Does Africa have its own (unique) definition of democracy?

Does Africa have its own (unique) definition of democracy?

Juzi nilikuwa namsikiliza mhe. Hamad mwenyekiti wa ADC akawa anasema Marekani pamoja na demokrasia yao hawaruhusu mtu kuanzisha chama cha kikomunisti, vile vile china nao hawaruhusu kuanzisha chama cha kibepari.
Mathalani Tanzania tuna vyama vya siasa 20+ wakati Marekani wao wanavyo vichache.
Kuja na single definition ya demokrasia ni ngumu kulingana na mazingira husika, pengine labda ifanyike 'rating score' yenye vipengele tofauti tofauti ili kupata walau namna fulani ya kuipima hiyo demokrasia.
Jamaa alichambua vizur sana mpaka nikawa nawaza kwann wanasiasa wetu wasiyachukue yale mambo aliyo kuwa akiyazungumza na wayaishi kwa maslahi mapana ya taifa letu
 
Jibu ni NDIYO

Maana ya jambo kama falsafa, mfumo au itikadi unaweza kuipata kwa

1. Kuambiwa

Hii ni ni kama tulivyoambiwa na kuaminishwa kupitia mifumo yan kisiasa na kielimu kuwa demokrasia ni nini

2. Kutengeneza maana binafsi

Hii unaipata kutokana na jinsi unavyokiona kitu husika kwa mfano, kuna anayeamni demokrasia ni mtego tu tuliowekewa na watu ili uwanufaishe wao kwa kupitia milango ya nyuma na hauna maana nzuri kwa hali halisi tuliyonayo waafrika.

3. Kitu kma kilivyo

Hii inaweza isiingie kwenye hiyo milengo mingine, kwa maana kwamba siyo kile unachoamabiwa au anachoshinikizwa kuamini au unachoamini wewe mwenyewe lakini ndo uhalisia wa mambo

KUHUSU AFRICA, SI TU KWAMBA TUNA MAANA YETU YA DEMOKRASIA BALI TUNAPASWA TUWE NA MAANA YETU JUU YA JAMBO HILI MTAMBUKA.


Demokrasia tuliyoletewa na hao wageni ina maambo mengi lakini kwa haraka haraka makubwa ni kama vile

A. Uchaguzi huru na haki
B. Uchaguzi kufanyika kila baada ya kipindi filani
C. Mfumo wa vyama vingi
D. Uhuru wa kusema/ uhuru wa maoni
E. Kuheshimu haki za binadamu


Sasa the issue is hayo mambo yote pengine ni mazuri, lakini wanaotetea demokrasia bila kuangalia kwa undani wanayachukua yalivyo (they take ghem for granted)

Mfano mzuri, demokrsaia inataka vyama vingi lakini kuna tija gani kuwa na utitiri wa vyama vya siasa? Vyama vipo vingi ni sawa lakini, je ni vyote vina nguvu? Jibu ni hapana mfano hai kwa mazingira yetu vyama vya upinzani ni vingi vidogo vidogo kiasi kwamba havina nguvu ya kutoshana ubavu na chama tawala, kwa hiyo hapo takwa la demkokrasia limetimizwa lakini halina tija

Kuna uhuru wa kusema ni jambo jema, lakini ni vipi huo uhuru unapopitiliza mipaka? Kuna wapinzani wao wanachojua ni kusema al mradi wapinge tu. Mwanagenzi mmoja humu aliwahi kusema upinzani ni kama imani hivyo hata serikali ifanye mazuri vipi, ukiwa mpinzani kazi yako ni kupinga. Hili pia ni tatizo, kitu kikiwa kizuri kinaonekana na mpinzani anayepinga kila kitu ataonekana hafai, ukienda mbali kwenye hili, inafikia mahali mpinzani anapinga hadi anafikia hatua ya kuhatarisha uwepo wa mambo mazuri. Chukulia mpinzani anayeshabikia mali za nchi/ umma kusikiliwa na wadeni al mradi aonekane yuko tofauti unamchukuliaje, hapo uzalendo uko wapi? Mtu kama huyo akipewa mpango mbaya kuihujumu serikali ili ionekane haifai atasita kuutekeleza? Na serikali inapohujumiwa hasara ni kwa nani, kama sio kwa umma?Ni vizuri uwepo uhuru wa kusema lakini kuwe na mipaka fulani sio kusema sema tu hata kama unaharibu.

