Dkt. Slaa: Tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida

Dkt. Slaa: Tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida

Nikifaninisha tukio la Lissu na la ndugu zangu waliopoteza uhai Kibiti, na polisi waliopoteza uhai kwa kushambuliwa wakiwa katika malindo yao naona tukio la Lissu ni la kawaida tu. Viachwe vyombo husika vifanye kazi yao katika uchunguzi wa matukio haya.
Tukio la mwanasiasa wa upinzani kushambuliwa kwa risasi halafu uchunguzi ambao wewe na Dr Slaa mnasema polisi waachiwe, bado hata haujaanza!!

Zaidi, ni kujaribu kuzuia matokeo yake kisiasa yasiwe mabaya! Hizo ndo mbinu ninazoziona hivi sasa!

Slaa atageuka kuwa balozi wa propaganda dhidi ya shambulizi la Lissu.

Kitu kitakachokuwa kimemfanya akubali ni pesa pamoja na visasi!

Baada ya kumtoa supermarket huko Canada, sasa wanamtumia kama toilet paper.
 
FikraPevu Duu Dr. Slaa bora ungekaa kimya tu maana nakumbuka ulipokua Chadema uliwahi kudai ukiwa Igunga kua vyombo vya usalama viliweka vinasa sauti kwenye chumba chako na polisi hukwenda kutoa taarifa ulilaumu hadharani.

Kipindi cha Uchaguzi ukadai serikali imeingiza malori yenye karatasi fake za kupigia kura kupitia njia ya tuduma uliongea hadharani na hukwenda polisi. Uzuri nimegundua watu wakirudi CCM wanaanza kuongea na kuwaza in a rational way
 
Ni kweli kabisa na kila siku nimeendelea kusema humu JF ya kuwa hakuna ushahidi wa kutosha unathibitisha mtu aliyemdungua Lissu risasi. Nikaendelea kuwapa member walalamishi wasiotaka kuelewa wakereketwa wa upande wa pili kama wana evidence wapeleke polisi haki itendeke washukiwa wafikishwe kortini.

Note;"huna haki ya kuzungumza pasipo kuwa na ushahidi wa kile unachokizungumza"
CCTV cameras kufichwa na upande wenu ni evidence tosha....vipi zile footage za clauz Bashite aka Paul Makonda chupuchupu kuwakill vijana wa Shilawandu mulizikataa ....mungu anaona ...endelea kushabikia umwagaji wa damu za watu wa Yehova bila hatia!!
 
Ikiwa mwanadamu mwenye akili timamu anaweza kuliona tukio lile kuwa ni jambo la kawaida....tumedidimia chini mno.
 
  • Thanks
Reactions: 911
Ni kweli kabisa na kila siku nimeendelea kusema humu JF ya kuwa hakuna ushahidi wa kutosha unathibitisha mtu aliyemdungua Lissu risasi. Nikaendelea kuwapa member walalamishi wasiotaka kuelewa wakereketwa wa upande wa pili kama wana evidence wapeleke polisi haki itendeke washukiwa wafikishwe kortini.

Note;"huna haki ya kuzungumza pasipo kuwa na ushahidi wa kile unachokizungumza"
Ndo useme mtu Risasi ni cha kawaida??analaana ya upadre
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Balozi Mteule na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbroad Slaa amesema tukio la Tundu Lissu kupigwa risasi na watu ‘wasiojulikana’ ni jambo la kawaida na ameitaka jamii kuliacha Jeshi la Polisi kukamilisha upelelezi na kutoa majibu.

Wala si ajabu. Ni lazima watu waelewe kuwa Dr. Slaa kwa sasa lazima aongee kwa namna ya kuifurahisha serikali na Magufuli.

Kwani mlitegemea angesema nini? Tundu Lissu au Chadema wako sahihi kuwa kuna dalili za kuwa na mkono wa serikali katika jaribio hili la mauaji?
 
