Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Nasikitika ujinga kama huu kuandikwa kwenye mtandao wa kijamii unao ongoza hapa Tanzania! Propaganda za kijinga kama hizi zina shusha hadhi ya JF
 
Naona kwa sababu Dk Slaa aliwachana sana TISS Pamoja na ikulu kwa ujumla, pale kwenye mkutano mkubwa wa hadhara Mbeya.
Mkuu, TISS na vyombo vya dola hawafanyi michezo ya kitoto hivyo. Wamfuatilie kwa malengo gani. Kama lengo ni kutaka kumdhuru, iweje wasitekeleze mpango huo kwenye zile anga za kutoka iringa hadi morogoro kwenye milima ya uluguru na kule kitonga. Acheni propaganda za kipumbavu.
 
Nasikitika ujinga kama huu kuandikwa kwenye mtandao wa kijamii unao ongoza hapa Tanzania! Propaganda za kijinga kama hizi zina shusha hadhi ya JF
Mkuu, kitendo cha uzi kama huu kuwekwa hapa ni dhahiri kuwa kuna malengo maalum. Si unajua hawa jamaa walivyokamatika sasa.
 
Karibu sana mkuu. Ila siku nyingine ukitumwa kuandika propaganda waambie wawe makini na wanachukutuma. Hiyo namba uliyoandika ni namba ya gari la chadema ambayo hutumika maalum wakatiwa misafara ya viongozi wa chama hicho. Ni namba ambayo hubadilishwa pindi safari ikifika. Aghalabu hutumika kwa nadara sana hasa pale ambapo kunajengeka hisia kuwa viongozi wapo hatarini
Atongwele,

tafadhali usilete upotoshaji hapa.Hapa tunaongelea uhai wa watu.Utani huu haustahili sehemu hii peleka sehemu husika
 
Last edited by a moderator:
Karibu sana mkuu. Ila siku nyingine ukitumwa kuandika propaganda waambie wawe makini na wanachukutuma. Hiyo namba uliyoandika ni namba ya gari la chadema ambayo hutumika maalum wakatiwa misafara ya viongozi wa chama hicho. Ni namba ambayo hubadilishwa pindi safari ikifika. Aghalabu hutumika kwa nadara sana hasa pale ambapo kunajengeka hisia kuwa viongozi wapo hatarini
Ndiyo gari hilo hilo waliloamuwa kulipiga picha?
 
Bavicha akili zao vituko sana. Hivi habari sensitive kama hii ni ya kuletwa na ID ambayo siyo verifies kweli?

Kesho utasikia kiongozi mmoja wa chadema anasema hiyo namba ya gari lililotajwa lilikuwa lake na kwamba habari imelengwa kumchafua.

Wewe mleta mada kwa vile unajua mambo tokea Iringa mpaka Dar es Salaam maana yake ulikuwa na Dr. Slaa sasa kwanini usichukue responsibility ya kusema kilichotokea?

Kinachochekesha zaidi vijana wa bavisha hapa washaingia line tayari. Yaani mlaghaika kilaiiiiiiiiini...

Verified ID?Ni mambo mangapi yameletwa hapa kwa ID hizi hizi kuanzia EPA hadi RICHMOND na kuwa chanzo kikuu cha habari.Masharti na kanuni za JF zimezingatiwa.Tafadhali usituondoe kwenye mijadala
 
Mkuu, kitendo cha uzi kama huu kuwekwa hapa ni dhahiri kuwa kuna malengo maalum. Si unajua hawa jamaa walivyokamatika sasa.

Great Minds discuss Ideas,medium minds discuss events,small minds discuss people!
 
Funny how people who just joined the forum (Jan - April 2013) seems to have similar arguments. Scripted ..??
Why on earth this is said to be spinning..?? Ask Mwakyembe what happened to him that year, or even ask that police constable who saw the accident and the vehicle involved, and why he was transferred immediately. Yeah, it is Nyombi, now in DCI's office.
C'mon u a...s h...les

You seem to be too desperate for power!!

Uongozi mwanana wa kuongoza jamii unakuja automatically kwa mapenzi ya waongozwa. Mwl. Nyerere alisema kiongozi mzuri ni yule asiyetaka kuongoza. Ninyi kwa sasa inavyoonekana mnataka kuongoza kwa hali na mali.

