwahi kuzifanya nje ya eneo lake la kawaida la kazi. Hiyo ya kwenda Arusha haikuwa ya kwanza.

Pamoja na hayo, amekanusha kuiba fedha wala kutumia silaha. Kila alichokuwa anakifanya alipata ushirikiano wa vyombo vya dola. Hata aliyekuwa mkuu wa wilaya wa eneo husika alikuwa na taarifa juu ya uwepo wao.

Kwa maneno mengine alikuwa kwenye kazi maalum aliyotumwa na mamlaka ya uteuzi wake: siyo Dr. Mpango, Prof. Luoga au hao wengine aliowataja.
Jambazi ameamua kuweka wazi kuwa huu ujambazi aliofanya Arusha alikua anashirikiana na Magufuli na Mpango full stop.
 
Hiyu ana akili za kitoto sana.kesi hii sidhani kama ni ya kunyongwa.sasa anapowataja wakuu wa nchi ni dhahiri hakuwa jasusi .Kama kweli alitumwa sidhani kama alitumwa kufanya uhalifu.Amejiharibia kupita kawaida
 
hakuna kesi hapo.
kama alikuwa anatekeleza majukumu yake aliyo elekezwa na aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu ktk kuhakikisha kodi ya Serikali inalipwa. sasa huo unawezaje kuuita eti ni unyang'anyi?!!
ukiangalia hii kesi kwa jicho la tatu imejaa kisasi dhidi ya sabaya kutokana na majukumu yake aliyo kuwa akiyatekeleza, kwa vyovyote vile lazima angechukiwa sana na either;
1. wafanyabiashara au wanasiasa au wote kwa pamoja. ndicho kilicho tokea.
Amiri jeshi mkuu Ana vyombo rasmi vya kutekeleza jukumu hilo. Kuna vilivyo juu ya meza (overt) na viliyo chini ya meza (covert) na vyote vina wateule wake.

Jiulize, alimpaje kazi hiyo DC Sabaya mtu mwenye weledi haba na kelele nyingi za kujinasibu? Kwa kifupi ni game over kwake.
 
Inawezekana lugha aliyoitumia mtoa comment ni kubwa sana kwako. Kujitokeza ajisafishe ni lugha ya heshima ya kumwambia mtu ajitokeze kukana au kukubali hizo tuhuma. Akikana tuhuma ndiko kujisafisha kwenyewe, na akikubali tuhuma, ndipo hoja ya kuwajibika/kukaa pembeni inapoanza kujadiliwa.
Mleta uzi amezungumzia kuwa kama ni kweli Mpango amefanya madudu haya ajitokeze na ajisafishe ila wewe unasema kuwa kama ni kweli Mpango amefanya madudu haya ajitokeze awajibike.Huoni kuwa hizi ni sentensi mbili tofauti ambazo zimebeba jumbe mbili tofauti?(Hapa tunazungumzia upande mmoja wa Mpango kukubali tuhama pekee)
 
Mleta uzi amezungumzia kuwa kama ni kweli Mpango amefanya madudu haya ajitokeze na ajisafishe ila wewe unasema kuwa kama ni kweli Mpango amefanya madudu haya ajitokeze awajibike.Huoni kuwa hizi ni sentensi mbili tofauti ambazo zimebeba jumbe mbili tofauti?(Hapa tunazungumzia upande mmoja wa Mpango kukubali tuhama pekee)
Uko sahihi. Mada inataka kujua kama Dr pango alijua au hata kushiriki, na kama alishiriki basi ameharivu CV yake. Kama hakushirikia ajitokese akanushe. Ili kulinda heshima yake tunayompa sisi tunaompenda
 
Wanahusishwa kwasababu wanajua, sasa ili mambi yawe safi wayatolee ufafanuzi haya.
Ni rahisi tu Wajitokeze wasema aliyofanya Sabaya wao hawakufahamu kwa namna yoyote. Hata kama hawakumtuma ila kama walifahamu kinachoendelea kikaendelea maana yake walikibariki.
 
Inawezekana lugha aliyoitumia mtoa comment ni kubwa sana kwako. Kujitokeza ajisafishe ni lugha ya heshima ya kumwambia mtu ajitokeze kukana au kukubali hizo tuhuma. Akikana tuhuma ndiko kujisafisha kwenyewe, na akikubali tuhuma, ndipo hoja ya kuwajibika/kukaa pembeni inapoanza kujadiliwa.
Swadakta kabisa. Hii ndio lengo la uzi huu.
 
Watanzania wagumu kweli kuelewa. Kuna upotoshaji mkubwa sana unaendelea. Sabaya amesema alienda Arusha kwa maagizo ya mamlaka iliyomteua.

Prof. Lunga (Gavana) na Dr. Mpango (aliyekuwa Waziri wa fedha) wametajwa kama watu wanaojua moja ya kazi maalum aliyowahi kuifanya huko Dar es Salaam baada ya kukamata machine ya kutengezea fedha bandia.

Na amesema hivyo ili kuonesha kuwa kuna kazi nyingi tu aliwahi kuzifanya nje ya eneo lake la kawaida la kazi. Hiyo ya kwenda Arusha haikuwa ya kwanza.

Pamoja na hayo, amekanusha kuiba fedha wala kutumia silaha. Kila alichokuwa anakifanya alipata ushirikiano wa vyombo vya dola. Hata aliyekuwa mkuu wa wilaya wa eneo husika alikuwa na taarifa juu ya uwepo wao.

Kwa maneno mengine alikuwa kwenye kazi maalum aliyotumwa na mamlaka ya uteuzi wake: siyo Dr. Mpango, Prof. Luoga au hao wengine aliowataja.
umekubali na umepinga nini? Ugumu wa kuelewa uko wapi? inaonekana wewe ndiye mgumu wa kuelewa
 
Kosa la Dr. Mpango ni lipi? Naomba muwe mnasoma na kuelewa hoja kabla ya kujiandikia tu. Kutumwa Sabaya kuongoza operation ya kukamata mitambo ya kutengenezea fedha haramu ni kosa? Kwa hiyo mlitaka nchi iachwe watu watengeneze fedha vile wanataka? Hiyo si jinai kama jinai zingine? Sabaya ameshitakiwa kwa kosa la kushiriki ama kufanikisha ukamataji wa mitambo hiyo, tukio ambalo anasema Waziri Mpango na Governor wa BoT walijua? Assignment halali kama hiyo, inakosa gani hadi muwatuhumu Waziri na Governor wa Bank kwa kujua kwao?

Anaposema alitumwa kukamata Mitambo hiyo ambapo hata Governor wa BoT na Waziri wa Fedha wa wakati huo walijua, anakuwa anatoa utetezi wa shitaka lipi hapo huyo Sabaya?
AMEDANGANYWA. Kuacha kujibu mashtaka yanayomkabili na kuanza kuwa implicate viongozi kwa amri halali ambazo walimwagiza afanye na ambazo hazihusiani na mashtaka yake ni hallucination ambayo ni public entertainment tu. Mwambieni ajibu tuhuma alizoshitakiwa nazo. Kama ni kubaka, kunyang'anya fedha, n.k ajitetee vinginevyo anaoga mvua za kkutosha tu.
Sasa ametajwa vipi huko mahakamani? kumbuka ile ni kesi ya Uhalifu. Kiongozi wa umma kutajwa tu maana yake kuna association ya namna fulani. Hili ni doa.
 
Hizi operation zinahitaj watu wenye uvumilivu...sabaya mwez mmoja jela kashaanza kutaja? Akibinywa mbupu si fasta tu anatoa siri zote
 
Wanaonisononesha zaidi ni hawa viongozi wetu wa kidini ambao pamoja na ushetwani na unyama wa Magufuli na serekali yote aliyomrithisha Samia bado wanaendelea bila aibu kuwa nayo bega kwa bega na kuipamba.

Siku ya kiama Mungu aje kuanza na hawa viongozi wa kidini Tanzania wakawe kuni kwenye lile tanuru la moto wa milele!
Hakuna viongozi wa dini. Hapo kuna wafanyankazi wanaotafutia tumbo kama ilivyo kwa Mwalimu, Daktari, Polisi, Mwanajeshi, Mkulima na mjasiriamali. You should not expect anything than that.
 
Kukamata mitambo ya kutengenezea fedha haramu ni kosa? Msiingie mtego wa Sabaya. Anashindwa kutetea uharibu alioshitakiwa nao kama kubaka, kuteka, na kunyang'anya fedha, makosa ambayo alijifanyia mwenyewe kwa sababu ana hulka za kinyoli. Anababaisha kwa ku site matukio halali ambayo mfumo ulimutuma afanye kwa maslahi ya taifa.

Sabaya ni mjinga. Kukwepa kujibu matukio anayoshitakiwa nayo, kwa kujigundisha kwenye kazi halali, kisheria hakumwondolei wala kuhalalisha personal offences zake. Ni afadhali angejikita kua dress mashitaka yanayomkabiri. Ana implicate serikali na viongozi wake kama kuwadhalilisha ama tufe wengi ama kuwakomoa kwa kuwa hawajamtetea, bila kutambua kwamba ukiwa katika kazi, ukafanya makosa yako binafsi kama kubaka, ama kunyang'anya, matukio ambayo hayahusiani na kazi uliyotumwa, sheria inakuondolea kinga ya kio-office. Huo ni uharifu binafsi. Aki turn hostile, ama aamue kuwahusisha watu wengine, wakiitwa mahakamani watamwuliza, anashtakiwa kwa kosa lipi? Kubaka, kunyang'nya fedha n.k. Je ndiyo kazi walikuwa wamemtuma?
Hakuna mtu asiyejua serikali inaweze kumtumia mtu yeyeote kufanya kazi za serikali kulingana na uwezo wake au mazingira yake ya kufanikisha kazi hiyo kama alivyotumwa na hao WAheshimiwa kukamata mashine ya kufulia fedha, kitu ambacho wala hakiko katika mashitaka.

SIDHANI KAMA MWANASHERIA WAKE NDIYE KAMSHAURI UTETEZI HUO.
Huenda wanasheria wake uchwara wameona ndio namna ya kuchomoka. Lakini pia inaonekana ameanza kutapa tapa. Anaona waliomtuma wamemtelekeza.
 
Ktk mpira sabaya akifungwa inakuwa ni mbinu ya kutafuta kumpiga miaka mbowe.. Tunaita equalisation la sivyo kuna upande utajipanga kwa maangamizi makali zaidi na bibi atajuta in the end
Asante kwa kuliona hilo. Hapo wanataka kutuaminisha kuwa mahakama na polisi wanacheza fair.

Hili la Mbowe litawatoka puani. Tujipe muda
 
Back
Top Bottom