Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

Dkt. Slaa Afuatiliwa na watu wasiojulikana kutoka Iringa hadi Dar Es Salaam

umepotosha watu maana kwenye taarifa ya habari ya star tv slaa ameonyeshwa akiwa anahutubia njombe ina maana alienda dar kulala na leo akaenda njombe?

Jana Star TV walionyesha habari ya juzi.Leo wameonyesha habari ya mkutano wa jana
 
wamechelewa hata kama hakiwatisha ss kumeshakucha na kifo ni moja ya maisha na hujafa ujaumbika na kila siku tunaomba kuona mbingu mbingu haionwi na mtu hai. na ajabu watatukuta hukohuko
 
WANABODI,

Usalama wa viongozi wa chama kikuu cha upinzani Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) upo hatarini.Akiwa njia ni kutokea Iringa, Dr. Slaa amefuatiliwa na Gari aina ya Landcruiser yenye vioo vya giza (Tinted) lenye namba za usajili T963 ABN. Awali waliokua ndani ya gari la Dr. Slaa hawakushtuka sana japo waliona kuna mchezo wa gari hilo kuwapita kwa kasi na kisha kupunguza mwendo ghafla na kisha gari la Dr. Slaa kuwapita tena.Walichukulia kama vile ni mchezo wa kawaida hadi walipofika Morogoro na kushtuka zaidi na kuanza kuchukua tahadhari kwa kunakili namba ya gari hilo


Walipofika kibaha ilibidi watoe taarifa kwa askari wa usalama barabarani.

Dr. Slaa na maofisa wa chama akiwemo afisa habari walishtuka zaidi walipofika njia panda ya Tamko-Bunju ambayo mara nyingi hutumika kunapokua na foleni kubwa ya maghari(Traffic Jam) na kulikuta gari hilo likiwasubiri

Baada ya kufuata barabara kuingia jijini Dar Es Salaam gari hiyo ghafla ikaingia nyuma ya gari aliyokua akitumia Dr. Slaa aina ya Landcruiser yenye namba za usajili namba T834 BJG. Ndipo afisa wake aliyekua ndani ya gari akapanda juu (Roof Top) na kufanikiwa kulipiga picha gari hilo.

Kuona hilo likifanyika gari hilo likapaki pembeni na ghafla likaondoka na kupotea hadi muda huu walipoingia Ubungo.

Sasa katika mazingira haya taifa linaelekea wapi? Kama watu wanafuatiliwa na kufanyiwa vituko mchana kweupe usalama wa Watanzania na hasa wanaharakati na viongozi wa upinzani Tanzania uko wapi? Mambo haya ni bora yafahamike mapema na watanzania wayajue. Hili ni tukio lisilo la kawaida kipindi hiki ambacho umma umekosa imani (loose confidence) na vyombo vya dola vinavyotumika kwa matakwa ya kisiasa.

Kuna matukio kadhaa yametokea miaka na miezi michache iliyopita yanayotoa taswira mbaya juu ya usalama wa raia na baadhi ya viongozi wanaokosoa utawala. Siku za karibuni Viongozi wa CHADEMA wamekua wakiwindwa sana na tayari chama hiki kikuu cha upinzani kilishatoa tuhuma kwa Usalama wa Taifa na baadhi ya viongozi wa juu serikali kuhusika katika mipango haramu ya kukihujumu chama hicho na hata kufikia hatua ya kuwabambikia kesi viongozi wake.
Ungeweka picha ya hilo gari ingependeza zaidi
 
Tangu ufukuzwe Chadema umekua desperate sana kwenye mitandao.....
Inavyoonekana una uzoefu wa muda mrefu pamoja na kujiandikisha jf leo mpaka unafahamu ID za watu hapa jf waliofukuzwa CHADEMA.

Umeanza kuonyesha sura yako halisia. Simama kwenye uzi wako huu .Dude!

Ndiyo maana ninasema, hizi spinning zetu hazitawafikisha mbali. You lack experience on electronic warfare.
 
Turudi kwenye mjadala

Hapa hakuna mjadala. Kuna habari ambayo sio authentic. Sasa tutajadili vipi kitu cha magumashi wakati unayemzungumzia yuko hapa JF na anaweza kutoa maelezo ya kuthibitisha kilichotokea?

Kosa la jina tangu lini likaripotiwa polisi kwa maneno bila kuwa na nyaraka ya maandishi inayothibitisha kutoa ripoti?

Acheni uongo wa kitoto...
 
Inavyoonekana una uzoefu wa muda mrefu pamoja na kujiandikisha jf leo mpaka unafahamu ID za watu hapa jf waliofukuzwa CHADEMA.