Bila kuficha haya mambo tunapandikiziwa ili yatuvuruge tu, Afrika inahitaji kuwa namna yake ya demokrasia sio kuiga au kufuata tu tunayoaminishwa na jumuiya za kimataifa kwani hata wao kuna vitu vikifikia hatua fulani demokrasia yao hiyo hiyo wanaiweka pembeni mfano mzuri Marekani na Umoja wa Ulaya ziliilaumu sana Libya wakati wa maandamano yaliyopelekea machafuko na kisha kupinduliwa Ghadaffi kwamba serikali ya Libya ilkuwa inavunja haki za binadamu kwa kutumia nguvu kuzuia maandamano hadi ikafikia kupeleka majeshi ya NATO na wakafanikiwa kuung'oa utawala uliokuwepo lakini juzi hapa Marekani yenyewe imefanya vitendo vilevile dhidi ya waandamanaji na hali ni kimyaaa hakuna anayekohoa dhidi ya huyo baba na mtetezi maahuhuri wa demokrasia. Sasa hapo kama una akili pima uone,wao wakifanya hakuna shida sisi tukifanya tunaambiwa ni kinyume na demokrasia.


Kuna takwa la viongozi kupokezana madaraka, ni zuri tena sana lakini demokrasia hiyo hyo inasema sauti ya wengi ndiyo iamue, kwa mafano katiba zinaeleza mihula ya urais lakini demokrasia hiyohiyo inasema hata hiyo katiba inaweza kubadilishwa kwa sauti za wengi. Ni sawa kuna mihula ya urahisi inayoruhusiwa kikatiba lakini katiba ni yetu ipo kutusaidia na sisi ndo tunaoitengeneza vilevile sisi ndio wenye nguvu ya kusema kifungu fulani hapa tusikitumie na tuakakibadilisha kwa kufuata taratibu zote, tukikubaliana ni sawa maana sauti ya wengi ndiyo mwamuzi. Ajabu sauti ya engi kwenye hili jambo wenzetu hawapendi kulisikia, mi nadhani ni sahihi tu rais kama anakubalika na watu wake na wamekubali kutengeneza katiba yao hivyo, akae tu bila kujali ni muda gani ali mradi katiba imetengenezwa na wanachi na imefuata utaratibu halali. Mfano wa hili juzi tu hapa wananchi wa Urusi wameridhia mabadiliko ya katiba ya kumruhusu Putin kuongoza hadi 2036 ikiwa aataendelea kugombea na kushinda, lakini kwa sababu ni Ulaya hutasikia chokochoko, tatizo ni Afrika tukiamua mambo kama hivyo lazima tukosolewe, wanasiasa wetu wachochewe upuuzi na wao bila kujitambua wanafuata tu bila kujua kuwa wanacheza mdundo wa mabeberu ambao daima wanataka loopholes kama hizo za kubadili badili viongoli ili wapenyeze viongozi "wazuri kwao."


Pamoja na yote hayo simaanishi kuwa hawapo viongozi wa kiafrika au serikali za kiafrika zinazoharibu au zinazoenda kinyume na ustawi mzuri wa wananchi wao, zipo kabisa na hao kweli wanapaswa kurekebisha ili hii demokrasi inayotetewa sana iwasaidie.

Itoshe tu kusema Afrika tunahitaji demokrasia ya kipekee kwa ajili yetu, tusiingiliwe ingiliwe tu na watu wenye malengo yao binafsi dhidi yetu kwa kisingiziao cha demokrasia. Demokrasia ni nzuri kwa mambo mengi lakini tuwe na demokrasia ya kikwetu kwetu isiwe demokrasia inayoamriwa Washington na Brussels




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante sana kwa ufafanuzi wako mkuu. Je, ni sahihi kusema kwamba, Does Paul have a car?Au; Does Paul has a car?
Even though they come from the same word, there are slightdifferences in the way they're used. Have is used with I, you, we, and they, while has is used with he, she, and it. The verb to have has many different meanings. Its primary meaning is “to possess, own, hold for use, or contain.”
 
Even though they come from the same word, there are slightdifferences in the way they're used. Have is used with I, you, we, and they, while has is used with he, she, and it. The verb to have has many different meanings. Its primary meaning is “to possess, own, hold for use, or contain.”
Swali langu hili hapa;

Je, ni sahihi kusema kwamba;

Does Paul have a car? Au;

Does Paul has a car?
 
Jibu ni NDIYO

Maana ya jambo kama falsafa, mfumo au itikadi unaweza kuipata kwa

1. Kuambiwa

Hii ni ni kama tulivyoambiwa na kuaminishwa kupitia mifumo yan kisiasa na kielimu kuwa demokrasia ni nini

2. Kutengeneza maana binafsi

Hii unaipata kutokana na jinsi unavyokiona kitu husika kwa mfano, kuna anayeamni demokrasia ni mtego tu tuliowekewa na watu ili uwanufaishe wao kwa kupitia milango ya nyuma na hauna maana nzuri kwa hali halisi tuliyonayo waafrika.

