Dodoma kama Ulaya, Stendi mpya kama airport yashika namba 1 Tanzania, ina Kanisa na Msikiti

Dodoma kama Ulaya, Stendi mpya kama airport yashika namba 1 Tanzania, ina Kanisa na Msikiti

Hizi ndizo tunaita sifa za kijinga! Naona umedandia treni kwa mbele nisaidie chanzo cha habari kuwa ktk nchi a afrika mashariki, TZ, inaongoza kwenye inclusive economy!!
Naona unateseka, yeye kashasema hakuna kama hiyo au kufikia hiyo wewe unaepinga ndio ulete sasa hiko chanzo kinachoonesha nchi fulani kuna stand kubwa au ulete picha ya stand na utuambie hii ipo inchi fulan, sasa ukimwambia yeye ndio alete chanzo kinachoonesha hakuna kama hii hapo itakua una matatizo kidogo ktk lugha yetu ya Kiswahili itakua huijui vizuri.

Kwasababu haiwezekani wewe ndie unaepinga halafu yeye ndio akujibie hoja yako ya kupinga uliona wapi? Acha bla bla yeye kasema hakuna kama hiyo ukanda huu na Mimi nakubaliana na hilo, wewe unaepinga sasa sema zipo au ipo na lete na picha hapo tutajua kama kweli ipo au zipo.
 
hawa hawakosekani kama Kunyaland ingejenga vituo kama hivi kabla yetu ungewaona humu wakikosoa!
Ndio tatizo la hawa maroporopo, ingekua ni kwa wengine wangemuabudu huyo kiongozi wa hilo Taifa kama mungu wao.
 
Hizo nchi za wenzetu hizo stendi zao zina sadifu na hali ya maisha ya wananchi wao!!! Sifa za kijinga, wewe mwananchi wa kawaida inakusaidia nini hata iwe ya kwanza duniani, wakati ukienda hospital hata dawa za muhimu tu hakuna?!! Wenzako ulaya karibia kila kitu kiko sawa, mfano kwa mtu wa chini aliyeshindwa kupanda ndege kipindi fast jet zipo, nauli hata kwenda mwanza mtu angeweza kulipa 80,000!!!,asahau kabisa kupanda ndege, hizo zilizoletwa kwa mbwembwe, mgonga ulimbo gani anayeweza kuzipanda?!! Hilo daraja la tazara ukiangalia unafuu wake kwa watumiaji wanaotoka barabara ya Mandela bado ni mdogo mnooo!!! Ukilinganisha na tambo zilizokuwa zikitolewa na viongozi!!!
Hivi wewe ushawahi toka hata nje ya Tanzania. Ulaya maisha ya waty wengi mabovu tu ysiongope kuona yale ma flyover na magorofa. angalia wazungu na wachina walivyojazana Afrika wakisaka maisha.
 
Sema hapo ndiyo kwenye shida.usafi usafi ni janga kubwa bongo.nashauri wangebinafsisha hivyo vyoo labda inaweza saidia.maana huyo jamaa anayekula ugali na samaki baada ya wiki mbili tatu akirudi hapo na samaki wake ataweza dhani samaki ameoza
Ni shida kaka wabongo hatuna nature ya usafi ukicompare na wanyarwanda .watanzania tunayo nature ya uchafu.ambachi kingetusaidia ni bylaws kali za kutushurutisha .hata usafi wa makonda dar naona kashagive up. Usafi wa mwisho wa mwezi ni ndoto ya masika
 
Kwani kama serikali imeweza kugaramia fedha nyingi katika miundombinu ya majengo uju

Kweli ubinadamu kazi, nadhani mtazamo wako upo katika kuangalia mapungufu tu, na wala hakuna mtu aliyekataa kwamba hakuna changamoto kama unavyodai, lakini utambue hata hizi hatua serikali inazofanya zilikua ni changamoto pia ambazo zilikua ni kero kwa wananchi.

Nitakushangaa kama unapinga serkali kujenga vituo vya afya takribani nchi nzima eti kisa hakuna madawa na watumishi kama unavyodai, lazima utambue hilo lilikua tatizo ambalo ushukuru serikali imeliona na imechukua hatua, na pia nahamini bahada ya kumaliza ujenzi wa vituo vya afya hatua inayofuata ni ununuzi wa vifaa, madawa na kuajiri wahudumu wa afya na lazima ujue kila kitu kinakwenda kwa hatua ukizingatia nchi yetu bado ina changamoto nyingi.

