Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Dr. Wa ukweli usife moyo kwani penye mafanikio hapakosi changamoto kama hizi na mwisho wake mafanikio yatakuwepo mfano mzuri ni NELSON MANDELA wakati akipigania uhuru wa south afrika

mandela hakuwa muongo na mzushi kama dokta ni makosa makubwa dokta kumfananisha na mandela.
 
Ili nimuone Dr anaakili timamu
1. Athibitishe hiyo namba ya gari sisi tuko tayari kufuatilia na kutaja gari ni ya nani.
2. Abandike hiyo picha ya gari iliyo pigwa. Na kama picha imechakachuliwa tutaielewa ninazo tools.

La sivyo huyu mzee atakuwa anazeeka vibaya.
 
samahani Dr.W.Slaa tunaomba utuwekee hiyo picha mlio piga tuione. tunaweza kulitambua. mia
 
Last edited by a moderator:

kwa TISS ya sasa kwa jinsi wasivyo na akili haya yanawezekana. kwani dr ulimboka ilikuwaje?
 
Mkuu hawa jamaa wanatafuta attention kwa gharama zote sasa,
Usishangae kesho ukisikia mbunge wa chadema anatoa show ya bolingo kariakoo ili aandikwe magazetini.
Haya mambo ya magari kukufuata au kuongozana nayo katika safari ni jambo la kawaida , wakati mwingine hutokea tu kwani wengine wakiwa kwenye safari ndefu hupenda kuongozana na magari mengine ili wasichoke na pia kuwa na back up kama wakipatwa na lolote barabarani, mimi pia huwa napenda kufuata gari ambalo naliona linaenda safari ndefu kama yangu kama kampani.
Na pia ni kawaida kwa binadamu kuhisi anafuatwa hasa pale anapokuwa mtu maarufu kama Dr.
Mbona mimi nilipotoka kwa Dr kuna magari mawili yalinifuata sana mpaka nikaamua kusimama na kuwapiga mkwara wakasepa? Dr si ana walinzi? kwa nini mlinzi asifyatue moja ya juu ili jamaa wasepe? Unajuje kama hao sio vibaka waliokuwa wanataka kuwapora hela walizochangisha kwenye mikutano?
 
Mkuu si unajua usiposikika ndio unakuwa umekwisha kisiasa ?
Inabidi ufanye lolote lakini sio kama anavyofanya lema ili uonekane upo, hiyo ndio siasa ya chadema
 
Mkuu si unajua usiposikika ndio unakuwa umekwisha kisiasa ?
Inabidi ufanye lolote lakini sio kama anavyofanya lema ili uonekane upo, hiyo ndio siasa ya chadema
Hawa jamaa wanadhani wanaogea na watu ambao hamnazo.
Hivi kweli wewe inakujia akilini. Mzee mzima unakua muongo.
Na Mzee Slaa anatoa maelezo ya kitoto kabisa. Hivi anatuona sisi kama nini huyu mzee?
Asipo thibitisha basi huyu mzee kila kitu atakacho ongea nitajua tu akili zake zimeanza kuliwa nauzee
 
Wanasema hilo gari limewafuata kwa muda mrefu sana na waliweza kulitambua kila wakikutana nalo.
Hata kama hawajalipiga picha basi watupatie usajili wa hilo gari/ namba zake
Kama hawana mimi naweza kuwapatia namba ya gari la polisi moja
STG 8915 TOYOTA LANDCRUISER
Kama hiyo haitoshi naweza kuwapatia nyingine nyingi tu ninazikumbuka nilipokuwa polisi au kuna lile la usalama wa taifa namba T500 SER nalo ni li landcruiser ila sijui kama rangi zinafanana
 
Hao ni CCMTISS. Kudos Jack Zoka and Ramadhani Ighondu, the nation is watching everything you do...

Waliomfuatilia wanajulikana na sababu zinajulikana. Amezaa na mke wa mtu mkuu, kwa hiyo ni lazima ashughulikiwe. Sio kila kitu eti TISS wakati mitaani mnabeba wake za watu.
 
