Dkt. Mwigullu Nchemba: Hatuwezi kumuacha mtu awe tajiri kwa kukusanya pesa za Watanzania

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Your browser is not able to display this video.

Waziri wa fedha Mhe.Dkt. Mwigulu Nchemaba leo mei 22,2024 Bungeni Jijini Dodoma amesimama kujibu hoja za wabunge waliochangia bajeti ya makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha 2024/2025 ya Wizara ya Viwanda na Biashara

Katika majibu yake Dkt. Mwigulu amesema kuwa mtu yoyote anayekusanya fedha ya Serikali ni lazima aifikishe sehemu husika

Dkt. Mwigulu amesema haiwezekani kumuachia mtu anayekusanya fedha za watanzania halafu akawa tajiri huku akina mama wajawazito na wanafunzi wanakosa huduma kwa sababu yake
 
Leo nimekuelewa sana ndg yangu Mwiguli
 
mod fungal hii post yajayoo yanahuzunishaaa watanzania hasana stamina
 
Tena amesema Samia anawafanyia fair like ingekuwa mwingine au yeye hakuna rangi wangeacha kuiona.

Alikuwa anaizungumzia ule utaratibu wa eti mfanyabiashara akipitiliza miaka 3 aachwe,hiyo haipo
 
Dr Kigwangalla: Ukiwa Juu epuka sana Jeuri Kiburi na Majivuno kwani kuna kupanda na kuanguka

πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Juu ya nini? Hapo Kuna jeuri na majivuno yapi? Shenzi kabisa wewe Watumishi wenye vimishahara vidogo wanalipa kodi na hawana room ya kukwepa afu unasemaje?

Ndio maana Huwa nawashangaa watu wasiodai risiti yaani nilipe Kodi nikufaidishe wewe kirahisi tuu?
 
Hadi alalamike hivi, maana yake ni kwamba watu hao wanaoachiwa wapo sana,; na hakuna lolote lililofanywa dhidi yao.
Huyu ni waziri tu, leo atatoa 'sound byte' yake Bungeni na kuishia hapo
Huko juu kunakoruhusu baadhi ya watu wafanye hivyo ndiko kwenye matatizo.

Hizi "kamba za ulaji" haziishii kwa watumishi serikalini, huko kwenye sekta binafsi ndiko zipo imara zaidi.
 
Kuna wakati unaeleweka vizuri, kama ulivyoonyesha hapa. Sasa sielewi matatizo yako huwa yanatokana na kitu gani mara nyingi!
 
Aanze na raisi ,Makamu na wabunge nk wasiokatwa kodi kwenye Mapato Yao walipe kodi stahiki hao ndio wakwepa Kodi Namba moja akiwemo yeye akamatwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…