Dkt. Sule: Kutumia Majini kupata Mali si dhambi/ haramu

Dkt. Sule: Kutumia Majini kupata Mali si dhambi/ haramu

Mizimu kila mtu anayo, tunachotofautiana ni unamizimu ya aina gani? Ipo mizimu ya kimasikini, mizimu ya maradhi, mizimu ya kuvuruga mahusiano mizimu ya utambuzi , mizimu ya kichawi , mizimu ya utajiri n.k

Hao ulio wataja wana mizimu ya utambuzi mizimu ya kiganga kwenye watu elfu 30 unaweza kupata wawili au watatu tu.
Kazi ipo
 
Hawa watu ni waganga wa kienyeji wanawashika masikio waislamu wanaopenda short cut na wasio na maarifa wala utambuzi juu ya dini yao, habari za kuabudu na kuomba msaada majini ni katika madhambi yanayomtoa mtu kwenye uislamu.

Na siku atakayowakusanya wote, kisha atawaambia malaika: "Hivi hawa walikuwa wakiwaabudu nyinyi"? watasema: "Tunakutakasa kukutakasa, wewe ndiye kipenzi chetu kinyume na wao, bali wao walikuwa wakiwaabudu majini, wengi wao wakiwaamini hao".

Qur'an 34:40-41

Huu ndio uislamu wa sawasawa unamtaka mtu kufanya kazi na kutafuta rizki ya halali, na si kutumia ushirikina wala kafara na matambiko na kuwanyenyekea majini kupata mali, nimeona hapo juu watu wengi wameutukana uislamu kwasababu ya neno la mtu mmoja asiyejua hata uislamu ni nini.

Wakuu kuweni na uvumilivu sisi ndo tumeshakuwa waislamu na tutabaki hivyo mpaka siku ya kufa kwetu kwa idhini ya allah, punguzeni chuki na muache matusi yasiyo na maana, uislamu uko mbali na kuabudu na kuwataka msaada mashetani.
Samahani mkuu, kwa hiyo wewe hauamini kama kuna ushirika wa Majini na Waislam ambao unaruhusiwa kwa mujibu wa imani?.

Vipi zile kauli za uwepo wa Majini mema yanayomuabudu Allah kwa kushirikiana na Waislam si za kweli?.

Naomba unisaidie kuondoa mkanganyiko huo.
 
Mimi sio mwisilam ila Mganga sule ni yuko shallow sana kwenye dini lakini anatafuta attention to mitandaoni mara awadiss wasanii Yani ni chizi wa umaarufu
Exactly anatumia ule uwezo wa kuongea sana wa huko pwani, na hawa watu wa kufanya mijadala ya biblia na wachungaji ndio zao, na wanagawana sadaka zinazopatikana na wanawauzia watu dua, dua zinauzwa?.

Kuna mahala nilipata kuona waliwapa watu wote uwanjani ndizi za kuiva, kisha wale watu wakaanza kutapika uwanja mzima wao sasa wakawauzia sijui dawa ili wakae sawa, ni upuuzi na uganga wa kienyeji kwa jina la uislamu na wanawakamata wengi, hapo amesema hivyo ili aanze kutafutwa na watu wajinga awatapeli.
 
Samahani mkuu, kwa hiyo wewe hauamini kama kuna ushirika wa Majini na Waislam ambao unaruhusiwa kwa mujibu wa imani?.

Vipi zile kauli za uwepo wa Majini mema yanayomuabudu Allah kwa kushirikiana na Waislam si za kweli?.

Naomba unisaidie kuondoa mkanganyiko huo.
Naam mkuu wangu, mimi ni muislamu wa kuzaliwa na ni mwanafunzi niliyechukua faragha kuisoma dini namaanisha nina miaka 10+ nikiwa nasoma na bado ningali darasani, ninachokueleza hakuna ushirika wowote baina ya majini na wanadamu bali wao ni viumbe mbali na sisi ni viumbe mbali.

Mkanganyiko uliopo ni huu ufuatao na nitasema ukweli kwa mujibu wa uislamu, majini ni viumbe kama sisi wameumbwa kwa malengo ya kuabudu kama sisi, wao wapo kwenye ulimwengu usioonekana na sisi tupo kwenye ulimwengu huu unaoufahamu, kuna wema na waovu kama ilivyokuwa kwetu wanadamu, na wao wana maisha yao na sisi tuna maisha yetu.

