DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

DODOMA: Tundu Lissu ajeruhiwa kwa risasi, akimbizwa Hospitali

Hivi watu wasiojulikana ni pamoja na walioingia clouds wakamkata mtama sudy na kwisa. Na wengine niwale walimnyooshea bunduki nape hadharani??. Watu wasiojulikana hivi huwa wanakaa wapi? Hata mimi sijulikani
Mwenye macho haambiwi tazama
 
Mbona sielewi kule wanasema anapelekwa Muhimbili huku mnasema anapelekwa Nairobi mbona taarifa zinakingana
 
Sijawahi kuona Lissu akiwasilisha hoja kwa interest zake, hakika ni mtetezi wa wanyonge anayehitaji sala zetu. Uhai wake ni muhimu sana katika Taifa hili, hivyo kila tunapolitaja jina la Mungu wetu tusisahau kumwombea kwani ni yeye Mungu ndiye anatupa pumzi.
 
Lissu bado wanyonge wa kweli wanakuhitaji,tu nakumbuka ulipokuwa umewekwa ndani Mara nyingi na Hawa polisi wetu uliwatafuta wanyonge walioonewa na kuwekwa ndani miezi kadhaa bila kupewa haki ukawatetea bure,mungu huyu ni mtetezi wa kweli wa wanyonge tunakuomba kwa hisani yako mponye baba mungu,bado tunamuhitaji
 
Hii ni habari mbaya sana na inapaswa kukemewa na kupingwa kwa nguvu zote.
Sasa najiuliza dereva mzoefu kiasi cha kumuendesha mtu ambaye ni 'high risk' unagundua kuna gari inakufuata katika options zote unaamua kwenda nyumbani? Tena unajua ukishaingia getini ni dead end utajiteteaje kwenye incident kama hii?
Una VX V8 unahisi gari inakufuata nyuma unashindwa kukamua mashine hio unaamua kwenda nyumbani?
Mimi nikihisi gari inanifuata nyuma siingi nyumbani napitiliza.

Hata mimi haya maelezo yamenichanganya sana. Kwa kweli dereva atueleze vizuri, kwa nini aliamua kuingia nyumbani hata baada ya kugundua kuna gari linawafuatilia? Kwa nini hakurudi bungeni baada ya kugundua hilo? Na hao wauaji walipata wapi confidence ya kulifuata gari nyuma mpaka nyumbani wakati wakijua dereva angewashtukia?
 
Hii ni kitu mbaya sana.INACHAFUA TASWIRA YA NCHI YETU na HESHIMA TULIYOJIJENGEA NDANI NA NJE YA NCHI na PIA ni kiashiria cha uvunjifu wa AMANI kwenye nchi yetu mnayoimbanua kuwa ni KISIWA cha AMANI.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mahakama msimwachie huyo eti kwa sababu mgonjwa. Siku ya kesi yake ni lazima aitwe tu, kama Manji na Seth.
 
Back
Top Bottom