DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

Hell no
Naomba hizi taarifa za Kifo nilizozisikia sasa hivi zisiwe za kweli....sitaki hata kuandika. MUNGU Baba naomba tenda muujiza wako leo hii tukakuone.
please
 
Unaibua ishu na kusimama mwenyewe ili watu wakuone wewe ndie mpiganaji pekee uliebaki ndani ya chama,
Unafanya press conference kipekee² bila kuifanya kuwa ya kichama na hivyo kujipatia nafas ya kujijenga mwenyewe ndani ya chama:-
Unataka kuwa Chairman wa chama ajaye?
Unategemea nn kitokee km si kukupoteza ktk nyakati ambazo ni rahis kuisingizia serikali..
 
Roho imeniuma kama vile ni mzazi wangu..!!
Ila ukweli utabaki ukweli ..
Time wil speak out..
 
Fursa ya kuuza vioo vya magari ambavyo ni bullet proof.. wtanzania tulipofikia ndo hapa tukijifanya bado hatuoni itakua tunaendeleza africa kua dark continent.. [HASHTAG]#enlighten[/HASHTAG]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu Baba wa mbinguni, pengine naweza kuwa sistahili mbele zako kuleta maombi haya kwako kutokana na mapungufu yangu, lakini katika hili Baba Mungu nakuomba usiyatizame mapungufu yangu bali ukusikie kuomba kwangu.

Mungu mwenye enzi Mungu mkuu, Tia mkono wako juu ya kiumbe wako huyu Tundu Lissu kama ulivyomuinua mwanao baada ya shetani kushindwa, Mungu baba wafanye mashetani haya yashindwe vile vile kama yalivyoshindwa kwa mwanao mpendwa Yesu Kristu.

Tundu Lissu amekuwa akiifanya kazi yako kwa kuwakemea mafalisayo na wakuu wa sheria bila woga kama alivyofanya mwanao mpendwa, Baba usiruhusu washinde bali uwaoneshe kwamba huyu anaifanya kazi inayokupendeza wewe na kwamba saa yake haijafika ya kumuondoa kwenye kazi yake uliyompa kwa ajili yetu.
Mpe uzima mpe uponyaji wako ili wapate kujua kuwa shetani hana mamlaka juu ya kiumbe wako hata kama wamemmiminia risasi zaidi ya ishirini, umemkinga Baba kwa muujiza wako maana bila hivyo hata hospitali asingefika akiwa hai kama walivyodhamiri hao shetani.

Nakutumaini Mungu maana hujawahi kuniangusha, nisikie na katika hili wapate kutambua kwamba shetani atendaye kinyume na kazi zako daima hatofanikiwa.

Ahsante Mungu Baba kwakuwa umenisikia na umenipa kibali kuyaomba haya kwako. Ni katika njia ya Yesu Kristu ninakushukuru.
Aamina.
 
Acha Ku create utetezi mkuu wa kindezi. Hamna cha vita ya uchumi wala nini, acheni kuwapa watu usafi wasiokuwa nao. This is too obvious please
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…