Ama kuhusu ushirika au ushirikiano wowote baina ya waislamu wanadamu na waislamu majini huu haupo kabisa, bali ukifanya hivyo ndio maana halisi ya ushirikina unaopigwa vita na uislamu tangu hapo kale.

Amesema allah aliyetukuka: "Na wamemfanyia Allah majini kuwa washirika wake, na hali ya kuwa yeye ndiye aliyewaumba, na wakamzulia kuwa ana watoto wa kiume na wa kike pasi na elimu yoyote, ametakasika kutakasika kabisa! na ametukuka juu ya hayo wanayomsifia!".

Qur'an 6:100

Sasa ni jambo lisilowezekana Qur'an ambayo ndiyo sheria mama kwenye uislamu ijigonge yenyewe kwa yenyewe, nadhani nimefafanua kama una swali au hujaelewa naweza kueleza tena kwa namna nyingine, asante.
 
Hawa watu ni waganga wa kienyeji wanawashika masikio waislamu wanaopenda short cut na wasio na maarifa wala utambuzi juu ya dini yao, habari za kuabudu na kuomba msaada majini ni katika madhambi yanayomtoa mtu kwenye uislamu.

Na siku atakayowakusanya wote, kisha atawaambia malaika: "Hivi hawa walikuwa wakiwaabudu nyinyi"? watasema: "Tunakutakasa kukutakasa, wewe ndiye kipenzi chetu kinyume na wao, bali wao walikuwa wakiwaabudu majini, wengi wao wakiwaamini hao".

Qur'an 34:40-41

Huu ndio uislamu wa sawasawa unamtaka mtu kufanya kazi na kutafuta rizki ya halali, na si kutumia ushirikina wala kafara na matambiko na kuwanyenyekea majini kupata mali, nimeona hapo juu watu wengi wameutukana uislamu kwasababu ya neno la mtu mmoja asiyejua hata uislamu ni nini.

Wakuu kuweni na uvumilivu sisi ndo tumeshakuwa waislamu na tutabaki hivyo mpaka siku ya kufa kwetu kwa idhini ya allah, punguzeni chuki na muache matusi yasiyo na maana, uislamu uko mbali na kuabudu na kuwataka msaada mashetani.
Mbona nawasikiaga' Waislam wengi tu wanazungumzia hayo.majini.kama maswahiba wao
.mara nna jina langu !na blabla.kibao....
 
Mbona nawasikiaga' Waislam wengi tu wanazungumzia hayo.majini.kama maswahiba wao
.mara nna jina langu !na blabla.kibao....
Naam hao ni waislamu washirikina mkuu, wanadai uislamu na bado wana makando kando yao na wengi utakuta ni waislamu wa ukanda wa pwani yaani dar, zanzibar, lindi, mtwara, na tanga na uislamu uko mbali kuliko umbali wa mbingu na ardhi kuhusu huo ushirika.
 
Sule ni mwanazuoni mkubwa kwaiyo anajua dini hiyo kuliko wewe
Mwanazuoni ? nani alimpa title ya mwanazuoni ? Alisomea chuo gani kinachojulikana duniani kwa elimu ya dini ya kiislamu? University of madina?, dammaj ? Al azhar ? E.t.c

Kingine uislamu unaenda kwa dalili na dalili tunazipata kutoka kwenye quran na sunna pekee nje ya hapo ni uzushi, kikawaida inatakiwa kumtegemea na kumuomba Allah( the all knowing, all powerful) kwenye kila jambo letu wanaadamu majini ni viumbe vya Allah (the almighty) kama tulivyo binadamu , malaika na wengineo .

Nao wanamtegemea Allah( the almighty) kwenye kila kitu , sasa ni ajabu kwa binadamu kutegemea kiumbe kinachokufa kama yeye huu ni ujinga na unatakiwa ukemewe kama aya hii hapa inavyojieleza kwenye surat jinni.

Al-Jinn 72:6

وَأَنَّهُۥ كَانَ رِجَالٌ مِّنَ ٱلْإِنسِ يَعُوذُونَ بِرِجَالٍ مِّنَ ٱلْجِنِّ فَزَادُوهُمْ رَهَقًا

Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani

"Na hakika walikuwako wanaume katika watu walio kuwa wakitafuta kujikinga kwa wanaume wa kijini; kwa hivyo wakawazidisha madhambi."