Ni kweli kabisa na kila siku nimeendelea kusema humu JF ya kuwa hakuna ushahidi wa kutosha unathibitisha mtu aliyemdungua Lissu risasi. Nikaendelea kuwapa member walalamishi wasiotaka kuelewa wakereketwa wa upande wa pili kama wana evidence wapeleke polisi haki itendeke washukiwa wafikishwe kortini.

Note;"huna haki ya kuzungumza pasipo kuwa na ushahidi wa kile unachokizungumza"

Huu uzi wako umeuleta kama sehemu ya kutaka kuchota watu mawazo ukidhani hiyo nafasi aliyopewa Slaa ya kupotosha watu itawatoa watu kwenye shaka ya yule wanayemshuku. Kwa taarifa yako huyo Slaa wala haaminiki kama unavyofikiri kiasi kwamba udhani alichosema kinaweza kubadilisha yule tunayemshuku. Huyo Slaa wakati fulani akiwa jukwaani kwenye kampeni aliwahi kutangaza na kuongoza sala fupi ya kumuombea aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Shinyanga wakati huo, kwamba amefariki, wakati si kweli. Slaa huyohuyo aliwahi kusema kuna lorry limeingiza karatasi za kura zilizokwisha pigwa, alizua taharuki ile bila kuripoti polisi zaidi ya kutuhumu waziwazi, matokeo yake lorry lile lilikutwa ni la vipodozi. Slaa huyo huyo aliongoza maandamano yaliyopolekea vifo vya watu watano jijini Arusha kwa kile kilichodaiwa ccm kumpitisha mayor wa wakati huo kinyume na sheria. Je kwanini hakwenda mahakamani wakati ule? Ninamuheshimu sana Slaa, tunamuomba alinde mkate wake bila kupotosha wala kupumbaza watu akidhani bado tuna imani naye kama huko nyuma.

CC: Dr. Wilbroad Slaa
 
Mwacheni aendeleze siasa bongo asishangae siku anarudishiwa airport Canada
Lissu mwenzio nanihii wa mihogo anasema waliokupiga risasi walifanya jambo la kawaida
TL huko uliko unaishi na vyombo vya haki za binadamu mlipue huyu mzandiki kwa wenye akili mpaka ajue maharage ni mboga sio kitafunio
Utasemaje kupigwa risasi ni jambo la kawaida? Slaa mtafute aliyekuloga
No wonder upadre ulishindwa
Kuukosa urais ndio ujitoe ufahamu kiasi hiki
Mbona wewe hukusema waliokuvunja mkono walifanya jambo la kawaida
Mungu angekuwa anaadhibu wazandiki hawa huku tunaona
Ungeweza kazi ya urais kweli?
Huna huruma si mstaarabu mchoyo mbinafsi huna kumbukumbu sasa urais huu si ungetuangamiza wote
Mpeni Mungu yaliyo ya Mungu ya Kaisari yaliyo ya Kaisari
Tukisema Slaa unashirikiana na wasiojulikana unaweza kusaidia kujibu shambulio la Lissu tutakuwa tunakosea??!
 
Mkuu, kwenye criminal case kwa kawaida huwa kunakuwa na Potential suspects ......... sasa kinachozungumziwa humu ni potential suspects. Potential suspects naye huwa anaweza kujisafisha mwenyewe. Dr. Slaa must know better!!

Hata huko Canada anakokuzungumzia kama kuna potential suspect police huwa wanamfuata na kumhoji .... kama hakuna huwa wanajaribu kuto features au michoro tena hata hadharani ili raia wema wasaidie kuwaidentify wahalifu.