Hizi spinning mnazozianzisha zitakuja kuwarudieni ninyi wenyewe. Historia ya chaguzi nyingi za nchi za Afrika imebainisha hili. You're setting the spinning bar very high kiasi kwamba hata mkiingia madarakani hamuwezi kuwapa wananchi kile mnacho spin kucha kutwa kama kinawezekana. otherwise, tunaanza kuona kama mko na mission za kutaka kujinufaisha kibinafsi
 
Mkuu, TISS na vyombo vya dola hawafanyi michezo ya kitoto hivyo. Wamfuatilie kwa malengo gani. Kama lengo ni kutaka kumdhuru, iweje wasitekeleze mpango huo kwenye zile anga za kutoka iringa hadi morogoro kwenye milima ya uluguru na kule kitonga. Acheni propaganda za kipumbavu.
TISS kufuatilia watu ni michezo ya kitoto?

Unafahamu maana ya intimidation?

Unauliza afauatiliwe kwa malengo gani,halafu hapo hapo unasema eti "kama lengo ni kumdhuru iweje wasitekeleze kwenye milima ya Kitonga",kama hufahamu lengo lao,haina maana kuwa hawakumfuatilia...
 
Verified ID?Ni mambo mangapi yameletwa hapa kwa ID hizi hizi kuanzia EPA hadi RICHMOND na kuwa chanzo kikuu cha habari.Masharti na kanuni za JF zimezingatiwa.Tafadhali usituondoe kwenye mijadala

Kuondolewa kwenye mjadala maana yake nini?

Dr. Slaa anapenda sana kujibu habari za udaku hapa JF. Kwanini asije kuthibitisha hii habari in person?

Story za kutekwa siku hizi zimekuwa deal la kupata umaarufu!!!
 
Hapo watu walikuwa wanasubiri simu ya kupewa go ahead baaasi mambo yamalizwe du mwaka huu tutang'olewa kucha mpaka ukombozi utapokuja tutakuwa tumekwisha...any way hata musa hakufika nchi ya ahadi.....
 
CDM mnafanya mambo ya hatari na kujiweka hatarini na kuwaweka viongozi hatarini. Mmegundua kuwa kuna gari linawafuata halafu mnafanya nini?

a. Mnategeana na gari (mnalipita linawapita) wenyewe mnasema "Walichukulia kama vile ni mchezo wa kawaida hadi walipofika Morogoro na kushtuka zaidi na kuanza kuchukua tahadhari kwa kunakili namba ya gari hilo" Really? Mchezo wa kawaida barabarani? grrrrrrrrr!!!!!!

b. Mnachukua namba ya gari ambalo limekuja nyuma yenu (kwanza gari hadi linaingia nyuma ya gari ya Katibu Mkuu ni kashfa ndan yake..)!

c. Mkaenda na hilo gari halafu "Walipofika kibaha ilibidi watoe taarifa kwa askari wa usalama barabarani."

Yaani, mna usahaulifu hivyo? Hawa hawa Polisi waliomkamata Mbunge Lema jana usiku; hawa hawa waliowapiga virugungu, hawa hawa... mnawapelekea haya haya mkitumaini kuwa wataikamata ile gari? Halafu wakikuta ni watumishi wenzao wa serikali (TISS au secret branch) mnatarajia watawafanya nini?


Ndugu zangu, mnatutisha... Yaani, mikakati yenu yote ya counter-intelligence mlichofanya ni hicho? haya bana...
 
Hiyo gari naifahamu, ni ya manyigu. Ila inawezekana haikuwa na nia mbaya. Inawezekana ilikuwa na assignment ya kuhakikisha dr slaa anafika safari yake salama. Nadhani ingekuwa jambo la busara kufanya uchunguzi kujua nia ilikuwa ni nini kabla ya ku judge.
 
Pole sana Kiongozi wangu (Dr.Slaa) pamoja na Maofisa wa chama mliokuwa nao ktk safari hiyo.Ni wazi na ni Dhahiri kuwa Serikali Dhaifu na Dhalimu ya CCM imeshakabwa pabaya na viongozi wote wa CCM wameshakabwa koo hawapumui badala yake kila kukicha TISS imebaki kuwa chombo maalumu cha kupanga mikakati maalumu kwa watu maalumu kwa kuagizwa na Watu maalumu(Magambazi).Nawaasa tu Magamba kwa kushirikiana na maofisa wake qakubali yaishe kwani wao ndo walijisahau na kuwageuza wananchi kuwa shamba la bibi kwa kushindwa kutekeleza Ilana na ahadi za ccm badala ya kuulizana wenyewe ni wapi wameshindwa sasa wanafikiri njia sahihi ni kudhuru viongozi na wanaharakati wa CDM.Dola wajue kuwa wanachokifanya wakilenga kuihujumu CDM ni sawa na mtu anayezuia Mafuriko kwa kutumia matope au Nyavu.Vile vile ni sawa anayezipa shimo la panya kwa kutumia mkate akiamini panya atashindwa kuingia.Watanzania wenzangu pamoja na Vikwazo hivi hakika TUTASHINDA.CDM KUKUBARIKA KWA WANANCHI NI MPANGO WA MUNGU NA MABADILIKO TUNAYOYATALAJIA NI MPANGO WA MUNGU WA MUNGU HAKUNA WA KUZUIA MPANGO WA MUNGU HATA ATUMIE RISASI WALA MABAVU.MUNGU IBARIKI CDM NA WATANZANIA WANAOSUBIRIA MABADILIKO.''VOTE FOR T2015CDM'' AMEN. COPY KWA Sumu,Wingu,Bungeni,My web na ZeMarcopolo.
 
