DP World kuanza kuendesha bandari ya Dar es Salaam tarehe 01 Novemba 2023

Sidhani kama DP World ama mawakala wao wa hapa nchini watakuwa na ubavu wa kuweka miguu yao kwenye bandari ya Dar!. Siamini kama hawajitaki!! Mungu wetu ni mkuu sana! Kama hawajitaki ngoja tuone!!
Wewe wasema
 
Tatizo sio uraia wa mtu tatizo ni aina ya vifungu vya mkataba ambavyo havina afya kwa Taifa!!
 
Kama kukufahamisha kuwa IGA ilishakufa wewe unaona ni ujinga, basi elewa wazi kuwa wewe ni mpumbavu.
Naamini unavyo vyanzo vyako serikalini, waulize wakupe ukweli kuliko kuona ufahari kutukana humu JF wakati unaweza ukapewa taarifa sahihi.

IGA iliyopitishwa bungeni ndio imezaa project contracts zinazokwenda kutumika kibiashara katika mkataba wa Tanzania na Dubai unaoanza kazi Novemba mwaka huu hapo bandarini.
 
Ingekuwa inatafuta kutuuza utumwani TPA wasingekuwa na jeuri ya kutangaza tender za magati namba nane mpaka kumi na moja.

Ingekuwa inatafuta kutuuza utumwani TPA wasingekuwa muda huu wanajiandaa kutangaza tender ya kupangisha bandari ya Tanga wakati michakato ya kuiendesha bandari ya Bagamoyo ikiwa inaendelea.

Huu upotoshaji mnaoufanya ndio unakuwa sababu ya mikataba yote kufanyika kwa usiri mkubwa kuanzia sasa na kuendelea.
 
Kwa nini niwe na "vyanzo serikalini", kwani siwezi kuwa serikalini mwenyewe?

Hata hivyo, haihitaji kuwa serikalini kujua mipango inayoendelea katika nchi hii.
Wewe hapa umekwishajulikana upo humu kwa kazi ya upotoshaji tu, tokea mwanzo. Baada ya IGA kubuma, sasa upotoshaji unahamia kwenye kuhusisha miradi yote inayofanyika na ujinga huo uliokataliwa na waTanzania.

Nirudie tena, hakuna uhusiano wowote kati ya IGA na miradi ya bandari inayoendelea sasa hivi. Acha upotoshaji huo.
 
Ingekuwa inatafuta kutuuza utumwani TPA wasingekuwa na jeuri ya kutangaza tender za magati namba nane mpaka kumi na moja.
Kwani kutangaza tenda kumeanzishwa na IGA. TICTS walipokuwa hapo hawakuingia kwa tenda?
Nirudie tena mara ya kumi, kukufahamisha kwamba, hakuna uhusiano wowote kati ya maswala ya Dubai na IGA yake na kazi zinazofanyika bandarini na kwingineko nchini. Hii ni mipango iliyokuwepo serikalini, na inaendelea kutekelezwa, kama huo mradi wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo. Achana na upotoshaji.
 
Tuombe uhai kwa Mungu, DP World anaanza kazi hapo bandarini Novemba mosi, roho mbaya yako haikusaidii chochote.
 
Hujui lolote bora ukae kimya tu kama kiburi chako kinakunyima uwezo wa kupata taarifa sahihi kutoka kwa watu mbalimbali.
 
Nimeipenda sana. Hata hivyo wamechelewa mimi nataka waje hata kesho. DP WORLD ni watu wema sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…