Kwa kawaida watu hawawezi kwenda tu police kutoa ushaidi unless wameombwa ..... kwa nini hawakutangaza number ambayo raia wanaweza kutoa taarifa kwa siri au hata kutoa posho ya million 10 kwa yule atakayesaidia kutoa ushahidi!!?
mkuu nadhani tuna lack wataalam wa hayo mambo huenda ika sijasema na uhakika chamsingi ni kuleta vyombo huru vya uchunguzi vitende kazi ndugu.
kuhusu kuweka nambari ya mawasiliano nadhan polisi wana kitengo hicho hivyo nisiwe msemaji sana juu ya hilo niwaachie vyombo husika.
 
Yeye ile list of shame alikwenda kutoa taarifa Polisi au TAKUKURU? Au anavyokomaa kuwa Lowasa ni fisadi kuna taarifa yoyote aliyoipeleka TAKUKURU?
Swali gumu nadhani au naona shujaa ametekwa analazimika kutamka asiyo yataka taafifu mungu wangu
 
Ni kweli kabisa na kila siku nimeendelea kusema humu JF ya kuwa hakuna ushahidi wa kutosha unathibitisha mtu aliyemdungua Lissu risasi. Nikaendelea kuwapa member walalamishi wasiotaka kuelewa wakereketwa wa upande wa pili kama wana evidence wapeleke polisi haki itendeke washukiwa wafikishwe kortini.

Note;"huna haki ya kuzungumza pasipo kuwa na ushahidi wa kile unachokizungumza"
Acha ujinga, unapomzungumzia Mungu ina maana unakuwa umeonana naye?
 
Sasa naanza kuiona hadharani chuki ya Dkt Slaa kwa chadema, kauli yake ya "hili Ni Jambo la kawaida" imenifumbua macho. Mbunge alishambuliwa kwa risasi zaidi ya 20+ . Unadiriki kusema Ni Jambo la kawaida? Najiuliza maswali mengi sana juu ya Msomi Dkt Slaa.
 
Wakati wa kumuanika huyu mzee hadharani sasa umefika rasmi , tukimuacha atadhani tunamuogopa , ukiheshimiwa na ukashindwa kujiheshimu basi unastahili kipondo .

Wito - JF msiingilie tuachieni tupeane taarifa Muhimu .

Nakala kwa Salary Slip , Chakaza .

Mkuu katika watu waliokuwa wanamuheshimu Slaa mimi ni mmojawapo. Nimejizuia sana kumtamka vibaya hata kama sikufarahishwa na maamuzi yake ya kujitoa cdm ila niliheshimu uamuzi wake, na mchango wake katika ujenzi wa cdm yenye nguvu. Lakini kwa hili aliloliongea leo kuhusu Lissu ni wazi ameamua kupigania maslahi yake kwa lengo la kupotosha kwa kuwa anaona ana hadhira ya kumsikiliza. Nakupa baraka zote, mwaga mboga ili ajue watu wanamstahi kisha anataka kupotosha ukweli kwa maslahi yake.
 
Anashangaza sana huyu Mzee ni bora akae kimya ili kujitunzia heshima yake ndogo iliyobaki badala ya kuropoka pumba na kuzidi kujidharaulisha.

Chimbua zaidi , amewataka mwenyewe.
 
Ni jambo la kawaida kwenye nchi ipi kwa mbunge kupigwa risasi hadharani ? Ni Tanzania hii au ? Shibe mwanamalevya ,Sasa yeye alikuwa analalamika nini mkewe kupasuliwa Arusha ? Angetulia tu maana ni mambo ya kawaida ile list of shame yeye aliipeleka polisi ? Siasa ni usenge fulani hivi
 
Hata alipoanguka bafuni akavunjika mkono bado hawakusema ni kawaida. Pia alipowekewa vinasa sauti kitandani kule Dodoma!
Huyu Slaa wa ajabu kwelikweli!Wenziye wakizeeka wanamkana "shetani" (ref:Kingunge,Sumaye,& Other Coys).Sasa yeye anamkumbatia shetani na kumbusu.Awe na hadhari,ataungua mdomo na moyo!
 
Back
Top Bottom