Pre GE2025 Dr. Slaa: Ni dhahiri Milioni 150 zilizotolewa na Rais Samia zimeingia kwa sura ya kampeni, anayebisha abishe!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hapa napingana na Dr. Slaa huwezi mpangia mtu nini cha kutoa, atoe wapi na atoe kiasi gan?
 
Kwani hakuwa na haki ya kukisema CHADEMA? CHADEMA si ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo?

Kwani hakuwa na haki ya kufanya kampeni dhidi ya CHADEMA na Lowassa? Mbona hiyo ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania? Unataka kulazimisha kila Mtanzania alazimishe kumkubali Lowassa na CHADEMA? Mbona mpaka sasa historia imemuonesha Slaa alikuwa sawa, Lowassa karudi CCM, na watu wengi ndani ya CHADEMA wanajuta kumkubali kuwa muwakilishi wa chama baada ya shutuma nyingi za rushwa?

Unajuaje kuwa Slaa anapinga mchango wa sababu ya KKKT/RC n si kwa sababu hii ni hongo inayoweza kuchukua sura ya kisiasa? Mbona hata mimi ambaye sipo KKKT wala RC naliona hilo?

Kitu cha muhimu ni kama kasema ukweli au si ukweli, hiyo ndiyo hoja, hizo habari za unafiki wewe huwezi kuujua ubongo wa mtu.

Jadili hoja, usijadili mtoa hoja. Unapojadili mtoa hoja badala ya hoja, unafanya logical fallacy ya ad hominem.

Unajionesha kuwa ni mtu uliyefilisika kihoja, huna hoja, unabaki kumshambulia mtoa hoja kama mtu binafsi.
 
Mbowe ni CCM B, ukimsema vibaya wapuuzi wanakushambulia. Huwezi kuona huo upuuzi unafanywa na Lissu au Heche never!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…