DPP, TAKUKURU na Polisi: Wasikilizeni CHADEMA. Kuna jinai kubwa imetendeka

DPP, TAKUKURU na Polisi: Wasikilizeni CHADEMA. Kuna jinai kubwa imetendeka

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kuna jinai kubwa imetendeka.

Kuna uvunjaji mkubwa wa Katiba na Sheria za nchi umetokea. Mhusika lazima abainishwe na achukuliwe hatua kali za kisheria. Mambo yako hivi: CHADEMA wamesema na wanaendelea kusema kuwa hawakuwasilisha Orodha ya Wabunge wa Viti Maalum NEC. Hiyo ni kauli ya Katibu Mkuu wa CHADEMA ambaye ndiye mhusika wa kupeleka majina na mjazaji wa Fomu za kisheria.

Katiba imevunjwa, sheria zimevunjwa. Orodha haikupelekwa. Orodha aliyopewa Spika, kuiamini na kuwaapisha jana ameitoa wapi? Anzeni na Spika. Kama ameipata Orodha kutokea NEC, NEC wamepewa na nani? Nendeni na NEC. Halafu, wote 19 walioapishwa jana wahojiwe na waeleze, pamoja na mambo mengine, waliambiwa na nani kuwa wameteuliwa kuwa wabunge. Waseme waliambiwa kwa njia gani.

Hapa kuna mambo ya pesa za umma. Kuna mambo ya katiba na sheria. Hapa kuna mambo ya jinai kubwa. DPP, TAKUKURU na Polisi, wasaidieni watanzania. Lindeni pesa zao, katiba yao na sheria zao. Mtaheshimiwa na kuthaminiwa. Wakati ni huu!

Mwaka 2020 kulikuwa na uchafuzi mkuu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam.
 
Umeandika vizuri ila kwa speed ya ajabu.

Twende kwenye uhalisia wa mfumo wetu huu huu mbovu, kuna wafungwa wa kisiasa watano na juzi wametolewa mmojawapo amekula kiapo jana, tuhoji hapo kwenye kuwatoa na haraka kapelekwa kula kiapo, kuna nini kimejificha, je jinai haikuanzia hapo?

Kuna msemo unasema "Mfumo ukiharibika hata waliomo wameharibika" serikali inajinasibu kufanya uchaguzi mzuri toka kuwepo kwa taifa la Tanganyika kama si Tanzania, ila wale wanaotakiwa kuwepo siyo waliopo ila wanalazimisha kuwekwa wasiokuwepo kwenye ubunge.

Hakuna msimamizi wa sheria za nchi atakayekuwa tayari kusikiliza kilio cha mwananchi huko nje 'eti' katiba na sheria imevunjwa na muhimili wakati kila mtu ana hofu na nafasi yake.
 
Huwezi kumfukuza mtu bila kumsikiliza lazima wasikilizwe hata kumfunga mtu kuna process
Basi tulieni kwanza mpaka mpate kibali cha mabosi wenu,
Narudia hapa tena, muwe na kiasi kwenye midomo yenu.
Haitapita wiki tu mtarudi hapa na kuwaita haohao akina Mdee makamanda.
 
B
Basi tulieni kwanza mpaka mpate kibari cha mabosi wenu,
Narudia hapa tena, mue na kiasi kwenye midomo yenu.
Haitapita wiki tu mtarudi hapa na kuwaita haohao akina mdee makamanda.

Mataga bana[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Wanaopaswa kulaumiwa ni hao waliokwenda kuapa, hizi kelele za dpp, polisi na tume ni kujaribu kukuumbatia mbuyu tu. Hawa akina mdee ni watu waliokaa kwenye mfumo wa chama chao kwa muda mrefu, inapofikia hatua anafanya hivi ni kwa aidha utashi wake au kuna mkulungwa yupo nyuma yake.

Tunashupava shingo zetu mwisho wa siku tutakuja kuvunja shingo zetu ndiyo tuelewe.
 
Chadema wasanii wasanii

Ngoma hii wameibariki undergroundly!

Kwanini Tangu Uchaguzi Mkuu umeisha hawajakutana na kutoa msimamo rasmi wa chama kama wataridhia Wabunge wa viti maalum au laaa!


Mwanasiasa wa mwisho mzalendo Tanzania alizaliwa 1922, zaid ya hapo ni Usanii mtupu
 
Bila kukwepesha ukweli hapa naona kuna 'usanii' viongozi wa CHADEMA wamefanya au lugha nyepesi kuna mtu 'kazungukwaa', haiingii akili kusema eti hao wamama wote19 kununuliwa na ma - CCM, kuna mchezo viongozi wa CHADEMA wanatuchezea na kutu hadaa wapiga kura, ila ni suala la muda tuu kujua ukweli.
 
Watawala wetu sasa hawaoni aibu tena kuvunja Katiba na kufuata sheria zinazoiongoza nchi.

Ndio maana nikisoma mahojiano aliyofanyiwa Matiko na moja ya chombo cha habari nae anaonesha alibebwa tu toka pasipojulikana akaenda kuapishwa Dodoma.

Japo Chadema kama chama kikuu walitakiwa wawe na intelijensia ya kun'gamua hilo mapema, hizi tetesi zilishakuwepo muda.

Pamoja na yote hayo, chama kinatakiwa kuwachukulia hatua kali wahusika wote wa huo mchezo wakithibitika kukiuka makubaliano, wakianza na viongozi wao Mdee na Bulaya, kwasababu hilo lipo ndani ya uwezo wao.

Baada ya hapo ndio waripoti hiyo jinai polisi, tuone kama Sirro anaweza kujitutumua kufanya chochote, kwasababu inaonekana hao wasaliti hata ulinzi wa serikali wamepewa.
 
Back
Top Bottom