Dkt. Vicencia Shule: Ubora wa filamu ya Royal tour ni wa kiwango cha chini. Hata vijana wa bongo movie wangeweza kuitengeneza

Producer ana Emmy award,director ni nominee wa awards nyingi USA,kafanya royal tour na Poland,Mexico,Israel na rwanda ..leo waharibu franchise yao kwa Tanzania!!!?
 
John cosmas ngoteya,miaka mitano iliyopita nikimuona alifanya promo national geographic,juzi nikaona kampuni yake imefanikiwa kurusha national grographic
Kijana kwa sasa ni habari nyingine anavifaa sana vya maana

National gr ishakuwa home
 
basic drone shots, basic camera movements/shots, color grading hata sijui kama walifanya? Kwa hiyo hela trust me kuna vijana bongo wangetoa kitu kizuri mno
Mtaalam, Mbona hatujawahi kuona hizo docs kutoka kwa vijana wabongo zenye hizo basic issues kama unavyosema!
 
Huku sasa ni kupoteza nini jamani, dira au muelekeo?
Mbona tunakosoa hadi yasiyo tuhusu??

Idea siyo yetu! Filamu siyo yetu! Fedha siyo zetu! Audience lengwa siyo akina sisi!
Sasa kama watengenezaji wenyewe wanatamka wazi kwamba hii ya SSH imekuwa bora zaidi kuliko RT zingine za nyuma sisi ni nani tukatae?

Nadhani kuna wengi hawajui mengi kuhusu Royal Tour. Labda kuna scenes watu walishazizoea basi hawazioni kwenye hii RT.

Mimi nishashiriki maandalizi ya promotional video kwa ajili ya watalii wa dunia ya leo... mtaalamu mmarekani alikazia kuwa iwe very organic as possible, casual na siyo scifi ~science/fictional. Niche ya watalii na wawekezaji wenye fedha zao wanaokuja TZ ni retired veterans. Peter Greenberg wa RT anajua wanataka nini na awapa wanachokita! Nadhani hapo RT wamefanikiwa!
Zaidi ya yote nyuma yake kuna nguvu kubwa sana... Kufanya RT na viongozi wa nchi si jambo la mchezo!

Sisi tuachane kabisa na hoja za ubora turudi kwenye hoja za msingi.
Tufukunyue kuhusu nani yupo nyuma ya harakati za kumuondoa Masai Ngorongoro. Je, ule ujenzi wa mtandao wa mahoteli ya kifahari hifadhini ni muendelezo wake?
Je, hizi harakati za RT zinahusika? Kwa gharama za nani, faida ya nani, ili iwe nini?

NB: Pale unapohisi bidhaa yako inafahamika basi ni wakati wa kuzidisha matangazo!
 
Wanasema bora ujumbe Umefika 😂😂.
Haipendezi kwa kweli.
 
Watabisha tu ila kweli ile kazi wabongo wangefanya...
 
Hebu tafuta bajeti ya salt au movie yoyote ya Hollywood unayoijua,uone Kama Kuna movie ya maana inayopingua bajeti dola 30m,muigizaji anapewa chake kabisa,hakuna mkopo,ndiyo huwa wanatafutwa investors...na kwa Hollywood wapo tu
Wee jamaa inatosha umetudanganya vya kutosha
 
Yule" mbongo star"wa milima Kilimanjaro uko Arusha et al ndio watengeneze Royal tour documentary ya quality 😂😂....What a joke!!!!
 
Kwani nani anajuwa ubora wa Dr Vicencia Shule? Beauty is in the eyes of the beholder.

Hayo ni mawazo yake tu. Kwani ni lini movie/ film ilipendwa na watu wote? Kila mtu ana namna anavyovutiwa, waache waliovutiwa waje watembelee Tanzania ndiyo Vicencia aje asome comments zake
 
Royal Tour hakuna editing ya Marangi rangi Kama bongo Movie so hapo wabongo ndo Mama kawapiga gori la kisigino if ingekuwa tofatuti hii Filamu Ni kwa intellectual tu.
 
Royal Tour hakuna editing ya Marangi rangi Kama bongo Movie so hapo wabongo ndo Mama kawapiga gori la kisigino if ingekuwa tofatuti hii Filamu Ni kwa intellectual tu.
Mhaya kama mhaya... Labda intellectuals wa kaitaba na ijuganyundo
 
Kama Dr Vicencia Shule hajaielewa ajuwe kuwa yeye siyo target audience. Aendele na kazi zake zinazomupa shibe.

Peter Greenberg hajaanza kuandika na kushoot royal tour ya Tanzania, hiyo ndiyo layout yake kadri director alivyoiandika, Soma hapa;

"He also produces and hosts a television series called The Royal Tour which airs on PBS. The series features various heads of state giving Greenberg and viewers a personal tour of their country. It has featured a number of world leaders including New Zealand's Helen Clark, Israel's Benjamin Netanyahu, Abdullah II of Jordan, Peru's Alejandro Toledo, Mexico's Felipe Calderón, Rwanda's Paul Kagame, Poland's Mateusz Morawiecki and Tanzania's Samia Suluhu Hassan. Greenberg was previously the Travel Channel's chief correspondent."
 
Hii Nchi inahitaji Rais mwenye akili zaidi ya Nyerere na mwendawazimu zaidi ya Magufuli lasivyo hakuna chochote tuta achieve kama Nchi.
 
Hoja hapa ni ubora wa Royal tour ya Tanzania. Hata vijana wa Tanzania wangetengeneza ya kiwango hiki. Bil 11 zimepigwa na mafisadi wa Makunduchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…