3. Kitu kma kilivyo

Hii inaweza isiingie kwenye hiyo milengo mingine, kwa maana kwamba siyo kile unachoamabiwa au anachoshinikizwa kuamini au unachoamini wewe mwenyewe lakini ndo uhalisia wa mambo

KUHUSU AFRICA, SI TU KWAMBA TUNA MAANA YETU YA DEMOKRASIA BALI TUNAPASWA TUWE NA MAANA YETU JUU YA JAMBO HILI MTAMBUKA.


Demokrasia tuliyoletewa na hao wageni ina maambo mengi lakini kwa haraka haraka makubwa ni kama vile

A. Uchaguzi huru na haki
B. Uchaguzi kufanyika kila baada ya kipindi filani
C. Mfumo wa vyama vingi
D. Uhuru wa kusema/ uhuru wa maoni
E. Kuheshimu haki za binadamu


Sasa the issue is hayo mambo yote pengine ni mazuri, lakini wanaotetea demokrasia bila kuangalia kwa undani wanayachukua yalivyo (they take ghem for granted)

Mfano mzuri, demokrsaia inataka vyama vingi lakini kuna tija gani kuwa na utitiri wa vyama vya siasa? Vyama vipo vingi ni sawa lakini, je ni vyote vina nguvu? Jibu ni hapana mfano hai kwa mazingira yetu vyama vya upinzani ni vingi vidogo vidogo kiasi kwamba havina nguvu ya kutoshana ubavu na chama tawala, kwa hiyo hapo takwa la demkokrasia limetimizwa lakini halina tija

Kuna uhuru wa kusema ni jambo jema, lakini ni vipi huo uhuru unapopitiliza mipaka? Kuna wapinzani wao wanachojua ni kusema al mradi wapinge tu. Mwanagenzi mmoja humu aliwahi kusema upinzani ni kama imani hivyo hata serikali ifanye mazuri vipi, ukiwa mpinzani kazi yako ni kupinga. Hili pia ni tatizo, kitu kikiwa kizuri kinaonekana na mpinzani anayepinga kila kitu ataonekana hafai, ukienda mbali kwenye hili, inafikia mahali mpinzani anapinga hadi anafikia hatua ya kuhatarisha uwepo wa mambo mazuri. Chukulia mpinzani anayeshabikia mali za nchi/ umma kusikiliwa na wadeni al mradi aonekane yuko tofauti unamchukuliaje, hapo uzalendo uko wapi? Mtu kama huyo akipewa mpango mbaya kuihujumu serikali ili ionekane haifai atasita kuutekeleza? Na serikali inapohujumiwa hasara ni kwa nani, kama sio kwa umma?Ni vizuri uwepo uhuru wa kusema lakini kuwe na mipaka fulani sio kusema sema tu hata kama unaharibu.

Bila kuficha haya mambo tunapandikiziwa ili yatuvuruge tu, Afrika inahitaji kuwa namna yake ya demokrasia sio kuiga au kufuata tu tunayoaminishwa na jumuiya za kimataifa kwani hata wao kuna vitu vikifikia hatua fulani demokrasia yao hiyo hiyo wanaiweka pembeni mfano mzuri Marekani na Umoja wa Ulaya ziliilaumu sana Libya wakati wa maandamano yaliyopelekea machafuko na kisha kupinduliwa Ghadaffi kwamba serikali ya Libya ilkuwa inavunja haki za binadamu kwa kutumia nguvu kuzuia maandamano hadi ikafikia kupeleka majeshi ya NATO na wakafanikiwa kuung'oa utawala uliokuwepo lakini juzi hapa Marekani yenyewe imefanya vitendo vilevile dhidi ya waandamanaji na hali ni kimyaaa hakuna anayekohoa dhidi ya huyo baba na mtetezi maahuhuri wa demokrasia. Sasa hapo kama una akili pima uone,wao wakifanya hakuna shida sisi tukifanya tunaambiwa ni kinyume na demokrasia.


