Donald Trump ashinda Urais wa Marekani kwa 51.05% dhidi ya Harris Kamala aliyepata 47.46%

Donald Trump ashinda Urais wa Marekani kwa 51.05% dhidi ya Harris Kamala aliyepata 47.46%

Imetangazwa dakika chache zilizopita na vyombo vya Habari

=====

Rais wa zamani Donald Trump kutoka chama cha Republican, ameshinda Uchaguzi wa Marekani.
View attachment 3144969
Chanzo: Spectator Index

Donald Trump ameoa mara tatu, Ivana na Marla Maples, mke wa kwanza na wa pili mtawalia ambao wote ametalikiana nao. Mke wake wa sasa ni Bi Melania.

Bwana Trump ana watoto watoto watano, watatu wa kiume Donald Trump Jr, Eric, Barron na watoto wawili wa kike Ivanka na Tiffany.

Rais huyo wa Zamani wa Marekani alizaliwa Juni 14 mwaka wa 1946, mjini New York, akiwa mtoto wa tano kati ya watoto sita.

Babake Fred alikuwa tajiri aliyemilki majumba na babu zake Trump walikua wahamiaji kutoka Ujerumani.

Mamake Mary alikuwa mzaliwa wa Scotland.
View attachment 3144983
Tangu utotoni, Trump alikuwa mtundu na wazazi wake walimpeleka shule ya msingi iliyofadhiliwa na jeshi mjini New York.

Baadaye alifuzu kutoka Chuo Kikuu cha Pennsylvania, kitivo cha elimu ya biashara mwaka wa 1968.

Alifanya kazi katika kampuni ya babake ambaye aliendesha biashara ya kuuza nyumba kwa raia wa kipato cha kadiri, viungani mwa New York.

Hata hivyo Donald Trump alikuwa na ndoto ya kufanya biashara nje ya makaazi ya Queens na Brooklyn.

Aliwekeza katika biashara kubwa ya ujenzi na kuweza kujenga mojawapo ya mijengo ya kifahari zaidi nchini Marekani. Alifanikiwa kutokana na sera ya kiuchumi iliyowekwa na utawala wa Reagan miaka wa 1980.

Yapo mahoteli, viwanja vya mchezo wa gofu, makazi ya kifahari, majumba ya kamari kutoka Carlifonia hadi Mumbai nembo yake ikiwa ni Trump.

Ameandika Riwaya kadhaa kuhusu biashara, huku umaarufu wake uking'aa zaidi katika makala yanayoelezea maisha halisi, "The Apprentice," katika runinga ya NBC. Hata hivyo alitupwa nje ya makala hayo baada ya kutoa kauli zilizowakera raia wa Mexico.
SHIT HOLE countries tutakoma!
 
FB_IMG_1730878057200.jpg
 
Biden pamoja na uzee wake nadhani angekuwa competitive kushinda Kamala.
No, Biden pia angeshindwa.

Biden alipaswa atangaze mapema zaidi nia yake ya kutogombea tena kiti cha uRais ili kutoa nafasi kwa Watu wengine ambao ni wagombea sahihi & competitive ndani ya chama chake cha Democrats kuweza kuonyesha nia zao za kugombea.
 
Mkuu ipo hivi. Majimbo ya marekani (states) zimepewa idadi fulani ya electoral college kulingana na uwingi wa watu. Mfano carlifonia ina electoral collage 54. North Carolina 16, etc.

Mhombea anayeshinda jimbo husika kwa kura za wananchi pia anashinda hizo electoral college. Mfano kamala kashinda califonia ina maana pia kapata electoral college za carlifonia.

Kwa hivyo ni wananchi ndo huamua mshindi na sio hao wajumbe 538 wa electoral college.

Umeelewa?
Kifupi, wale wajumbe (electoral college) wanapiga kura kwa kuzingatia mshindi wa jimbo husika. Ndiyo maana hata kabla hawajapiga kura, mshindi anakuwa amejulikana.

Kazi yao kimsingi ni kuidhinisha au kurasimisha tu kile ambacho tayari kimeshafanyika.
 
Chombo gani wewe hapo BBC,CNN na aljazeera wanasema ameshinda majimbo mawili makubwa bado mengine wewe jamaa muongo sana

USSR
Florida watatangaza muda si mrefu na tayari ameshinda majimbo ya Pennsylvania, North Carolina na Georgia.

Hapo kabla alitabiriwa kushinda majimbo ya New York na Massachusetts.

Kwenye majimbo ya Nevada, Michigan, Arizona na Wasconsin anashinda.

Ndo maana saa hii yupo Palm Beach alihutubia na Kamala Harris ameenda nyumbani kujipumzisha.

Marekani ukiona wasema exit poll fulani katoka fahamu huyo mgombea ni mshindi.
 
Biden pamoja na uzee wake nadhani angekuwa competitive kushinda Kamala.
Wewe ndiye uliyenifanya nifuatile speech za Kamala, kuna siku ulisema hana kitu kichwani.

Nilifuatilia speech zake nyingi sana nikahakikisha kuwa ni mtupu...hayuko smart.

Sasa sijui nini ilikufanya uamini atashinda😂
 
Kipondo ili kiishe Ukraine hapaswi kujiunga na NATO na ndicho ambacho mrusi anacho kutaka kuhakikishiwa Hilo Kwa mikataba , so akiingia trump lazima atafanya Hilo cause alikuwa na mahusiano Mazuri na Putin kitendo cha Ukraine kutojiunga na NATO kikiafikiwa it means Russia watakuwa wameshinda dhamira yao ya kuzuia Hilo lisiweze kutokea
Hapo sasa kipondo kwisha Ukreni. Unapaswa kufurahi, wala si kulia.
 
Back
Top Bottom