Donald Trump Pamoja na kupigwa Risasi na Kujeruhiwa lakini hapiti kwenye vyombo vya habari kuichafua Marekani kama alivyofanya Lissu kwa Tanzania

Ndugu yangu kumbuka scenario ya kupigwa risasi Trump na Lissu ni mbili tofauti.

Aliyempiga risasi Trump alidhibitiwa muda ule ule na alijulikana fasta tu kwahiyo Trump atalaumu nani wakati mhusika alipatikana na alipigwa risasi akauawa?

Lissu alipigwa risasi mchana kweupe kwenye eneo la makazi ya wabunge na mawaziri tena kwenye eneo lenye ulinzi na hakuna uchunguzi wala taarifa zozote za kupatikana washukiwa.

Licha ya Lissu kuomba uchunguzi huru ufanyike hakuna aliyekuwa tayari kufanya uchunguzi. Katika mazingira kama haya akiilalamikia serikali atakuwa amekosea?
 
Kuna tofauti kubwa sana ktk haya matukio mawili.

. Lisu alipigwa risasi kwa maagizo ya rais wa nchi (dikteta jiwe), wakati Trump kapigwa risasi na mhuni tu.
 
Wewe ungeweza ? Yaani umebaki na kasikio kamoja Kama bundi alafu uanze kulandalanda kwenye korido za TV sijui redio eti kuituhumu serikali ?

Huu muda yupo chimbo wanasayansi wanaangalia namna ya kuunganisha kale kasikio kalikodondoka alafu wakaunge vizuri ndiyo atoke nje kuanza kelele 🙊
 
Kuna tofauti kubwa sana ktk haya matukio mawili.

. Lisu alipigwa risasi kwa maagizo ya rais wa nchi (dikteta jiwe), wakati Trump kapigwa risasi na mhuni tu.
Acha kuropoka.weka ushahidi wa maneno na kauli yako.
 
Una ushahidi dola inahusika .?
Yule kichaa jiwe:-
1. Alikataza wanaccm wenzake kwenda kumuona Lisu hospitali.
2. Alipiga marufuku kumchangia damu.
3. Kama kiongozi wa nchi, hakutoa pole kwa Lisu wala kutoa kauli ya kulaani tukio lile.
4. Alizuia uchunguzi kufanyika.
5. Alimvua ubunge.


Ndiyo maana kafa!
 
Bora ukae kimya unakaza fuvu ndiyo unadhihirisha ukilaza wako. Wewe elimu yako ya MEMKWA inatosha kuwasifia Mama Abdul,Makonda na Kafulila.
Akili yangu huwezi kuifikia hata kwa robo tu.mimi na wewe ni kama Mlima na kichuguu .wewe ni kichuguu tu kwangu
 
TRUMP NI MNYAMWEZI OG , LISSU NI MTU YA SINGIDA ....


KINGINE KAMA TAIFA LA TANZANIA , TUMUUNGE MKONO MHE. RAISI wetu SAMIA SULUHU HASSAN , nae ni kiongozi mwenye upendo wa dhati . Kiongozi bora ni yule mpenda watu kuanzia jamii yake paka ya jirani . Mungu bariki viongozi wetu wa Afrika . Mungu ibariki Tanzania
 
Hakuna hoja yenye mashiko ambayo inathibitisha maneno yako. Wewe ndiye kichaa.
 
Lissu hakuwai kuichafua Tanzania kama nchi, bali aliichafua SERIKALI ya Tanzania ya CCM chini ya Magufuli , pili neno kusema kweli si kuchafua bali alikuwa anaeleza yaliyo wazi,

Sera za Trump ni dhid ya SERIKALI ya Marekani chini ya Biden wala si dhidi ya Nchi ya Marekani,

1. Anakataa Ushoga
2. Sera mbovu ya mambo ya nje na Ushirikiano kimataifa
3. Matumizi mabovu ya walipa kodi wa Marekani kuendelea kutumika kufadhili Mapigano sehemu mbali mbali za dunia
4. Uhamiaji holela ambao haudhibitiwi vema! Na hii Biden amelegeza sana watu wanahamia hamia na kupewa Pesa na Marekani kwamba wanatafta asylum, wakati wananchi baadhi wana shida kibao


Britanicca
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…