Dkt. Sule: Kutumia Majini kupata Mali si dhambi/ haramu

Dkt. Sule: Kutumia Majini kupata Mali si dhambi/ haramu

Naona wagalatia wanakuja mbio na matusi pasi na kujua Sule kazungumza nini.
Mleta mada ungeweka video watu wasikilize sio kuleta maneno baadhi yenye mkanganyiko.
Sule alichosema ni kuwa kuwatumia majini wenye mali kupata mali sio haramu.
Ila katika kuwatumia huko ni kwa kumuomba Mungu hao majini watii kwa kupitia neno la Mungu.
Kuna majini wanashikilia mali za dhahabu,almasi,ruby.
Unawafanyaje watii wakugaie mali?
Ni kupitia visomo vitakaowafanya wanyeyekee kwa jina la Mungu.
Na Sule alitanabaisha kuwa sio kwa kutumia makafara kutoka kwa waganga na ukapewa mapepo ya kafara laa hasha huo ushirikina.
Ila kwa kutumia kumuomba Mungu ili uwanyenyekeshe majini hilo ni sawa.
Kama Nabii Suleyman alikua akiwanyenyekesha majini kwa kumtaja Mungu maana Mungu ndio kaumba hao majini.
Narudia Sule hakukusudia kutumia mashetani ya kafara.
Kuna kitu katika uislam tunakiita Khadiim,maana yake mtumishi wa kiroho.
Hao watumishi wa kiroho wapo malaika na majini wasafi ambao huwezi kuwaona abadan mpaka ufanye utajo wa Mungu.
Na ukiwa mtu wa ibada sana katika masiku meupe hawa viumbe wanaweza kukutembelea pasi na wewe hata kuwaita ukashangaa wamekutembelea.
Niishie tu hapa ila kiufupi Dr Sule hajakusudia mashetani ya kafara.

Cha kuongezea,hao khudaam huwezi kuwafuga hawafugiki ng'oo.
Bali unawanyenyekesha na wakitimiza ulichoomba wanaondoka na mpaka warudi tena aisee ufanye kazi uache kazi.
Yani khadim ni sawa na nyota ya jaa.
Umesomeka sheikh kuna watu wanadandia gari kwa mbele
 
Quran 27:17 Na alikusanyiwa Suleiman majeshi yake ya majini, na watu na ndege nayo yakapangwa kwa nidhamu.

Msingi wa wakuyatumia majini uko hapo binadamu mwenye elimu juu ya anachokifanya bila kumshirikisha Mwenyezi Mungu majini ni kama mbwa unatuma anakufanyia kazi zako sema wasio kuwa na elimu ni waoga kwakua hawana elimu na kuzusha vitu someni mjue
Umemaliza kila kitu
 
Naam hao ni waislamu washirikina mkuu, wanadai uislamu na bado wana makando kando yao na wengi utakuta ni waislamu wa ukanda wa pwani yaani dar, zanzibar, lindi, mtwara, na tanga na uislamu uko mbali kuliko umbali wa mbingu na ardhi kuhusu huo ushirika.
Aisee...Sasa hii imekomaa sana,hadi sisi wengine tunaihusisha Dini ya Kiislam na hao viumbe ...kuwa Wana undugu! Sasa mbona huwa halikemewi Kwa nguvu! Kama anavyokemewa Nguruwe!?
 
Kati ya majini 99 haya hapa ni baadhi. Sina muda wa kueleza kazi zake ambazo ni mbaya kwa ujumla hakuna jini mzuri hata mmoja. Jini badri/albadri, jini zohari/zuhura, jini zabaniat, jini mwarabu/araba, jini khadtazi/kaim, jini subisubi/subian, jini jabrin/juber, jini maimuna, jini makata. Orodha ni ndefu naishia hapo majini yote ni makorofi ila kuna jini taariki kazi yake ni kufarakanisha na kutoa amani akijifanya ni mwema kumbe ni hatari. Wafuga majini ni washirikina
 
Kama ni suala la kumuomba Allah(the almighty) akukinge na hila za mashaitan ni swahihi , samahani kama sikuelewa nini ulimaanisha .

Ila kuhusu surat kawthar mara 1000 wacha nifuatilie zaidi.

