DP World wawepo Uingereza kwa wanaojitambua halafu Waswahili wa Tanzania tuikatae?

GENTAMYCINE ukiona muarabu kaoa uingereza, hiyo Ni sababu tosha na wewe umpeleke mtoto wako akaolewe na huyo muarabu, hata Kama umesikia huyo muarabu ana kesi mahakamani za kuwatendea watalaka wake ukatili wa kijinsia?
Ndio mlivyofundishwa SAUT!

You need your head examined.
 
Kwani tatizo ni DP au ni mkataba!? Kwani mkataba wa uingereza umeuona!? Hivi huko shuleni SI mliwasumbua Sana walimu!!!?
Watu hawakatai DP wanakataa mkataba!?
 
Inaonekana huko shuleni walimu wenu chamoto walikiona, watu hawakatai hiyo kampuni wanachokataa ni mkataba!!! Kwan mnatumia kiungo Gani kusikiliza!? Kinyeo au!?
Pili !! Mkataba wa UK na huu ni sawa!??
Duuu watu wagumu kuelewa kama " jiwe"!!
Halafu unakuta unautaka ukuu wa waliya!! Fxck yuuu
 
Nakwambia Kuna watu Wana vichwa vigumu kama jiwe!!
 
Mkuu roadmaster huyu bwege anataka u DED. si kwa uchawa huu wa kujitoa ufahamu.
 
wapo uingereza hadi marekani. hatubishi. tunachobisha, hao wenzetu wameweka mkataba kama huu wa kwetu? hata sisi tunapenda DP WORD walete uwekezaji. na ni dhahiri kwasababu wao wamedominate kwenye hiyo tasnia watakuwa na dili za meli nyingi, meli nyingi zitapita dsm port na mombasa itavurugwa mbaya. hiyo ni faida kwetu. hoja yetu ni vipengele vya mikataba, kwanza kutokuwa na ukomo na pili, kutokuturuhusu kujenga bandari ingine kwenye huo muda usio na ukomo. kwahiyo hatutaendeleza bandari ya bagamoyo, tanga, wala mtwara, ziwa tanganyika etc? hapo unasemaje?
 
Ndugu Roadmaster unadhani matusi yako ni mapya? Jitahidi kuwa mbunifu angalau kwenye matusi kwasababu ndo jambo unaloweza. Kasafishe hicho kinyeo chako ndo uje u-comment hapa
 
Hiyo Uengereza inaongozwa na CCM?
 
Wape na mkeo pia,wako vizuri.
 
Bhangi ni kweli haijawahi kumwacha mtu salama.kichwa kisichokuw na akili ni mzigo kwa shingo.
 
Unasema kwamba mkataba ulioletwa Tanzania au unaotaka kusainiwa ndiyo huo unaotumika pale Uingereza au sijakuelewa chief
 
Na Uingereza nako bandari zote mpaka inayofanana na ya Kibirizi nayo wamepewa DPW?
Uingereza nako wamepewa mkataba at infinity?
 
Je mkataba walioingia na Uingereza unafana na huu wa Tanganyika? Maana kuna uwezekanao mkubwa kwamba kuna vifungu ambavyo huku Tanganyika vimewekwa kwa ajiliya kuibana Tanganganyika, lakini kule kwa waingereza havikuwekwa maana walivikataa.
 
Mkataba wa Uingereza una masharti gani na mkataba wa Tanzania una masharti gani ?
Hoja ni masharti ya mkataba kwa nini mnahama kwenye hoja ya msingi mnatafuta visingizio kibao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…