Dr. Mwele Malecela: Asiyekuumba, kukuumbua hawezi

Dr. Mwele Malecela: Asiyekuumba, kukuumbua hawezi

Aliyekua Mkurugenzi Mkuu wa NIMRI Bi.Mwele malecela ameposti katika akaunti yake ya twitter maneno haya. Nadhani huu ni mrejesho baada ya tamko la Mwenye nyumba kuwa Daktari Mwele malecela alikua anatumika na MABEBERU.


View attachment 1223939
View attachment 1223982
View attachment 1223983

=====

RAIS John Pombe Magufuli, amesema moja ya sababu kumtumbua aliyekuwa Mkurugenzi wa Taasisi ya Tafiti za Kiafya NIMR, Mwele Malecela, ni kiongozi huyo kutoa taarifa ambazo hazikuwa sahihi kuhusiana na ugonjwa wa Zika.

Magufuli ametoa kauli hiyo akiwa mkoani Songwe, wakati alipofika kwenye ziara ya kikazi na kufanikiwa kuzindua kiwanda cha kahawa kilichojengwa na wajasiriamali wa Tanzania, ambapo amesema moja ya mambo ambayo yalipelekea kumtoa kwenye nafasi hiyo Malecelea ni kutangaza ugonjwa.

“Maneno huwa hayaishi, kuna wakati walitangaza kuna ugonjwa wa Zika nchini Tanzania, alipotangaza hivyo wakati mimi najua haupo nilimfukuza saa 7:30 usiku, wala hakuna cha Zika iliyotokea. Baada ya wiki moja wakamteua akawa bosi wao, hii ilionyesha alitumwa kusema aliyoyasema; hizi ni mbinu za kibeberu,” amesema Rais Magufuli.

Dada Mwele Malecela ni binti wa Mzee John Samwel Malecela ambaye amewahi kuwa Waziri Mkuu wa nji hii lakini pia aliwahi kushika nyadhifa mbalimbali za Uwaziri katika Wizara tafauti tafauti enzi za Mwalimu na wakti wa Mzee Ruksa.
Jambo ninalofikria hapa ni vipi Bwana John Pombe Magufuli anaweza kuthubutu kumtukana, kumdhalilisha Dada Mwele kiasi hichi kisa ugonjwa wa ZIKA..?? Kumdhalilisha au kumtukana mtoto wa Mzee Malecela ni sawa na kudhalilisha na kumtukana Mzee huyo..!!Hivi Mzee Malecela anajisikiaje anapomwona Magufuli akiongea kwenye runinga au redio?

Mtu ulishamtumbua...lakini ana elimu yake ya Kimataifa na kaajiriwa huko kwa sifa alizonazo halafu Rais unaanza kuropoka eti MABEBERU ndio waliomtuma kusema Tanzania kuna ZIKA....!!! Hawa Mabeberu unaowasema ni Shirika la Afya Kimataifa (WHO-World Health Organization)linaloshughulikia maswala ya Kiafya dunia nzima...!!!

Swali la Kufikirisha : Hivi Rais Magufuli akishtakiwa Mahakamani na Shirika la Afya Duniani(WHO)kwa kulidhalilisha na akaambiwa alete USHAHIDI USIOTILIWA SHAKA ya kwamba Dr. Mwele Malecela alitumwa na WHO(Mabeberu-according to Magufuli)kutamka kwamba ZIKA ipo Tanzania na ndo maana wakampa kazi ataweza???
 
Na ile nyingineje? Sihitaji jibu kwa sababu umekwishatoa jibu katika mstari huo mmoja.
Huyu anatafuta sifa kwa kuwafukuza kazi wengine hata kama hawana makosa?
Ile nyingine imeondoka na uhai wa mtu
 
Binafsi naamini Raisi naye anapenda kuanzisha Mijadala isiyo na tija.

Kwani ni lazima kusema kila Jambo linalomfurahisha au kumkera Sana?

Suala la Dk. Mwele lilishapita na hakutakiwa kulizungumzia tena kwa kuliunganisha na taasisi za kimataifa ambazo kesho na kesho kutwa tutahitaji msaada wao pale ambapo magonjwa ya mlipuko yatakapo tokea.

Jana nimeona BBC NEWS habari kubwa ilikuwa ni Raisi kumpongeza Ofisa aliye charaza wanafunzi viboko.

Huu nao pia ni mjadala mkubwa ambao ameuanzisha na hauna tija. Chanzo cha mjadala huu ni hotuba yake aliyoitoa Jana.

Mh. Raisi ajitahidi kuwa na kifua cha kuifadhi mambo hata kama yanamfurahisha au kumsikitisha.
Binafsi nimekuelewa kwa uzuri kabisa mkuu.
 
Hayo ma dessertation watu wengi wanayo swala la uwepo kwenye google au laa....is all about technology.....
but msifate mkumbo kwa mambo ya kijinga...
yule dada aliharibu sana....
muda ni mwalimu mzuri sana....
huo ugonjwa wa zika hatujauona...
Si mnatumia nguvu kuficha
 
Katika hili Magu is right mbona hako kagonjwa alikosema mbombezi wa magonjwa hakakuendelea? Au aliondoka nako? Maana mwele dr alikuwa sahihi tungeendelea kusikia ama kushuhudia watu wakifa. Lakini kimyaaaa
Si mnatumia nguvu kuficha. Mmebana kila kona na miphd yenu uchwara
 
Uko sahihi mkuu lakn kwa hulka za wanadamu huwa ni ngumu mno kushinda hali kama ile, muda mwingine tunaumizwa ama kufurahishwa na ishara ya haya ni mtu akiumizwa analia, anaweza pia kupigana hata ngumi yote hii ni ishara ya disscontent lakn pia akiwa na furaha atacheka, kutabasamu ama hata kuimba wimbo wenye kuonyesha hali ile, kwa mh Rais na tukio alilolitenda Dr Mwele bado inajimuktadhanisha na maelezo yangu haya na ukweli hakuna ugonjwa wa ZIKA uliokuja kutukia sasa swali tulitakiwa kujiuliza je zika aliizika dr mwele? Kwanini hakukuwa na hata dalili baada ya taarifa yake hyo na kutumbuliwa kwake? Kwanini Rais asionyeshe hasra zake kwa alichokifanya huyo mtumishi wa umma?