Umeanza kuonyesha sura yako halisia. Simama kwenye uzi wako huu .Dude!

Ndiyo maana ninasema, hizi spinning zetu hazitawafikisha mbali.

Huyu jamaa tabia zake kama nyoka mmoja anaitwa COBRA.

I hope you know what am talking about...
 
Spinning at the highest order.

Hivi wewe kwa akili zako kama kweli kuna watu wanataka kuwadhuru viongozi wa CHADEMA watahangaika kwa jinsi unavyoelezea hapa.

Siyo kila jambo ni siasa siasa siasa. Siku hizi mwanasiasa hata akikumbana na vibaka anadai wanasiasa wanamfanyizia.

Jifunzeni kutokuwa wepesi wa kupata majibu kabla ya uchunguzi makini.

Cha kushangaza hao hao watu wa usalama mnaowatuhumu kwa matukio mbali mbali yanayowahusu, ndiyo hao hao mnaotueleza mlienda kulipoti tukio.

Yaani umeamua kuja na ID mahususi kwa ajiri ya SPINNING za kiulinzi.

Kweli tutasikia mengi.
sasa wewe ndo msemaji wa serikali au Magamba?Unatoka povu as if you are very sure with anything. Are you real a Tanzanian by the way? Shameless
 
Ni wazi sasa chama cha demokrasia na maendeleo kimekosa la maana la kuwaambia watanzania ili kuwashawishi kukipa kura katika uchaguzi mkuu mwaka 2015.
Matukio yanayoendelea katika nchi ambayo almost 80% yanakihusisha chadema na matukio haya ni dalili za kupoteza muelekeo kuelekea 2015.
Tumeshuhudia kifo cha mwandishi wa habari mwangosi katika maandamano yasio na kibali cha polisi,
Vifo vya vijana wengine wawili katika nyakati tofauti katika maandamano ya cdm yalioharamu,
Vurugu za bungeni zikiongozwa na Godless Lema.
Uchafuzi wa hali ya usalama wa mji wa Arusha aliosabibisha huyu Lema.
M4c inaondeshwa kiuchonganishi zaidi na sio kuwaelimisha wananchi elimu ya uraia kama kinavyodai cdm kuwa ndio lengo la m4c.
Chama kinalalamika kama yatima na kila tukio utasikia serikali ndio chanzo.
Leo tena Slaa anafuatiliwa mbona mnahangaika kiasi hicho? Matukio yote ya uvunjifu wa amani uliosababishwa na chadema mnayatumia kama mtaji wa kisiasa.

Mtahubiri sana Uvunjifu wa Amani, ndo kazi iliyo bakia kwenu, Wale wamasai wananyang'anywa Aridhi yao si Uvunjifu wa Amani?

Ndo ngao pekee ambayo sisiemu imebaki nayo
 
CHADEMA mmezidi sasa hadi inatia kinyaa! Mnashindwa hata kutunga uongo ukafanana japo kidogo na ukweli?

Njoo na ID yako verified halafu uone kama wiki ijayo hukupelekwa mahakamani kwa kumchafua anayetumia hilo gari ulilotaja namba zake (Kama sio feki).
Vp battybwoy kichaa kimeisha...
 
Kuna watu wengi hawajajisajili JF lakini ni wasomaji kwa muda mrefu
Sasa wewe unamfahamu vipi mtu aliyefukuzwa CHADEMA lakini hatumii verified id na mpaka muda huu ulikuwa haujakuwa jf members wakati yeye unayo.

Something fishy...
 
sasa wewe ndo msemaji wa serikali au Magamba?Unatoka povu as if you are very sure with anything. Are you real a Tanzanian by the way? Shameless
Una maana gani unaposema REAL. Kwa hiyo kwako REAL ni yule anakubali cheap spinning. Kama hiyo ndiyo maana yake, I'm not REAL Tanzania
 
Kuondolewa kwenye mjadala maana yake nini?

Dr. Slaa anapenda sana kujibu habari za udaku hapa JF. Kwanini asije kuthibitisha hii habari in person?

Story za kutekwa siku hizi zimekuwa deal la kupata umaarufu!!!

I know you butt boy about your hatred on Dr Slaa. Nothing new. Son of a devil is a devil.
 
duuuu magamba bwana asa wanafikiri kumpata dr wa ukweli ni raisi ivo analindwa kuliko wanavofikiri na muda wote watu wapo makini ushauri wafanye kazi za wananchi si kufatilia watu wenye mapenzi na nchi yao
 
Back
Top Bottom