Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World

Dodoma: Bunge lapitisha azimio la kuunga mkono mkataba wa Tanzania na DP World

Mwita Chacha anapendekeza Raisi apewe heshima ya kuitwa mama wa taifa rasmi na kikatiba. Ndo raisi wa kwanza kuleta mkataba kujadiliwa bungeni na hadharani hata Nyerere hakulifanya, mimi na muunga mkono. Mama apewe heshima
Rais wa kwanza kuleta mikataba ijadiliwe hadharani [emoji123][emoji123][emoji123][emoji7][emoji7]

#MamaKaja
#MamaAnaupigaMwingi[emoji7]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mwl Nyerere aliwahi kusema huko nyuma kwamba , nanukuu "ANAYEKULA NYAMA YA MTU HAACHI" Mwisho wa kunukuu , kwa tafsiri pana maana ya usemi huu wa Nyerere ni kama ile methali ya wahenga iliyosema MAZOEA HUJENGA TABIA

Kwamba ukizoea kufanya jambo fulani basi utaendelea tu kulifanya hata kama ni baya , ili mradi wewe binafsi au familia yako inafaidika .

Bandari zetu wamepewa Waarabu kibwege kabisa kwa vile tu wenye mamlaka wameamua kuigawa ili wao wafaidike , nakuhakikishieni kwamba hakuta kuwa na ufanisi wowote ule , NIPO HAPA JF NIMEKAA , Yaani tunauza mali zetu kwa ajili ya uvivu tu wa kazi na fikra , yaani tunaamini tu kwamba hatuwezi , ila wanaoweza ni waarabu ! Poor Tanzania !

Tumesahau ya NET GROUP , ATCL , TRL , TTCL na hata RICHMOND , tulitumia nguvu kubwa kushawishi na kudanganya umma kwamba kutakuwa na Tija , leo kiko wapi ?

Haya mmeuza Bandari kwa watu wenu ni Shirika lipi lingine mnafuatia kuliuza ili tujiandae ?

Nakulilia Tanzania .

View attachment 2652644
Bunge nalo liuzwe tu limeshindwa kujiendesha
 
Issue hii haikomei hapa, hao wabunge walipewa mlungula, wale wafurahi na familia zao. Lakini hamtakuwa na amani.
yajayo yanafurahisha
 
Tatizo ndio liko hapo. WAMESHINDWA (hawa wavivu wa kufikiria)! lakini hawataki kutoka.

Sasa kwakua WAMESHINDWA, wanataka kutumaminisha kwamba NCHI imeshindwa

Jiulize, kama wameshindwa kuisimamia na kuiendsha Bandari kwa ufanisi wa kiwango cha juu?

Wataweza: Kusimamia na kuendesha SGR kwa ufanisi hata wa wastani? - hiyvo watakodisha?
Wataweza: Kusimamia na kuendesha TTCL, ATC, TANESCO etc kufikia kupata faida? - hivyo watakodisha?
etc
Mh.Rais SSH anakua wa kwanza kuruhusu mjadala wa mikataba bungeni.....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Kwa hizi kauli zake hapa mwisho basi hili bunge ni takataka tu.

Eti bunge ni la CCM na hakuna mbunge anaeweza kupinga hoja ya mama samia?

Hili bunge ni takataka kabisa.
Sasa kama UPINZANI ni dhaifu bungeni unategemea nini ?!!!

Hata huko kwenye demokrasia....watawala wanatamani kuwa na wabunge wengi bungeni......[emoji1787]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom