Donald Trump Pamoja na kupigwa Risasi na Kujeruhiwa lakini hapiti kwenye vyombo vya habari kuichafua Marekani kama alivyofanya Lissu kwa Tanzania

Wewe na Lissu akli yenu ni moja tu.
 

Usilinganishe Marekani na shithole
 
Mwandishi hajawahi hata kukoswa koswa na manati kwa hiyo hoja yake ni VOID.
 
Ni kwa vile mtu akiwa mpumbavu ukimwita hivyo inaonekana umemtusi basi ngoja nisifanye hivyo.
Hivi kwa akili za kawaida na upo humu JF unaweza kulinganisha matukio hayo mawili?
Kwanza la Trump ona anafanya kampeni akilindwa na secret service na walichukua hatua immediately na uchunguzi unaendelea.
Pili Rais Biden amelaani mara moja tukio hilo.
Sasa njoo huku. Ulinzi makazi ya Lissu uliondolewa na wahusika hawahojiwi mpaka leo.
Hakuna faili la uchunguzi jeshi la polisi.
Rais aliyekuwepo alikataza hata watu kukusanyika kumuombea majeruhi na mengi zaidi kuonyesha uhusika wao.
Hivyo, thread hii ina haki kabisa kuitwa ya kipumbavu.
 
Kumbe makonda alimpiga risasi lisu hii taarifa mpya umeipata wapi?
 
Suala la Lissu lina utofauti mkubwa na la Trump. Ile serikali ya kidhalimu ilimnyima haki zake za matibabu na mbaya zaidi ilifika hatua hata wanaomwombea Lissu hadharani wanakamatwa. Wabunge wa CCM walishindwa kwenda kumuona hospitalini kwa kumuogopa mwenyekiti. Spika mpuuzi Job akamfuta ubunge Lissu kwa kudai ni mtoro wakati dunia nzima inajua Lissu ni mgonjwa. LISSU ALIONEWA. Kama unamsapoti Mama Samia lazima umpe maua yake jinsi alivyoshughulikia suala lake. Mama alienda hospitalini na kwenye uongozi wake ndo alikuja kulipa stahiki zote za Lissu.
 
Lissu ana haki ya kupiga kelele, vipi mpaka leo hakuna uchunguzi? Hakuna aliyeshikwa? Hata kama hawashikiki lakini hata wananchi hatupaswi kuelewa kilichotokea?
 

Mpigaji wa trup alipatikana akauliwa

Je wa lisu alipatikana?
 
Aliyempiga risasi Trump kapatikana na aliuliwa palepale, na amefahamika ni nani. Na serekali ya US imewajibika kwa upuuzi ule. Umeona serekali yao ikaanza kuweka mkwamo wa uchunguzi muhuni yule? Lisu aliichafua serekali, kwani ilikuwa safi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…