Elections 2010 Dr. Shein aibuka kidedea; kuiwakilisha CCM urais Zanzibar 2010

Elections 2010 Dr. Shein aibuka kidedea; kuiwakilisha CCM urais Zanzibar 2010

Na mwandishi wetu.
Emanuel Sukariguzi

Habari kutoka Dodoma zinasema kuwa dalili zote zinaonyesha kuwa makubaliano ya ndani kabisa ya CCM ni kumpitisha Dr Shein.

Shein ambae alikuwa amezingirwa na wapinga maendeleo yake huku akishutumiwa na kukandamizwa kwa sababu mbali mbali ikiwemo ile ya kuonekana kuwa ni mpemba.Hali iliyowafanya wapenda maendeleo wa Zanzibar akiwemo Dr Salmini Amour kutoikubali na kulazimika kuhamia upande wa Shein katika kumuunga mkono.

Pia hali iliyokuwa imezingira wakutanaji wa mkutano huo ni kule kuhudhuriwa na wakuu wa walioshiririki Mapinduzi ya kumuondoa mkoloni mwarabu ,Mheshimiwa Moyo na Mheshimiwa Natepe ,waliosikika wakieneza umoja wa kulaani sumu ya upemba na uunguja kwa kuwataka wapiga kura kutokumchagua yeyote yule anaeonekana ni mwenye kupandikiza chuki za aina hio.

[FONT=ArialMT, sans-serif]Minong'ono ya ndani inadai sababu kubwa ya kutaka Dk. Shein ateuliwe kugombea nafasi hiyo, kwanza ni kudumisha umoja na mshikamano visiwani na pili kutaka kuendeleza yale ambayo tayari yamefanyika[/FONT].

Habari ambazo zimepatikana kutoka ndani ni kuwa tayari uhakika wa ushindi wa Shein umeshahakikishwa iliyobaki ni utekelezaji tu.

Shein bwana naye kazidi uzezeta bana...we mtu hata mkwara hawezi kupiga sa rais gani wa ivo..apewe bilal tu kieleweke
 
Ninacho shindwa kuelewa hapa ni jinsi watu wanaunga mkono Dr.Shein kupitishwa na kundi linalotaka hawe "puppet" wao na wanawapinga wale watakao leta changa moto na kundi la ccm bara kama dr.bilal.


Kutokana na watu wengi humu kuunga mkono kupandikiziwa wagombea kutokana na maslahi ya kundi binafsi na sio maslahi ya nchi basi tuwache unafiki wa kuuponda uongozi wa Kikwete kwani yeye pia kapata nafasi hili kutekeleza maslahi ya kundi binafsi amablo leo hii humu watu wanaliunga mkono kumpa nafasi Shein.


Mimi ningependa Dr.Bilal au Vuai wapite hili tuone hio tofauti watakayo leta hiwe kwenye muungano au chochote kwani bila kupingana mabadiriko hayatapatikana kamwe.Tumekuwa waoga sana wa upande wa pili wa shillingi hata kuutizama tunaogopa na ndio maana hatupigi atua yoyote hile.
 
Shein bwana naye kazidi uzezeta bana...we mtu hata mkwara hawezi kupiga sa rais gani wa ivo..apewe bilal tu kieleweke

Mzee wa Mikasi Dr Shein hapendi makuu na hana kabisa damu ya ufisadi na hashirikiani nao utafikiri si mwanaCCM! Hivi bara itaacha lini kuwachangulia raisi kule visiwani?
 
Mkulima.. lakini ni Mkutano Mkuu wa CCM ndio unapiga kura kumchagua nayo ni kesho.. maana NEC ilikuwa ichuje majina matatu tu au ndio wamebadili utaratibu tena?
Si kweli MKJJ majina matatu yamechujwa na CC, NEC inachuja jina moja kati ya matatu kazi ya mkutano mkuu ni kupiga kura ya ndiyo au hapana kwa jina litakalopelekwa na NEC, si unajua jina likishapita NEC mkutano mkuu ni kama stamp tu. Msikilize Chilighati alivyosema leo alasili alipoongea na waandishi wa habari,

KAMATI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC - CCM) leo imepitisha majina ya wana CCM watatu kati ya 11 waliokuwa wakiwania kugombea urais Zanzibar.

Waliopitishwa kuwania nafasi hiyo ni Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Ali Mohamed Shein, Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Shamsi Vuai Nahodha, na Waziri Kiongozi Mstaafu wa SMZ, Dk Mohamed Gharib Bilal.

Katibu wa Uenezi na Itikadi wa CCM, John Chiligati, amewaeleza waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa, wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho watapiga kura jioni hii kumchagua mmoja atakayepeperusha bendera ya CCM katika Uchaguzi Mkuu ujao.
 