Mwisho lazima ujifunze kueshimu mawazo na hisia za watu wengine, kwani inaonekana imekukera kuona watu wengine wanafurahia mradi huu wa standi na ukadhani kwa kua wameona ni jambo nzuri ukajua labda hawajui kwamba kwenye hii nchi kuna changamoto nyingine, lakini kumbe ni hulka ya binadamu wanaojitambua kama mtu, tasisi au serikali imefanya jambo nzuri basi nilazima tuwapongeze kwa jambo walilofanya, ukizingatia Dodoma ndio makao makuu ya nchi lakini kulikua hakuna standi ya mahana ilikua ni aibu kubwa kwa makao makuu ya nchi kukosa hata standi ya mabasi
Nadhani unatumia nguvu nyingi kumuelezea mtu ambaye anajitambua ila anafanya kusudi tu kwa ajili ya itikadi yake, tumeshawazoea hao ndio maana wakianza kutumia huduma walizoziponda wanapigwa picha ili waumbuke
 
Hii ingepelekwa kwenye jukwaa zenu huko maana haina uhusiano wowote na Kenya. Jukwaa la mapenzi ingekuwa bora zaidi.
Leo koo limekukauka subiri nikuletee maji ulainishe koo, ili uanze kutiririka [emoji2][emoji2][emoji2]
 
Ipe miezi 3 Halafu nenda kaangalia vyoo na viti
Mkuu siku hizi kidogo tunaanza kuelewa labda baada ya miezi sita labda, kwa Dodoma naona kuna ustaarabu si Sawa na Dar ndio maana nikaweka neno labda
 
Stendi hii ingekuwa mojawapo wa Hospitali za Rufaa za wilaya au mikoa zinazotoa huduma masaa 24 zikiwa na vifaa tiba vya kisasa vingi, madawa na wafanyakazi wa kutosha wa sekta ya afya nadhani ingependeza zaidi.

Sielewi kwanini wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na Halmashauri za miji / town councils wakaamua kutumia fedha nyingi ktk ujenzi wa stendi kila kona ya Tanzania badala ya kuanza na mahospitali.

Labda sera ya Maendeleo ya Vitu vya CCM Mpya ni kipaumbele zaidi ya Maendeleo ya Watu ktk kupata huduma bora za matibabu ili waendelee kuchapa kazi .
Shida ya CCM na uongozi wake hawajui ku set vipaumbele vinavyogusa uchumi wa mwananchi mjamja ndio maana hata wafanye vipi hawawezi kupendwa na hawana hoja bila polisi hamna kitu.

Unashangaa wako busy na mamiradi ambayo hata hayana impacts yoyote kwa mtu wa kawaida ila sifa za kupigia picha eti wafanane na ulaya sijui inasaidia nini zaidi ya kuwa ni matumizi mabaya ya rasilimali.Nchi nzima wamekomaa na mastendi na masoko tena ya gharama kubwa,yenye maghorofa nknk wakati sera ya kumtua mama ndoo inasua sua,hospitali na madawa kila kata na zahanati hakuna,watoto wamerundikana kwenye madarasa kama wako zizini na wamama wanalala zaidi ya 1 kwenye vyumba vya kujifungulia,barabara za vijijini ni shida na wao ni mashahidi kila kwa kilio cha wabunge huko Dodoma.

Ukienda huko kijijini unakuta umeme wa umefika lakini wananchi walio na uwezo kuunga ni shida maana hali yao ni mbaya kiuchumi sas huu uchumi wa miradi mikubwa wanini? Nakupa mfano mdogo nilimsikia waziri wa nishati anasema uwezo wa mkoa wa kigoma ni kutumia mg 15 tu lakini wanajenga kituo cha kufua umememe mg 100 hata yeye akawauliza wananchi maumeme yote haya watayapeleka wapi?

Ndio maana huwa sikubalianai na aina ya miradi ya CCM na timing yake, huwezi target umeme wa mg 10,000 ukaweka resources huko wakati hata mg 1600 za sasa ni excess, huwezi jenga SGR za matilioni afu zitabaki kuwa iddle kisa tu unataka ufanane na wa ulaya,hii sio sawa tunaelekea njia ya Ethiopia kwenye uchumi. Kuna shida mahali tusubiri mda utasema.
 
Gharama za mastendi ni kubwa mno kuli
Kati ya hospitali na stendi zipi zimejengwa zaidi awamu hii?
Pesa iliyokuwa ommitted kwenye mastendi na miradi ya dizaini hiyo kwa lugha ya miradi ya kimkakati ni nyingi sana kuliko iliyopelekwa kwenye vituo vya afya, complications kwenye stend na gharama kubwa hivyo ni za nini? watu wajifunze optimal allocations of resources.

