Dkt. Wilbert Kleruu - Utata wa kifo chake, historia na maisha yake

Kumbe vichaa walikuwa tangu zamani?
 
MKASA MZIMA NI HUU


Kleruu alipofika Nyang’olo hakumkuta mkulima Rashid Juma. Siku hiyo ya Krismasi Rashidi Juma alipata habari, kuwa kuna ng’ombe wake walipotelea milimani. Alikwenda huko milimani kusaka ng’ombe wake. Hivyo, Kleruu akafunga safari kurudi kwa target namba mbili, baba yangu Mzee Mwamwindi. Ni njia hiyo hiyo, Nyang´olo iko mbele ya ilipokuwa ngome ya mzee.”

”Basi, Kleruu akafika kwa Mzee. Baba akiwa shambani akaliona gari la Kleruu limesimama nje ya mji wake. Kisha akamwona Kleruu akitembea kumfuata shambani. Baba alihisi tu, kuwa Kleruu amekuja na shari.

Kleruu akamuuliza Mzee kwa ukali, ”Mbona mnafanya kazi leo siku ya Krismasi?” Baba akamwomba Kleruu waende wakazungumze nyumbani. Akamwambia mdogo wangu Mohammed aendelee kulima. Mzee akatangulia mbele, nyuma anamfuatia Kleruu. Kabla ya kufika kwenye nyumba yake wakayapita makaburi. Kleruu akamtamkia baba mzee Mwamwindi; Hapa ndipo unapozika mirija yako?” Alitamka hivyo huku akimtomasa tomasa mzee na kifimbo alichoshika mkononi.

Jambo hilo lilizidi kumkasirisha marehemu mzee. Akafika nyumbani kwake. Mlangoni alisimama mke wake mdogo. Inaonekana mzee alishafanya uamuzi. Jana yake alikwenda kuwinda. Hakupata mnyama. Bunduki yake moja aina ya riffle kati ya bunduki zake mbili ilikuwa bado ina risasi. Akamwambia mke wake mdogo huku Kleruu akiwa anasikia; kanichulie bunduki yangu,”
 
Habari wanajukwaa, poleni na msiba wa kupotelewa na ndugu zetu kwa ajali ya kivuko cha 'MV Nyerere'.

Niende moja kwa moja katika lengo la andiko hili.

Naomba kufahamu kiundani zaidi kisa hiki cha miaka ya 1970+, cha mkulima- Mwamwindi kumuua mkuu wa mkoa wa Iringa wakati huo- Kleruu(samahani kama nimekosea jina). Naomba kujua kiunda kisa kizima. Na zaidi nimjue huyu mwanaume aitwaye Mwamwindi ni nani hasa hadi anafikia kumuua mkuu wa mkoa na kuipeleka maiti yake kituo cha polisi yeye mwenye.

Naomba kujua kwa sababu nimesikia hii stori kwa kusimuliwa na watu tu. Na pia ni kwanini hii stori haipendwi kuongelewa na serikali au hata kufundishwa ili watu waijue.

Kwa wale wajuzi tu. Ila kwa wale wanaopenda utani naomba usome na kupita tu.

NB: Mods naomba uzi huu ubaki kama 'topic' kuu na usipachikwe sehemu nyingine ili watu wauone wengi na wenyekujua waweze kunisaidia kujua kisa hiki kiundani.
 
Kuna mzee mmoja alinisimulia story yote ilivotokea huko iringa ila siwezi kuiandika kimtiririko mzuri kwa sababu nishaanza kusahau baadhi ya vitu, ngoja waje wataalamu wa uandishi.
 
Nitaupataje mkuu? Kama unaweza kuni-connect itakuwa vema
habari ndugu.

site:jamiiforums.com "kleruu" "mwamwindi"

Ukihitaji kutafuta kitu jf fungua google kisha anza kwa kuandika hivi site:jamiiforums.com
Ikifuatiwa na keyword mbili au tatu za kitu unachohitaji. Mfano kwa hii thread yako key words ni kleruu na mwamwindi, Unapo andika hizi key word weka hii alama. ", mwanzo na mwisho wa neno

Kwa wale wajuzi tu. Ila kwa wale wanaopenda utani naomba usome na kupita tu.
Nitaupataje mkuu? Kama unaweza kuni-connect itakuwa vema
Hizo thread mbili zinajibu maswali yako yote.

KARIBU
 
Mwamwindi alikuwa shujaaa kama mkwawa, na ukiangalia na mambo yanayotokea sasa utaona usawia utawala wa kitanzania hasa wa nyerere na jiwe hawawpendi matajiri, lakini kwa kuchagua, ujamaa , kleruu , mchaga unasukumwa kwa nguvu iringa, lakini kilimanjarona moshi waliachwa, walahakuna hatakijiji, hakuna tofauti kina cchotokea na akina rostam leo, huyu sawa , huyu funga, huyu weka ndani, huyu kanipigia kura muacheni. Lazima tupinganena utawala wa aina hii
 
Mzee Said Mwamwindi katika miaka ya mwanzo ya 1970 alimuua Mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Kleruu ambaye alikuwa akitumia madaraka ya ofisi yake kunyanyasa wananchi.

Kwa wakati ule alishtakiwa kwa mauaji na kuhukumiwa kunyongwa kama muuaji.

Lakini ni kama Solomon Mahlangu aliyehukumiwa na mahakama ya makaburu kwa hatia ya ugaidi na uhaini anavyo onekana Leo shujaa na mpigania uhuru, kwanini na sisi tusimtangaze Mzee Said Mwamwindi kama shujaa na mpigania haki dhidi ya watumia ofisi vibaya dhidi ya Wananchi?

Maana baada ya tukio lile tabia za ma RC na ma DC zilibadilika na kuheshimu sheria na katiba hadi kilipo ingia madarakani kizazi hiki kisicho soma historia.

SAID MWAMWINDI NI SHUJAA


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nasikia jamaa alimuua kisha akamtia ndani ya gari na kumpitisha kwa wake zake wote kabla ya kumpeleka moja kwa moja kituo cha polisi.

Alipomfikisha akawaambia askari polisi, "mtu wenu yule pale"

Hapo ndiyo unajua jamaa alichoka kwa dhati mateso na uonevu wa kipindi hicho.
Tofauti na hawa wenzetu wa leo wanakesha Twita wakitype nyuma ya batani za simu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…