Mzee wa Mikasi Dr Shein hapendi makuu na hana kabisa damu ya ufisadi na hashirikiani nao utafikiri si mwanaCCM! Hivi bara itaacha lini kuwachangulia raisi kule visiwani?

hahaaaa nimekupata mkuu..ila naye achangamke bana..kapooza utadhani mgonjwa
 
Taarifa ya nini wakati ni Shein? Unategemea Shein ataanguka? MAKAMU WA RAIS alipokwenda kuchukuwa form mlifikiri wanabahatisha? Mambo yooooooooooooote yalishaisha kinachofanyika sasa ni formalities tu

Hapo ndipo nilipowashangaa wengi sana ,makamo wa kwanza wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano Tanzania ,wazuke akina Bilali na Pandu ,basi msubiri jawabu tu ,nawambia kuwa SHein anashinda tena kwa kura nyingi kama si zote ,ao wengine ndio wanaoingizwa kitanzini bila ya wenyewe kujua kama wanajua wangelijitoa na mapema ili kulinda kuwepo kwenye siasa.
 
Mh! Siasa ni Ngumu jamani poleni sana wanasiasa
 
Nasikia Augustino Lyatonga ni mmoja kati ya Wageni Waalikwa jamani
 
Na mkumbuke tu kuwa Shein hana shida ya URAISI wa Zanzibar ,ila kunani kamammesoma ippmedia leo mngeweza kuona sababu ya Shein kusimikwa katika kugombea Uraisi wa Zanzibar.
 
hivi huyu Lyatonga yupo bado ,,teh teh teh .mzee wa kiraracha ananipaga raha sana.hasa pale alipoomba msamaha bungeni duuuuh
 
Nasikia Augustino Lyatonga ni mmoja kati ya Wageni Waalikwa jamani

wewe unafurahisha baraza!!! Ila nimeshangaa Guest wapo karibu 200 mh!!! hawa ni akina nani waandishi wa habari? Wanasiasa au viongozi wa nchi? au wazawa?
 
Kwa hiyo nini future ya Karume (raisi wa sasa wa Zanzibar)?

Future ya nini tena wakati atakuwa mstaafu, kwani future ya mstaafu ni nini. au mpaka afie ofisini? ameshakuwa rais kwa miaka kumi that is enough. Kwani future ya Salmini ilikuwa nini?
kipipili hiyo post yako imenifanya nicheke sana, kweli mtu umeshakuwa rais unatafuta future gani tena zaidi ya kuwa rais mstaafu LOL!!! kweli hii ndiyo JF.
 
wewe unafurahisha baraza!!! Ila nimeshangaa Guest wapo karibu 200 mh!!! hawa ni akina nani waandishi wa habari? Wanasiasa au viongozi wa nchi? au wazawa?

Kwi kwi kwi! Wewe Ndiye nini maana it sound like " Wewe unafurahisha Bara Barasa"
 
wewe unafurahisha baraza!!! Ila nimeshangaa Guest wapo karibu 200 mh!!! hawa ni akina nani waandishi wa habari? Wanasiasa au viongozi wa nchi? au wazawa?

Watakuwa Viongozi wa NJI
 
kipipili hiyo post yako imenifanya nicheke sana, kweli mtu umeshakuwa rais unatafuta future gani tena zaidi ya kuwa rais mstaafu LOL!!! kweli hii ndiyo JF.
Yakhe huyo sio kwamba future yake ina-husisha mambo ya pesa, bali madarakaaaaa, baba alikuwa mwanzilishi wa Muungano, hivyo basi anatakiwa akae mwendo tayari kuchukua huraisia wa Muungano kunako 2015.
Hizi gheresha za Lau. Membe, EL, Prof, zitaisha kwenye ugombea mwenza.
Upo hapo
 
Ninacho shindwa kuelewa hapa ni jinsi watu wanaunga mkono Dr.Shein kupitishwa na kundi linalotaka hawe "puppet" wao na wanawapinga wale watakao leta changa moto na kundi la ccm bara kama dr.bilal.


Kutokana na watu wengi humu kuunga mkono kupandikiziwa wagombea kutokana na maslahi ya kundi binafsi na sio maslahi ya nchi basi tuwache unafiki wa kuuponda uongozi wa Kikwete kwani yeye pia kapata nafasi hili kutekeleza maslahi ya kundi binafsi amablo leo hii humu watu wanaliunga mkono kumpa nafasi Shein.


Mimi ningependa Dr.Bilal au Vuai wapite hili tuone hio tofauti watakayo leta hiwe kwenye muungano au chochote kwani bila kupingana mabadiriko hayatapatikana kamwe.Tumekuwa waoga sana wa upande wa pili wa shillingi hata kuutizama tunaogopa na ndio maana hatupigi atua yoyote hile.
Sasa mzee wa Arsenal kama wao ni puppets wa Shein ina maana wewe kwa vile unamtaka Bilal ni puppet wa Bilal.
 
Back
Top Bottom