Dodoma, Mbeya, Mwanza na Tanga sio majiji; zirudishwe kuwa halmashauri au manispaa

Mbeya the only issue ni Money circulation na hiyo haizuii kuwa jiji. Laumu investments na ndio ujue why watu wanalalama Serikali kuhamia Dom. Wewe umetembelea na hujaishi. Kaishi ndo urudi hapa Mwana Dar.
 
Siku narudi bongo ndio nilijua why M Jackson miguu yote hakukanyaga chini bongo mmoja ulikatalia kwa ndege akarudi USA akaakataa huku sio kabisa
Dah hv bado kuna mtu anaamini huu ujinga.? Ama kweli ww na wenzako wote ni mazumbukuku.
 
Sasa wew unaona Dar ni jiji kweli...

Angalia posta barabara zilivyo mbovu, miwaya ya umeme kila mahali, hakuna side walks, kariakoo chemba zinatema muda wote, machinga kila mahali, hakuna recreation parks, maghorofa mengi machakavu nk nk

Yaan Bado tunasafari ndefu kama nchi...tofauti ya dar na mwanza labda maghorofa tu na ukubwa wa mji lakin mengine yote yale yale

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Arusha Umeiacha Kwa kigezo kipi!
Upuuzi mtupu
 
Siku narudi bongo ndio nilijua why M Jackson miguu yote hakukanyaga chini bongo mmoja ulikatalia kwa ndege akarudi USA akaakataa huku sio kabisa
...Achana na Stori za Vijiweni zisizo na Ukweli za Kujidhalilisha Nchi Yako!
Hii ñi Stori ya Kijiweni.
Nani alikuambia MJ aliwahi kuja hapa na akakatalia ndani ya Ndege??
Punguza kukaa Vijiweni!
 
Kuna sehemu nyumba zimesambaa kama takataka Tanzania hii kama Dar

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna rafiki yangu alisafiri kwenda S.A alipofika kule siku ya kwanza kuoga akakutana na "shower gel" Basi akaoga alivyomaliza kuangalia chini akakuta mabaki kabaao ya taka kwenye tiles[emoji16][emoji16]alitoka huku bongo alijiona msaaaaaafi mwenyewe na alikuwa maji ya kunde Fulani ya kung'aa.

Alikaa S.A week mbili halfu akaenda USA huko sasa alikaa Miaka miwili aliporudi bongo alifurahi sana ila alikuwa mweupe mnoo,yaani kaivaaa[emoji16]..Aliniambia wewe utarudi mzungu ukienda huko[emoji16][emoji16]ila hakuacha kunisimulia miyeyusho ya watu weupe yaani[emoji21][emoji21]

Ulaya ni ulaya TU ila HOME SWEET HOME..huyo rafiki yangu alikubali kuwa Tanzania NI kuzuri na kutamu mno ukiwa na mkwanja,anatafuta pesa huko anakuja kutumia bongo na investment zake anafanyia huku ili siku moja arudi kwao aishi kwa furaha na amani,LAKINI KWANZA PESA,TUTAFUTE PESA VIJANA WENZANGU NCHI TAMU HII[emoji16]
 
Je ukisafiri kutoka dubai ukaenda Switzerland au New York utapaona pabaya? Standard ni standard tu. Hayo sio majiji.
 
🤣

Kuna mswahili alienda USA halafu alivyorudi Dar. Akasema anasikia kama Dar ina harufu fulani mbaya anaisikia kila anakopita 🤣🤣🤣
Huu ni ukweli. Safari fulani nilikuwa natoka uswisi na nilisikitika sana niliporudi na kutambua kwamba nchi yangu ni chafu sana.

Pia kuna wakati nilienda Bangkok Thailand na nikaona ile nchi ina harufu fulani kila sehemu ambayo sikuipenda kabisa.
 
Kila nchi hua na vigezi vya sehemu kua na hadhi fulani, ndio maana manispaa iliyoko Malawi kwa Tz ni halmashauri ya mji pia umetumia kigezo cha makazi holela kuondoa uhalali wa majiji tajwa hapo juu labda nikuulize hivi ukiondoa Mbeya ni mji gani wenye makazi holela kuizidi Dar ? 70% ya makazi yapo kiholela, pia Dar ilipopewa hadhi ya jiji ulikua ni mji duni sasa kuliko miji uliyotaja inavyoonekana leo je wahusika walikosea kuipa hadhi ya jiji ?,kwa vigezo unavyovitaka tuviongeze hata Dar itakosa hadhi ya jiji
 
Inategemea ni mkoani wapi, mfano mji wa Arusha una mazingira mazuri kuliko Dar hali ya hewa nzuri, kijani kibichi
 
Upandishaji wa majiji uliwekewa vigezo, ila vigezo vya kisiasa pia vilikuwepo ila havikuwekwa wazi ulikuwa under the capet. Usishangae unachokiona kwenye majiji hayo uliyoyataja kwani hii ni TZ. Makazi ya watu zamezidi uwezo wa serikali kupanga and kuwaletea wananchi huduma stahiki kwa wakazi wa majiji hayo. Mikoa ilipigania miji yao kuwa majiji kwani mgao wa keki ya Tiafa ni kubwa kuliko kwa halmashauri na manispaa. But, kiini cha yote haya ni Serikali kuu kukumbatia kila kitu na kutokuwapa nguvu mikoa/miji kujiendeleza bila kuingiliwa na serikali kuu. Serikali kuu imeingilia mapato yote ya miji yote na kuyakusanyia mfuko mmoja ambao kwa sasa huitwa mfuko wa Rais alie madarakani, kuanza kugawa kwa hisani na sio kufuata budget ilivyopangwa na basically on political grounds/personal.
 
Kama ni hivyo basi tuambie, hivi Tz kuna jiji?....ikiwa unatumia vigezo ulivyotaja, hatuna majiji tuna mazizi.
 
Ni kweli kabisa vigezo vilivyotumika ni vya kisiasa zaidi. Mahali panaitwa jiji lakini ardhi katikati ya hilo jiji haijapimwa na makazi ni holela.

Miundombinu ya barabara, maji safi na taka na usafi wa mazingira ni hatarishi kabisa. Yaani hizi ni halmashauri tupu, hakuna jiji hapa.
 
Inategemea ni mkoani wapi, mfano mji wa Arusha una mazingira mazuri kuliko Dar hali ya hewa nzuri, kijani kibichi
Arusha nilikaa 2011 na huwa napita mara kadhaa na ninakubaliana na wewe kwamba mandhari ya arusha inazidiwa na dar peke yake katika nchi hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…