Muda mwingine tunashabikia ujinga tu lakn ukwel wa habar hii tulipaswa kujiuliza swali hili tu kwamba huu ugonjwa ulikuwepo kweli? Kwann ulipotea?
Umesomeka vizuri mkuu.

Kuna wakati huwa najiuliza maswali kuhusu weledi wa hawa wataalamu. Unapokuwa mkuu wa taasisi fulani lazima uwe na uwezo wa kupima athari za tamko lako kwa maslahi mapana ya nchi. Huwezi kutangazia dunia kuwa nchi yako ina ugonjwa fulani Just kwa kesi moja au mbili.
Ukiangalia tangu Dr. Mwele atangaze kuwa kuna Ugonjwa wa Zika mpaka sasa hakuna kinachoendelea kuhusu huo ugonjwa. Je yeye aliondoka na huo ugonjwa ? Au tuseme wagonjwa wa zika wamefichwa na serikali? Magonjwa kama yapo yataonekana tu huwezi kuficha kwa namna yoyote ile.
Juzi Kati WHO + US wanalazimisha Tanzania itangaze kuwa kuna Ebola eti kuna mtu mmoja amekufa kwa huo ugonjwa. Hivi tangu waanze kulazimisha mpaka sasa kuna wagonjwa wangapi wametokea? Je Ebola inaweza kufichwa chumbani?
Binafsi naamini kama hayo magonjwa yapo yataonekana tu muda ukifika lakini wasilazimishe nchi itangaze hata kama hizo issue bado. Tuzidi kumwomba Mungu atuepushie na hayo majanga
 
Subiri uzae taahira ndiyo utajua Zika ipo au haipo
Nimesuburi sana. Naona hakuna kitu. Hivi kusoma ni karibu tu halafu ndio tunakuwa wasomi? Hatutumii akili zetu?
 
Umesomeka vizuri mkuu.

Kuna wakati huwa najiuliza maswali kuhusu weledi wa hawa wataalamu. Unapokuwa mkuu wa taasisi fulani lazima uwe na uwezo wa kupima athari za tamko lako kwa maslahi mapana ya nchi. Huwezi kutangazia dunia kuwa nchi yako ina ugonjwa fulani Just kwa kesi moja au mbili.
Ukiangalia tangu Dr. Mwele atangaze kuwa kuna Ugonjwa wa Zika mpaka sasa hakuna kinachoendelea kuhusu huo ugonjwa. Je yeye aliondoka na huo ugonjwa ? Au tuseme wagonjwa wa zika wamefichwa na serikali? Magonjwa kama yapo yataonekana tu huwezi kuficha kwa namna yoyote ile.
Juzi Kati WHO + US wanalazimisha Tanzania itangaze kuwa kuna Ebola eti kuna mtu mmoja amekufa kwa huo ugonjwa. Hivi tangu waanze kulazimisha mpaka sasa kuna wagonjwa wangapi wametokea? Je Ebola inaweza kufichwa chumbani?
Binafsi naamini kama hayo magonjwa yapo yataonekana tu muda ukifika lakini wasilazimishe nchi itangaze hata kama hizo issue bado. Tuzidi kumwomba Mungu atuepushie na hayo majanga

Soma hii babu kuhusu ugonjwa wa Zika maarufu kama ZIKA FEVER.
https://en.wikipedia.org/wiki/Zika_fever
Katika maelezo hayo ya mtandao wa Wikipedia wataalamu wanasema dalili za Homa ya Zika zinafanana sana na Homa ya Dengue. Hivi karibuni kumekuwa na mlipuko mkubwa sana wa Homa ya Dengue kwa Jiji la Dar na mikoa jirani kama Tanga. Je, kama ni kweli dalili za homaya Zika na Dengue zinafanana kwanini tusitile shaka kuwa hawa wanao ambiwa ni wagonjwa wa Dengue ni wagonjwa wa Zika? Kama nchi hii leo watu wanauawa, wanapotezwa na wanashambuliwa kwa risasi mchana kweupe lakini Serikali hii inakuja na majibu rahisi ya WATU WASIOJULIKANA, kwanini tusiamini kwamba hata hii DENGUE ndiyo hiyo ZIKA? Never trust a Government of Liars like the one we have it now...!
 
Acha kudanganya watu wewe..!!
Hivi Mkurugenzi wa Hali ya Hewa kila siku wanapotangaza UTABIRI WA HALI YA HEWA huwa lazima kwanza aongee na Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi? That is unnecessary bureaucracy so to speak..!!!
Mkuu unaniaibisha, unalinganisha hali ya hewa na utangazaji wa ugonjwa!, kuutangaza mlipuko wa ugonjwa ni kazi ya waziri wa afya. Dada Mwele alipaswa kwanza kuongea na waziri wake ndipo atangaze kama zika imeingia Tanzania au la.
 
Back
Top Bottom