Kuna takwa la viongozi kupokezana madaraka, ni zuri tena sana lakini demokrasia hiyo hyo inasema sauti ya wengi ndiyo iamue, kwa mafano katiba zinaeleza mihula ya urais lakini demokrasia hiyohiyo inasema hata hiyo katiba inaweza kubadilishwa kwa sauti za wengi. Ni sawa kuna mihula ya urahisi inayoruhusiwa kikatiba lakini katiba ni yetu ipo kutusaidia na sisi ndo tunaoitengeneza vilevile sisi ndio wenye nguvu ya kusema kifungu fulani hapa tusikitumie na tuakakibadilisha kwa kufuata taratibu zote, tukikubaliana ni sawa maana sauti ya wengi ndiyo mwamuzi. Ajabu sauti ya engi kwenye hili jambo wenzetu hawapendi kulisikia, mi nadhani ni sahihi tu rais kama anakubalika na watu wake na wamekubali kutengeneza katiba yao hivyo, akae tu bila kujali ni muda gani ali mradi katiba imetengenezwa na wanachi na imefuata utaratibu halali. Mfano wa hili juzi tu hapa wananchi wa Urusi wameridhia mabadiliko ya katiba ya kumruhusu Putin kuongoza hadi 2036 ikiwa aataendelea kugombea na kushinda, lakini kwa sababu ni Ulaya hutasikia chokochoko, tatizo ni Afrika tukiamua mambo kama hivyo lazima tukosolewe, wanasiasa wetu wachochewe upuuzi na wao bila kujitambua wanafuata tu bila kujua kuwa wanacheza mdundo wa mabeberu ambao daima wanataka loopholes kama hizo za kubadili badili viongoli ili wapenyeze viongozi "wazuri kwao."


Pamoja na yote hayo simaanishi kuwa hawapo viongozi wa kiafrika au serikali za kiafrika zinazoharibu au zinazoenda kinyume na ustawi mzuri wa wananchi wao, zipo kabisa na hao kweli wanapaswa kurekebisha ili hii demokrasi inayotetewa sana iwasaidie.

Itoshe tu kusema Afrika tunahitaji demokrasia ya kipekee kwa ajili yetu, tusiingiliwe ingiliwe tu na watu wenye malengo yao binafsi dhidi yetu kwa kisingiziao cha demokrasia.
thanks mkuu@
 
Tafsiri ya demokrasia ni ile ile duniani tatizo liko kwenye kuiishi demokrasia yenyewe.Ndo maana tunapata videmokrasia vingi vingi uchwara vilivyotengenezwa na watawala kwa manufaa yao binafsi.
 
Taratibu kiongoz.... hebu tudadavue kdogo tuone kama tasfir ya demokrasi inafanana dunia nzima. Je?

Kufungia media zenye mrengo hasi na dola ni demokrasi?

Kuzuia uhuru wa kujieleza na siasa huru ni demokrasi?

Kunyima wapnzan haki ya kuishi ni demokrasi?

Kuweka sheria kali za kudhibiti mawasiliano na upashanaji habari ni demokrasi?

Uekezaji mkubwa kwenye usalama ni demokrasi?
 
Taratibu kiongoz.... hebu tudadavue kdogo tuone kama tasfir ya demokrasi inafanana dunia nzima. Je?

Kufungia media zenye mrengo hasi na dola ni demokrasi?

Kuzuia uhuru wa kujieleza na siasa huru ni demokrasi?

Kunyima wapnzan haki ya kuishi ni demokrasi?

Kuweka sheria kali za kudhibiti mawasiliano na upashanaji habari ni demokrasi?
Haya ni mawazo yako siwezi kukupinga@
 
Ninaweza kusema NDIO na HAPANA kwa wakati mmoja. Wazungu wasilazimishe utaratibu wa siasa zao ndio iwe desturi yetu.

Afrika tuna siasa zete zinazofanana na sisi, maisha pamoja na mazingira yetu.

Democracy ya mzungu ndio inaua wanawake na watoto huko Iraq, Afghanistan, Libya na Syria.
Hizo Ni chuki zako, jifunze kwanza kuhusu maana ya neno demokrasia.
Mbona haziuwi wanawake na watoto ulaya
 
Demokrasia ni uhuru wa kujiamulia mambo. Hii inategemea mazingira ya wahusika. Je Afrika tuna aina ya kipekee ya demokrasia, hapana, kila nchi inajiamulia mambo yake inavyowapendeza wananchi wachache (wanasiasa).

Kuna wanaobadili uongozi baada ya muda maalum, kama ilivyo huko Uholanzi au Marekani, kuna walioamua mtu mmoja atawale mpaka atakapoishiwa uwezo wa kutawala, kama ilivyo China ama Urusi.

Kulindana kimaslahi, kurithishana uongozi, kupo kama ilivyo popote duniani, tofauti, Afrika umma hauheshimiwi na kupewa unachotaka, pengine ni kama Marekani (electoral college vs popular votes), ila Afrika hata katiba haiheshimiwi. Je demokrasia ya Afrika ni kwa ajili ya nani? Ni kwa ajili ya wachache (wanasiasa) na maslahi yao.
 
Back
Top Bottom