Tunaomba na ufafanuzi kama huu kwenye suala la kutaka kumuua zitto
 
hivi ni mimi pekeyangu ninayehisi kuwa tangu Video ya Lwakatare itolewe, CHADEMA wamekuwa wakihangaika namna ya kuifunika na kuonesha kuwa mbaya ni serikali na vyombo vyake vya dola?? mana tangu kutoka kwa video ile, tuhuma dhidi ya serikali na vyombo vyake vimezidi maradufu, haya, lilipokuja bunge ndo kabisa, wakaweka tuhuma zao hadi kwenye hotuba ambazo zilistahili kulenga kuikosoa serikali katika kushindwa ama kuchelewa kuleta maendeleo ya nchi..badala yake zikaongelea tuhuma dhidi ya usalama, na kupigwa ama kutishiwa kuuwa kwa viongozi wa CDM?? hivi ni mimi pekee ninayeona kuwa hadi leo CDM imeshindwa kutoa neno ama skendo inayoweza fumba macho na ufahamu wa vijana wachache wa kitanzania ambao bado tuna uwezo wa kufikiri na kuamua tofauti na wale vijana waliokuwa brainwashed na kuamini kila neno linalotoka midomoni mwa viongozi wa CDM na kuwa tayari kutetea maneno hayo hata kwa uhai wao bila ya kufahamu ukweli wake??
Dr. W slaa, najua juzi tu CDM imetangaza kuwa wewe ndiye mgombea wa Urais 2015, hivi ukishinda, utahudhuria sherehe yoyote ya kitaifa?? hivi utafuta vyombo vyote vya ulinzi na usalama na kuweka watu wako?? hivi utafanya kazi na nani ambaye bado hujamtukana?? au hao vijana wako wanaovaa makoti makubwa meusi na miwani meusi ndiyo watakuwa wanausalama wako?? kwa akili yako, do u think its that simple?? au nawewe umekuwa brainwashed na wazungu??
 
Pre empting approach in solving difficult problems. Watuambie detailde information kuhusu kumvamia mama yake zitto..nyie ni wa maana wengine takataka
 
...Attention mbona mnatupa bure tu wenyewe? mfano MULONGO wenu wa Arusha ameieneza CDM kwa kasi sana siku mbili hizi hadi raha. Na kanda zitatengenezwa 3000 kuwaonyesha watanzania waamue nani ana hatia kati ya RC na Lema. Unajua pamoja na ubaya wenu Mungu ameamua kuwatumia ninyininyi kuwazindua watanzania.
 

Mkuu Zemarcopolo post yako ina thibitisha ya kuwa kuitetea CCM na Serikali yake lazima uwe tahira; Watu wenye uwezo finyu wa kufikiria kama wewe na shindwa ni waweke katika kundi gani. Mwanzoni mmeanza kumshambulia mleta mada kwa madai ya kuwa hizo ni porojo kwa sababu yeye siye verified user, imefikia mahali ambapo Moderator ameamua kuufunga huu mjadala kwa madai ya kuwa ni lazima tupate mtu mwenye credibility kutoka kwenye uongozi wa chama cha Ukombozi aweze kuthibitisha hayo madai. Dr. Slaa amejitokea na kueleza wazi bila kupepesa macho, kama kawaida yenu misukule mmegeuka tena na kuibuka na hoja ya kipuuzi ya kudai picha ya ghari; Je tuwaeleweje ?

Kwa taarifa yenu Tunampenda sana, tunamthamini, tunamheshimu, tunamwamini na tunamwombea Dr.Slaa usiku na mchana ili mwenyezi Mungu amuepushe na hila zenu chafu zilizo ghubikwa na ufedhuli.
 

Mkuu si kila police ni saidi mwema au kila TISS ni igondu. Mendine wanakerwa na uovu wa mabosi wao lakini hawana la kufanya kwakua wakubwa wameshika mpini ila wakipata nafasi wanadhibiti uovu ulioko ngazi za juu
 
Sijui nilikua naota au ni kweli, nakumbuka (kama nilikua naota sijui) Mzee Wassira alisema Bungeni kua Usalama wa Taifa hawawezi kumtesa Absalom Kibanda kwasababu sio kitisho kwa serikali labda Dr. Slaa au Mbowe, kama ni ndoto labda ndio inataka kutimia (kumbe ndoto zingine hua kweli) kama haikua ndoto may be we have to start connecting the dots here.
 

Too Low!
 
hivi una akili timamu kweli?Namba ya gari si imewekwa hapo juu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…