Elections 2015 Dr. Pombe Magufuli, Rais mteule wa Tanzania awamu ya 5

Elections 2015 Dr. Pombe Magufuli, Rais mteule wa Tanzania awamu ya 5

Dr. John Pombe Magufuli ametangazwa rasmi kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya 5 baada ya kuongoza kwa kupata kura 58.46%.


attachment.php



Lubuva: Kwa kuwa mheshimiwa Dr. Magufuli, John Pombe Joseph wa CCM amepata kura nyingi zaidi kuliko mgombea mwingine yeyote, kwa niaba ya tume ya taifa ya uchaguzi na kwa mujibu wa vifungu vya 35(e), 35(f) na 81(b) vya sheria ya taifa ya uchaguzi sura 343.

Ninatangaza rasmi matokeo ya uchaguzi ya urais wa mwaka 2015 kwamba

  1. Mheshimiwa Magufuli John Pombe Joseph amechaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania
  2. Mheshimiwa Samia Hassan Suluhu amechaguliwa kuwa makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.
Asanteni kwa kunisikiliza

Hongera rais mteule sasa kazi tu tunataraji utawatumikia watz wote kama ulivyoahidi bila kujali itikadi zao.na hongera lowasa na ukawa yako umeleta ushindani wa kweli hadi wastaafu wakashiriki kwenye kampeni na nyie ni washindi mmeongeza % zenu za ushindi kubalini matokeo rudini mkajipange tujenge tz yetu
 
Mungu akuongoze akupe zaidi hekima akili na maarifa ukaiongoze nchi yetu ipasavyo.
 
ARUSHA: Mji kama umetiwa ganzi wananchi hawaamini nini kimetokea, kauli za wengi ni 'basi tena'. Ila mitaa mingi ni kama picha inavyoonesha kwa mbali.
 

Attachments

  • 1446126437539.jpg
    1446126437539.jpg
    96.2 KB · Views: 351
Ukweli ni kwamba Tanzania imehukumiwa miaka mingine mitano ya Maisha magumu, Umasikini, kuporomoka kwa elimu, kuporomoka kwa shilingi, Mfumuko wa bei, kupanda kwa deni la taifa, kufutika kwa tembo wetu, kuporwa madini na gesi yetu, Ufisadi papa ulio juu ya sheria n.k. Ole wetu watz, ni nani aliyetuloga.

Acha kuwa mpuuzi mkuu. Unadhani wewe ndio pekee una akili kuliko mamilioni waliofanya maamuzi haya. Again, acha upuuzi na dharau kwa wananchi.
 
Hakika toka moyoni mwangu, Magufuli si rais wangu bali ni rais wa ccm. Ila kwa katiba iliyopo atanitawala kilazima. My heart to cdm and ukawa, shall remain.

Hata mimi hapa Ubungo wamechagua limbunge linafiki li-kubenea la chaggadema silipendi na kibaya zaidi na diwani ni chaggadema yaani ni kama naishi motoni.Nayachukia sana lakini ntafanyaje ndio demokrasia walio wengi wanaamua na wachache mnakaa kimya maana wanasema penye wengi hapaharibiki neno na sauti ya wengi ni sauti ya Mungu
 
Show zako za OZ zimeleta matokeo chanya.. Naamini utakua na faraja sana kwa malengo yako kutimia...

Sio vibaya ukituwekea links ya shows zote za OZ.
 
Baada ya kutangazwa kwa j.p.magufuli kuwa rais wa 5 wa tanzania leo tarehe 29.10.2015, ndio umekuwa mwisho wa ule umoja wa mashaka wa ukiwa. Kwani umoja huu ulijengwa kwenye kuaminishana kuwa fulani akiwa rais basi na sisi tumeula na kupiga dili za kufa mtu. Sasa wataanza kutimuana na kila mmoja kujifanya hamuamini mwenzake.

wataanza kumkumbuka Dr. Slaa ambaye aliposhindwa uchaguzi 2010 alitumia nguvu nyingi sana kukijenga chama.

tofauti na huyu mzee alishasema akishindwa anarudi kwao kuangalia mifugo yake
.
 
Wakuu

Baada ya matokeo yaliyompa ushindi 'wanaoujua' Dr John Magufuli kuna juhudi za kuwakatisha tamaa wana mabadiliko.

Kamwe sitawachukia Ukawa kumpa tiketi Edward Lowassa,matokeo yametutoa hatua moja mpaka nyingine,ntaendeleza harakati za chama ktk eneo langu kama kawaida.

Ntaendelea kuipenda chadema kama mbadala wa ccm,nafurahi wameongeza idadi ya wabunge mapambano yaendelee.

Nichukue fursa hii pia kumpongeza Freeman Mbowe..tunakuamini na endelea kuongoza chama kwani idadi ya madiwani na halmashauri tulizopata imekuwa maradufu.
 
cjawah kuona rais anatangazwa wananchi wapo kimya Yani dar kimya kama kuna msiba wa kitaifa hv mfano lowassa ndo angekuwa ndo mshind cjuh ingekuwaje mda huu
 
Hayo ndio maneno ya mwana demokrasia aliye komaa.
Kudos kwako pro UKAWA.
 
Hata mimi hapa Ubungo wamechagua limbunge linafiki li-kubenea la chaggadema silipendi na kibaya zaidi na diwani ni chaggadema yaani ni kama naishi motoni.Nayachukia sana lakini ntafanyaje ndio demokrasia walio wengi wanaamua na wachache mnakaa kimya maana wanasema penye wengi hapaharibiki neno na sauti ya wengi ni sauti ya Mungu

haaaaa haaaa
 
Na wengine baada ya 2010 walikuwa wanasema Slaa ni Rais wao...Rais wa mioyo ya watanzania...

Kazi kwelikweli...
 
Back
Top Bottom