Mwisho wa kunukuu.

Majini wanaelezea kwamba walikuwapo wanaume katika binadamu waliokuwa wanajikinga kwa wanaume wa kijini na hivyo wakajikuta wanazidisha madhambi kwa maana haitakiwa kutaka kumtegemea kiumbe ila Allah(the almighty) .


Ushauri
Si kila anayejiita shaikh/mwanawachuoni huwa anasifa hiyo kwanza kwa Tanzania waliosoma Elimu ya dini kwa kufuata misingi ya salafi swaleh ambao ni msingi bora kabisa ni wachache wengi waliobaki ni wanafuata uzushi bila ya kutaka kujifunza na wanajikuta wanawapotosha watu pamoja na kujipotosha wao wenyewe kama ilivyonukuliwa kwenye hadithi hii hapa.

Sahihi muslim , 2673

حَدَّثَنَا قُتَيْبَةُ بْنُ سَعِيدٍ، حَدَّثَنَا جَرِيرٌ، عَنْ هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ، عَنْ أَبِيهِ، سَمِعْتُ عَبْدَ، اللَّهِ بْنَ عَمْرِو بْنِ الْعَاصِ يَقُولُ سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ ‏ "‏ إِنَّ اللَّهَ لاَ يَقْبِضُ الْعِلْمَ انْتِزَاعًا يَنْتَزِعُهُ مِنَ النَّاسِ وَلَكِنْ يَقْبِضُ الْعِلْمَ بِقَبْضِ الْعُلَمَاءِ حَتَّى إِذَا لَمْ يَتْرُكْ عَالِمًا اتَّخَذَ النَّاسُ رُءُوسًا جُهَّالاً فَسُئِلُوا فَأَفْتَوْا بِغَيْرِ عِلْمٍ فَضَلُّوا وَأَضَلُّوا ‏"‏ ‏.‏

Translation

Verily, Allah does not take away knowledge by snatching it from the people but He takes away knowledge by taking away the scholars, so that when He leaves no learned person, people turn to the ignorant as their leaders; then they are asked to deliver religious verdicts and they deliver them without knowledge, they go astray, and lead others astray

Tafsiri

Hakika Mwenyezi Mungu haiondoi elimu kwa kuinyakua kwa watu, bali anaiondoa ilimu kwa kuwatoa wanavyuoni, ili asipomwacha msomi, watu wanawaendea wajinga kuwa viongozi wao; kisha wanaombwa watoe hukumu za dini na wanazitoa bila ya kuwa na elimu, wanapotea na wanawapoteza wengine.

NA ALLAH (THE ALMIGHTY) ANAJUA ZAIDI
 
Naam mkuu wangu, mimi ni muislamu wa kuzaliwa na ni mwanafunzi niliyechukua faragha kuisoma dini namaanisha nina miaka 10+ nikiwa nasoma na bado ningali darasani, ninachokueleza hakuna ushirika wowote baina ya majini na wanadamu bali wao ni viumbe mbali na sisi ni viumbe mbali.

Mkanganyiko uliopo ni huu ufuatao na nitasema ukweli kwa mujibu wa uislamu, majini ni viumbe kama sisi wameumbwa kwa malengo ya kuabudu kama sisi, wao wapo kwenye ulimwengu usioonekana na sisi tupo kwenye ulimwengu huu unaoufahamu, kuna wema na waovu kama ilivyokuwa kwetu wanadamu, na wao wana maisha yao na sisi tuna maisha yetu.

Ama kuhusu ushirika au ushirikiano wowote baina ya waislamu wanadamu na waislamu majini huu haupo kabisa, bali ukifanya hivyo ndio maana halisi ya ushirikina unaopigwa vita na uislamu tangu hapo kale.

Amesema allah aliyetukuka: "Na wamemfanyia Allah majini kuwa washirika wake, na hali ya kuwa yeye ndiye aliyewaumba, na wakamzulia kuwa ana watoto wa kiume na wa kike pasi na elimu yoyote, ametakasika kutakasika kabisa! na ametukuka juu ya hayo wanayomsifia!".

