DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

Sir GOD anatuangalia tu wanadamu tunavyotesana...ila na yeye uvumulivu humuishaga kipindi fulani.

Tusimfikishe kwenye hicho kipindi.

Jamani usiku mwema.
Mkuu kweli nimeamini kuwa taarifa hii umeipokea kwa masikitiko makubwa hadi mida hii unaaga usiku mwema? Get well Lissu
 
Our fellow MP for
Singida East Tundu
Lissu has been shot by
unknown people. He
has been rushed to
dodoma general
hospital~~~Zitto Kabwe
Very bad news, Tunamuombea kwa Mungu apate kupona
 
Kweli mkuu naona tunataka kuwapoteza wanaotupa changamoto tunataka kuongoza vibogoyo LISSU NA KIBATALA yafaa Taifa lijivunie ajabu wanatengwa wakat wanawapa changamoto wanasheria wa serikali.

Huenda TUNAONESHWA KWAMBA NCHI YETU HAIHITAJI WATU WENYE AKILI FIKIRISHI kama si KWAMBA TUNAHITAJI MABUBUSA NA WASHANGILIAJI KILA LISEMWALO PASINA KUJALI MUSTAKABALI WA NCHI YETU KIUCHUMI NA KIMAENDELEO.

Hatupaswi kuhoji hao kina NDIO MZEE wametufikisha vipi hapa hii leo.

Yanajengwa matukio ili kutuhamisha kwenye changamoto za kiuchumi na kimaisha tulizonazo. Hayatazamwi madhara kwa matukio yanayotengenezwa wala athari zake.
Tunazidi kutundikiwa weledi na kutawaliwa na fikra za leo yetu na si kesho wala vizazi vyetu.

Ukitaka kuamini wenye akili fikirishi hawahitajiki usifikirie kwa level ya TL mfikirie aliye-innovate Vespa kwanini walimkamata badala ya kumuunga mkono katika ubunifu wake! Hapo utafahamu tunaenda wapi!!!
Wako wanaoshangilia yanayoendelea...
 
Hakuna shida kwakua wanamuita nabii hata akifa atafufuka na atapaa ataendelea kuwasaidia maana nashangaa tangu lini mbunge akaongoza nchi nzima
Kwa hiyo ndio maana mnataka kumuua? Hivi wee jamaa umeandika ukiwa na akili timamu au bangi? Na kila baya ulilomuwazia Lissu namwomba Mungu likurudie...

Mungu ndio alituumba na yeye ndie atakaekuwa na mamlaka ya kutuchukua na sio kwa nguvu za binadamu

Shame on you....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Inadaiwa Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, ajeruhiwa kwa risasi.

Kwa sasa wapo hospitali ya Mkoa, mjini Dodoma.

Ameshambuliwa kwa risasi wakati akishuka nyumbani kwake Area D Mjini Dodoma, alikuwa akitokea Bungeni na alienda Nyumbani kula chakula cha mchana.

Lissu amepigwa risasi 5, miguuni na tumboni.

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema hali ya Mbunge huyo aliye hospitalini sasa ni mbaya!


56d494001b8e52eca1b71490ff9635e4.jpg


9f94cea0e0708e5fafb57915caf1dd27.jpg

abc21fedd617180297c6247f403b7362.jpg


Updates to follow

=======

UPDATES;

=======

TAARIFA YA AWALI KUHUSU SHAMBULIO LA KUPIGWA RISASI MHE. TUNDU LISSU

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa mshtuko mkubwa taarifa ya kupigwa risasi Mwanasheria Mkuu wa Chama ambaye pia ni Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Singida Mashariki, Mhe. Tundu Antipus Lissu baada ya kikao cha Bunge mchana wa leo.

Shambulio hilo limetokea majira ya mchana nyumbani kwake Area D Dodoma na kujeruhiwa vibaya na kukimbizwa katika Hosiptali ya Mkoa wa Dodoma.

CHADEMA tunalaani vikali kitendo hicho, na tunafuatilia kwa karibu hali yake.

Taarifa zaidi zitaendelea kutolewa.

Imetolewa na Kurugenzi ya Uenezi, Mawasiliano na Mahusiano ya Nje.

CHADEMA MAKAO MAKUU

DAR ES SALAAM.

=====

Preliminary Press Statement on the incidence of Hon. Tundu Lissu being shot

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) has received with great shock the report on the shooting of the Attorney General of the Party who is also the Chief Whip of the Official Opposition in Parliament and MP of Singida East, Hon. Tundu Antipus Lissu just after a Parliamentary session today.

The attack took place at his Dodoma residence at midday and was seriously wounded and had been rushed to the Dodoma Regional Hospital.

CHADEMA strongly condemns this act, and we are following up closely on his condition.

We will continue to update as we get more information.

Issued by the Directorate of Ideology, Publicity, Communications and Foreign Relations.


My take,

Wataalamu wa forensics wazipime hizo bullets zilizo kutwa kwa mwili wa lisu na zilizokutwa kwa gari na ndio mtajua siraha iliyo tumika na mmiliki kama record za siraha ziko sahihi.

One of the very terrified mistake attempted kwa walio tumwa hii yaweza leta machafuko ndani ya nchi wakifanya mizaha kama hiyo.

Na kulichafua Taifa letu katika msingi tulio uzoea wa Amani sasa nchi itakuwa na sintofahamu ya freedom of speech tuna rudi kwenye ukoloni maomboleo.
 
Back
Top Bottom