ALLAHU A'LAM.
Elim ni pana sana zaidi tunavyo fikiria,kutojua kitu fulani haimanishi hakipo,tuendelee kujifunz
 
Kuna jini anaitwa Tajirun, ni jini wa kifahari. Hutumwa kwa mtu afanye kila jambo au kazi yeyote ili awe tajiri. Jini huyu hukupa moyo wa kupenda pesa kuliko Mungu. Ana uwezo wa kufanikisha miradi yako na kufanikiwa sana lakini hutakuwa kabisa na Mungu. Hayo yanayosemwa ni majini mazuri mwisho wake hugeuka kuwa mabaya. Hakuna jini mzuri
 
Kuna jini anaitwa Tajirun, ni jini wa kifahari. Hutumwa kwa mtu afanye kila jambo au kazi yeyote ili awe tajiri. Jini huyu hukupa moyo wa kupenda pesa kuliko Mungu. Ana uwezo wa kufanikisha miradi yako na kufanikiwa sana lakini hutakuwa kabisa na Mungu. Hayo yanayosemwa ni majini mazuri mwisho wake hugeuka kuwa mabaya. Hakuna jini mzuri
Majini ni viumbe agressive sana.
Ndio maana kidini ni marufuku kushirikiana nao.
Kitendo cha kutumwa kwako umtumie ni sawa na unashirikiana nae.
Haifai.
 
Kati ya majini 99 haya hapa ni baadhi. Sina muda wa kueleza kazi zake ambazo ni mbaya kwa ujumla hakuna jini mzuri hata mmoja. Jini badri/albadri, jini zohari/zuhura, jini zabaniat, jini mwarabu/araba, jini khadtazi/kaim, jini subisubi/subian, jini jabrin/juber, jini maimuna, jini makata. Orodha ni ndefu naishia hapo majini yote ni makorofi ila kuna jini taariki kazi yake ni kufarakanisha na kutoa amani akijifanya ni mwema kumbe ni hatari. Wafuga majini ni washirikina
😂😂😂Kaka kuna majini zaidi ya 10000.
Hawa ni vipepo vichafu mkuu.
Ila kuna falme za majini huwezi kutana nao mpaka watake wao.
Hawa ndio huitwa khudaam.
Mfano;
-Aswaarul Kabiir.
-Hamamah.
N.k n.k,hawa wakitia timu sehem hadi mapepo machafu wakina maimuna wanakimbia kwa kishindo.
Huwezi kuwatumia kirahisi na huwezi kuwafuga kamwe.
Hawa ndio majini wa koo za kifalme.
 
Kama ni suala la kumuomba Allah(the almighty) akukinge na hila za mashaitan ni swahihi , samahani kama sikuelewa nini ulimaanisha .

Ila kuhusu surat kawthar mara 1000 wacha nifuatilie zaidi.

ALLAHU A'LAM.
Mkuu kuna kisomo cha ruqyah cha suratul yaasin 71.
Hiko pia unakijua?
Hiyo ni ruqyah kaka kaifuatilie,ina uwanda mpana,ruqyah ni kisomo cha Qur'an cha kumuomba Allah akisaidie kutatua shida zako mbali mbali ikiwemo za kiuchumi.
Kuna kisomo cha suratul ikhlasw 1000 pia.
Hikma yake ni nzito mzee.
Qur'an ina maajabu makubwa ya ruqyah.
 
Si kila mwanawachuoni ni wa kumfuata narudia tena watu tusome kwa misingi ya salafi swaleh ili tuweze kuielewa dini kama ambavyo inatakikana .

Kuwanyenyekeza kwa minajili ipi? Mtume alishindwa kuwanyenyekeza ili awatumie kwenye vita vyoote alivyopigana? Jibu ni hakushindwa ila alifanya nini kama mbadala? Jibu ni alimtegemea Allah(the all powerful) kwenye kila jambo lake .

Majini waachwe waishi maisha yao na sisi tuishi maisha yetu kwa kumtegemea Allah (the almighty )kwenye kila jambo unapoanza kuingiliana na hao viumbe utajikuta unaingizwa kwenye shirki kubwa angalia aya ya 102 ya surat baqara nanukuu.