Qur'an 6:100

Sasa ni jambo lisilowezekana Qur'an ambayo ndiyo sheria mama kwenye uislamu ijigonge yenyewe kwa yenyewe, nadhani nimefafanua kama una swali au hujaelewa naweza kueleza tena kwa namna nyingine, asante.
Nimekuelewa, ingawa sasa matendo ya viongozi na maneno yao ya kiimani wanayoyatenda huku mitaani, nadhani yamechagiza baadhi kuisema isivyofaa imani hiyo.

Utakuta mhusika ni Imam, Shekh au Usitadhat ila anahubiri habari za majini na ushirika wake na Waislam au anamiliki kiringe kihalali kwa ajili ya tiba zinazohusisha majini.

Nimeelewa wafanyayo hayo, wako kinyume na Uislam ingawa bado wanaitwa/wanajiita Waislam.
 
Kwa wasioelewa niwafungue ufahamu. Majini Ni malaika walioasi Wakatupwa Duniani pamoja na Bosi wao Lucifer . Hiyo Ndio maana ya Majini.
Soma ufunuo wa Yohana 12 yote utanielewa
Sasa NI dhahiri kuwa Huwezi tenganisha Ile Dini na Majini Hilo liko dhahiri. Sasa unaweza elewa wanamuabudu Nani. Somebody says Akifa anaenda peponi kuoa wanaweka wenye macho kama vikombe😂😂😂 Hayo yanaitwa majini mahaba Muhammad alifunuliwa na shetani. Ndio maana wakaanzia practice Duniani kuoa wanawake wengi. Sasa wengi wanajitahidi kutimiza masharti ya Dini yao Ili wakajipatie mademu huko wenye macho kama vikombe.
Hivi nikuulize wewe kama Una akili nzuri! Huo mwili ulionao ukifa tu umeuvua Je hiyo Ngono Utafanya na nini huko?
Kwa nini mnakubali kufia Kwenye dhambi Kwa uongo wa shetani. Kumbuka Shetani aliichezesha Bibilia kidogo tu Ili aanzishe kundi lake jipya la kwenda nalo Jehanam
Bibilia Inasema Shetani Ndio baba wa uongo wote Unaona uongo wote unaoongelewa huku Duniani Shetani Ndie baba wa uongo huo. Sasa alichukua Bibilia akageuza Baadhi ya maneno ambayo Ndio msingi wa Muumini akaandika cha kwake akampa Muhammad. Mfano angalia alivyocheza na Kitabu cha Mwanzo Habari za Ibrahim Kisha angalia vita yake kubwa iko Kwenye injili Hataki kabisa injili ihubiriwe amepingana nayo kwa nguvu zote hadi Leo. Hataki kabisa
Ndio maana vita ya Yesu aliileta Rohoni maana Majini nayo NI roho yanaonyeshwa cha Moto na Mnazareti. Maana Mnazareti Ndie ameukalia ulimwengu wa Roho Alienda huko kuzimu akamuambia Shetani leta funguo hizo haraka sina muda kupoteza
Shetani akampa: Akamuambia Shika Mkuu
Yesu akaingia zake Mjini Akasema Nimepewa mamlaka Yote Mbinguni na Duniani, Akawaambia wanafunzi Sasa enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi wangu.
Ni kiu yangu tuende Mbinguni pamoja Asiwepo anayepotea. Na Yesu Ndie njia kweli na uzima. Wokovu NI sasa baada ya kufa NI hukumu tu Hakuna kuoana tena huo ni uongo wa shetani. Mpe Yesu Maisha
Yeye Ndie njia kweli na uzima
Asante.
 
Nimekuelewa, ingawa sasa matendo ya viongozi na maneno yao ya kiimani wanayoyatenda huku mitaani, nadhani yamechagiza baadhi kuisema isivyofaa imani hiyo.

Utakuta mhusika ni Imam, Shekh au Usitadhat ila anahubiri habari za majini na ushirika wake na Waislam au anamiliki kiringe kihalali kwa ajili ya tiba zinazohusisha majini.

Nimeelewa wafanyayo hayo, wako kinyume na Uislam ingawa bado wanaitwa/wanajiita Waislam.
Hao ni waganga wa kienyeji mkuu na ukifanya utafiti utakuta ndio wapiga ramli wanaosaidia watu sijui kupata kazi kumleta mpenzi karibu, kuwawekea limbwata wanandoa na mambo kama hayo, jua mkuu uislamu ni mpana sana wengi katika hao unaowataja wala hawana maarifa stahiki ya uislamu.
 
Back
Top Bottom