Hawa ndio wanataka wapewe nchi!!!

Nchi sio kichwa cha mwendawazimu...
 
WANABODI,

Usalama wa viongozi wa chama kikuu cha upinzani Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) upo hatarini.Akiwa njia ni kutokea Iringa, Dr. Slaa amefuatiliwa na Gari aina ya Landcruiser yenye vioo vya giza (Tinted) lenye namba za usajili T963 ABN. Awali waliokua ndani ya gari la Dr. Slaa hawakushtuka sana japo waliona kuna mchezo wa gari hilo kuwapita kwa kasi na kisha kupunguza mwendo ghafla na kisha gari la Dr. Slaa kuwapita tena.Walichukulia kama vile ni mchezo wa kawaida hadi walipofika Morogoro na kushtuka zaidi na kuanza kuchukua tahadhari kwa kunakili namba ya gari hilo


Walipofika kibaha ilibidi watoe taarifa kwa askari wa usalama barabarani.

Dr. Slaa na maofisa wa chama akiwemo afisa habari walishtuka zaidi walipofika njia panda ya Tamko-Bunju ambayo mara nyingi hutumika kunapokua na foleni kubwa ya maghari(Traffic Jam) na kulikuta gari hilo likiwasubiri

Baada ya kufuata barabara kuingia jijini Dar Es Salaam gari hiyo ghafla ikaingia nyuma ya gari aliyokua akitumia Dr. Slaa aina ya Landcruiser yenye namba za usajili namba T834 BJG. Ndipo afisa wake aliyekua ndani ya gari akapanda juu (Roof Top) na kufanikiwa kulipiga picha gari hilo.

Kuona hilo likifanyika gari hilo likapaki pembeni na ghafla likaondoka na kupotea hadi muda huu walipoingia Ubungo.

Sasa katika mazingira haya taifa linaelekea wapi? Kama watu wanafuatiliwa na kufanyiwa vituko mchana kweupe usalama wa Watanzania na hasa wanaharakati na viongozi wa upinzani Tanzania uko wapi? Mambo haya ni bora yafahamike mapema na watanzania wayajue. Hili ni tukio lisilo la kawaida kipindi hiki ambacho umma umekosa imani (loose confidence) na vyombo vya dola vinavyotumika kwa matakwa ya kisiasa.

Kuna matukio kadhaa yametokea miaka na miezi michache iliyopita yanayotoa taswira mbaya juu ya usalama wa raia na baadhi ya viongozi wanaokosoa utawala. Siku za karibuni Viongozi wa CHADEMA wamekua wakiwindwa sana na tayari chama hiki kikuu cha upinzani kilishatoa tuhuma kwa Usalama wa Taifa na baadhi ya viongozi wa juu serikali kuhusika katika mipango haramu ya kukihujumu chama hicho na hata kufikia hatua ya kuwabambikia kesi viongozi wake.
Wivu na chuki uzushi utawapeleka wapi chadema.Nani ana Muda wa kumfuatilia huyu babu .He is irrelevant mkajipange upya.mmefulia
 
Verified ID?Ni mambo mangapi yameletwa hapa kwa ID hizi hizi kuanzia EPA hadi RICHMOND na kuwa chanzo kikuu cha habari.Masharti na kanuni za JF zimezingatiwa.Tafadhali usituondoe kwenye mijadala
What are you talking about?
Hayo ya EPA, RICHMOND unayosema yameletwa hapa jf na kuwa backed up by hard evidence.

Jf siyo kijiwe cha kahawa kama unataka habari yako watu wenye fikra pevu waiangalie kwa macho mawili na waichukue serious.

Ulicholeta hapa ni kama udaku ambao unaweza kuokota sehemu yoyote ile.
 
Back
Top Bottom