Al-Baqarah 2:102

وَٱتَّبَعُوا۟ مَا تَتْلُوا۟ ٱلشَّيَٰطِينُ عَلَىٰ مُلْكِ سُلَيْمَٰنَۖ وَمَا كَفَرَ سُلَيْمَٰنُ وَلَٰكِنَّ ٱلشَّيَٰطِينَ كَفَرُوا۟ يُعَلِّمُونَ ٱلنَّاسَ ٱلسِّحْرَ وَمَآ أُنزِلَ عَلَى ٱلْمَلَكَيْنِ بِبَابِلَ هَٰرُوتَ وَمَٰرُوتَۚ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنْ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَآ إِنَّمَا نَحْنُ فِتْنَةٌ فَلَا تَكْفُرْۖ فَيَتَعَلَّمُونَ مِنْهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِۦ بَيْنَ ٱلْمَرْءِ وَزَوْجِهِۦۚ وَمَا هُم بِضَآرِّينَ بِهِۦ مِنْ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذْنِ ٱللَّهِۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمْ وَلَا يَنفَعُهُمْۚ وَلَقَدْ عَلِمُوا۟ لَمَنِ ٱشْتَرَىٰهُ مَا لَهُۥ فِى ٱلْءَاخِرَةِ مِنْ خَلَٰقٍۚ وَلَبِئْسَ مَا شَرَوْا۟ بِهِۦٓ أَنفُسَهُمْۚ لَوْ كَانُوا۟ يَعْلَمُونَ

Swahili - Ali Muhsin Al-Barwani

Na wakafuata yale waliyo zua mashet'ani kuuzulia ufalme wa Su leiman. Na wala Suleiman hakukufuru, bali mashet'ani ndio walio kufuru, wakiwafundisha watu uchawi, na yaliyo teremshwa kwa Malaika wawili, Haaruta na Maaruta katika Baabil. Wala hao hawakumfundisha yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani; basi usikufuru. Wakajifunza kwa hao wawili yale ya kumfarikisha mtu na mkewe. Wala hawawezi kumdhuru mtu ila kwa kutaka Mwenyezi Mungu. Na wanajifunza yatayo wadhuru wala hayawanufaishi. Na hakika wanajua kwamba aliye khiari haya hatakuwa na fungu lolote katika Akhera. Na hakika ni kiovu mno walicho jiuzia nafsi zao laiti wangelijua.

Mwisho wa kunukuu.

Unaposoma aya hiyo hapo unagundua kwamba wapo pia walioweka ukaribu na mashetani (jinni ni jamii ila shetani ni sifa na kuna shetani wa kijini na wa kibinadamu).

Na hao mashetani wakawafundisha wao uchawi ambao ni kufru kubwa kabisa na dhambi ambayo ukifa haujatubia basi haina msamaha na mtu ataingia motoni milele.

Hivyo ushauri wangu ni kuisoma dini kutoka kwa wanawachuoni wanaoaminika na ambao wanafuata quran na sunna .

NA ALLAH (THE ALMIGHTY) ANAJUA ZAIDI.
Suleiman mwenyewe aliwatumia majini kwa kazi zake tena wazi wazi alipouliza majini na watu kipindi anataka wamletee kiti cha malkia wa Sheba ndio jini mmoja akajitokeza akasema atakileta kwa muda kabla ya kukaa akagoma akaja mwenye elimu zaidi ambaye ni binadam kwa muda kupesa jicho mara moja Nabii akamwambia akilete
 
😂😂😂Kaka kuna majini zaidi ya 10000.
Hawa ni vipepo vichafu mkuu.
Ila kuna falme za majini huwezi kutana nao mpaka watake wao.
Hawa ndio huitwa khudaam.
Mfano;
-Aswaarul Kabiir.
-Hamamah.
N.k n.k,hawa wakitia timu sehem hadi mapepo machafu wakina maimuna wanakimbia kwa kishindo.
Huwezi kuwatumia kirahisi na huwezi kuwafuga kamwe.
Hawa ndio majini wa koo za kifalme.
Du ,wewe ni Muislam!
 
Back
Top Bottom