Siku hizi kumezuka wizi mpya wa kutoza watu pesa kuingia stend au kuzuia malori kuingia mjini kwamba ukitaka kuingia mjini ulipe pesa,logic ya kitu hiki ni nini hasa?
 
Shida ya CCM na uongozi wake hawajui ku set vipaombele vinavyogusa uchumi wa mwananchi mjamja ndio maana hata wafanye vipi hawawezi kupendwa na hawana hoja bila polisi hamna kitu.

Unashangaa wako busy na mamiradi ambayo hata hayana impacts yoyote kwa mtu wa kawaida ila sifa za kupigia picha eti wafanane na ulaya sijui inasaidia nini zaidi ya kuwa ni matumizi mabaya ya rasilimali.Nchi nzima wamekomaa na mastendi na masoko tena ya gharama kubwa,yenye maghorofa nknk wakati sera ya kumtua mama ndoo inasua sua,hospitali na madawa kila kata na zahanati hakuna,watoto wamerundikana kwenye madarasa kama wako zizini na wamama wanalala zaidi ya 1 kwenye vyumba vya kujifungulia,barabara za vijijini ni shida na wao ni mashahidi kila kwa kilio cha wabunge huko Dodoma.

Ukienda huko kijijini unakuta umeme wa umefika lakini wananchi walio na uwezo kuunga ni shida maana hali yao ni mbaya kiuchumi sas huu uchumi wa miradi mikubwa wanini? Nakupa mfano mdogo nilimsikia waziri wa nishati anasema uwezo wa mkoa wa kigoma ni kutumia mg 15 tu lakini wanajenga kituo cha kufua umememe mg 100 hata yeye akawauliza wananchi maumeme yote haya watayapeleka wapi?

Ndio maana huwa sikubalianai na aina ya miradi ya ccm na timing yake,huwezi target umeme wa mg 10,000 ukaweka resources huko wakati hata mg 1600 za sasa ni excess, huwezi jenga SGR za matilioni afu zitabaki kuwa iddle kisa tu unataka ufanane na wa ulaya,hii sio sawa tunaelekea njia ya Ethiopia kwenye uchumi.

Kuna shida mahalitusubiri mda utasema
Chadema oyeee, tushawazoe Kwa sera za chadema hata barabara za rami zisingejengwa na ndio maana kina halima mdee walipinga kujenga barabara hata jimboni kwake Kwa kua haina faida Kwa mtu mmoja mmoja.
 
Tutasikia Mengi Sana
Ccm Hoyee!!!
Kosea Kuoa Ila Siyo Kuchagua
 
Chadema oyeee ,tushawazoe Kwa Sera za chadema hata barabara za rami zisingejengwa na ndio maana kina halima mdee walipinga kujenga barabara hata jimboni kwake Kwa kua haina faida Kwa mtu mmoja mmoja
Jana mkuu anapita kwenye tren watu wanalilia maji na shule ikabidi aanzishe harambee kuchangisha pesa. Mjifunze vipaombele vya kumsaidia mwananchi hamjengi hayo kwa faida ya mbuzi na muache miradi ya show off, sasa barabara ya lami ya nini kama hakuna hospital. Unakuta barabara zikijengewa mitaro zinapitika saafi lakini mnataka kuweka lami wakati hakuna maji nk nk sasa watu wawaeleweje.
 
Nyie mnavyotuletea humu hiyo miradi yenu ya bypass sisi tukae kimya? Na bado, tegemea projects zote zitakazokamilika tutaleta humu mzee baba.
Pelekeni huko kwenu. Sisi miradi zetu hatuziposti kwenye jukwaa zenu sasa mbona mnatuletea upupu wenu huku? Ama ni inferiority complex? Yaani lazima uringie jirani ndio uhisi vizuri? Grow up. Hata mods wenu naona wako immature sana. Threads kama hizi ambazo hazina uhusiano na Kenya zinastahili kugongwa na kung'olewa kabisa na kutupwa kwenye nyuzi za mapenzi na mapambo katika sekshen ya Tanzania.
 
Tuseme umetii kwa kuifananisha hiyo standi na mwanamke mrembooo hadi kuwekwa jukwaa la mapenzi huu mwaka lazima mtii niliwaambia mkabisha
Wewe shoga wa Dar siku hizi umetulia na kuchangia bila matusi. Umeanza kumature.
 
Back
Top Bottom